Kwanini Marekani wanaihofia sana kampuni ya HUAWEI?

Kwanini Marekani wanaihofia sana kampuni ya HUAWEI?

Xi Jinping

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2023
Posts
8,102
Reaction score
23,693
Tangu 2012 Marekani imekuwa ikifanya juu chini kuiangusha HUAWEI bila mafanikio.

Hivi karibuni HUAWEI ilizindua A.I chip ya hali ya juu iitwayo Ascend 910C ambayo imekuja kuichallenge ile ya NVIDIA.

Kuna wasiwasi unaoongezeka kwa Marekani kwamba hivi karibuni China itakuwa ikiuza AI processors hizo nchini China na masoko ya nje ambapo itashindana na zile za NVIDIA na za makampuni mengine ya Marekani.

Kutokana na ujio wa processors hizo, May 13 2025, U.S Chamber of Commerce na U.S Bureau of Industry and Security wametoa tangazo la kitisho kwa mataifa mengine duniani kwamba;

Wasitumie HUAWEI Ascend processors wakidai kuwa zimetengenezwa kwa kutumia teknolojia ya Marekani.

Lakini cha kushangaza hivi karibuni CEO wa NVIDIA Jensen Huang alipoulizwa:
“How far is China behind the US in AI?” hili ndio jibu lake


“China is not behind! Remember that 50% of world’s best AI researchers are Chinese and many of those work at U.S.-based AI labs. This is a long race.
It would be a tremendous loss to miss the Chinese AI market."

Nvidia CEO Jensen Huang
Pro-West husema Marekani iko mbele kwenye teknolojia imeizidi China.

Ok well tufanye imeizidi sasa kwa nini Marekani imekuwa ikiogopa high tech goods za China wanazodai zina low quality zisipenye soko la dunia au Marekani?

Marekani inahofia Ascend processors zikiingia soko la dunia, NVIDIA can't win a price war with HUAWEI.
 
Kwa nini YouTube, Google, WhatsApp, Facebook na X/Twitter zimepigwa pini China??
 
Kwa sababu ni kampuni kubwa ya kiteknolojia China na duniani kwa ujumla.
 
Naunga mkono hoja China ndio yupo juuu na propaganda za kuwadumaza Wachina zimeshindwa !!!!!

China ni kila kitu..

Wazungu wajiandae kwenda kupewa kazi za kufua nguo za Wachina mana wamedhidiwa Elimu. !!!!

Shubamit!!! Ulimwengu umebadilika Yajayo yanafurahisha !!
 
Naunga mkono hoja China ndio yupo juuu na propaganda za kuwadumaza Wachina zimeshindwa !!!!!

China ni kila kitu..

Wazungu wajiandae kwenda kupewa kazi za kufua nguo za Wachina mana wamedhidiwa Elimu. !!!!

Shubamit!!! Ulimwengu umebadilika Yajayo yanafurahisha !!
Hivi vijana wetu wanaenda China mbona output yao kwenye teknolojia hatuzioni?
 
Nakumbuka hii mada Wamarekani wa Buza walibisha sana kwenye jukwaa la tech kuhusu ubora wa Ascend

Hilo tangazo la Marekani kuyaonya mataifa mengine ni wazi wameona kuwa moto wa Huawei kwenye A.I processor utawapoteza
Walikuwa wanabisha kitu wasichokujua sio kosa lao.

Jiulize kwa nini serikali ya Marekani imepitisha kitisho cha kutonunua Huawei chips wakati Trump akiwa Mashariki ya Kati?

Saudi Arabia na UAE zinaunda vituo vikubwa vya data, ambavyo vitahitaji millions of GPUs.

Ndio maana Trump kwenye ziara yake Middle East alikuwa na CEOs wa kampuni kubwa za tech kama Nvdia

Anajua China ndio taifa pekee litacompete naye kwenye soko hilo la Middle East inapokuja kwenye AI na GPUs

Miaka hii kuhujumu wengine ili kushinda ndio siri ya Marekani ya kibiashara, ile free trade aliyokuwa akiihubiri kwenye majukwaa ya kimataifa miaka ya 1970s kushuka chini hana tena
 
Mchina ni hatari na nusu
Umesema vyema

20250516_064120.png
 
Kwa sababu ni kampuni kubwa ya kiteknolojia China na duniani kwa ujumla.
Ni sahihi

Na kwa sasa inachofanya Huawei nadhani kinaikasirisha sana Marekani

Huawei imekuwa ikishirikiana kwa ukaribu sana na kampuni zingine za tech za China na kuzipa technical assistance & technical know how kwenye masuala ya tech

Miaka 5 au zaidi ijayo Marekani haitakuwa ikipambana tu na Huawei pia na kampuni zingine za high tech za China

Je, Marekani wataweza kushindana nazo zote?
 
Walikuwa wanabisha kitu wasichokujua sio kosa lao.

Jiulize kwa nini serikali ya Marekani imepitisha sheria ya hakuna kununua Huawei chips wakati Trump akiwa Mashariki ya Kati?

Saudi Arabia na UAE zinaunda vituo vikubwa vya data, ambavyo vitahitaji millions of GPUs.

Ndio maana Trump kwenye ziara yake Middle East alikuwa na CEOs wa kampuni kubwa za tech kama Nvdia

Anajua China ndio taifa pekee litacompete naye kwenye soko hilo la Middle East inapokuja kwenye AI na GPUs

Miaka hii kuhujumu wengine ili kushinda ndio siri ya Marekani ya kibiashara, ile free trade aliyokuwa akiihubiri kwenye majukwaa ya kimataifa miaka ya 1970s kushuka chini hana tena
Marekani kwa sasa kwenye free and fair trade hayupo kabisa
 
Back
Top Bottom