Kwanini Marais wa Tanzania wanapenda kudhalilisha wateule wao?

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
877
4,105
Mara nyingi Mteule wa Rais akiwaza na kutaka kutekeleza mambo kwa uwezo wake wa kufikiri lazima atumbuliwe au aonywe. It's like kuteuliwa ni sehemu yakuua maono binafsi ya mwanasiasa badala yake anapaswa kusifia tu.

Nimeona namna Simai alivyodhalilishwa leo, kwamba alitaka aendeleze biashara yake ya pombe nikajiuliza kama anauza pombe ameanza leo? Wakati anateuliwa alikuwa auzi hizo pombe

Lakini pia wakati amejiuzulu alimshukuru Mhe. Rais na akaeleza kwamba ameshindwa kutekeleza maono yake kwa wananchi. Leo badala ya pongezi ameonekana adui na si mzalendo kwa sababu tu alizungumza na vyombo vya habari.

Katika hali ya kawaida nani anafahamu huu moshi ulivyofukuta huko ndani?Je, kama Simai aliona asipowahi ataonekana kwenye vyombo kutumbuliwa? Politics and personality requires timing at right time. Means Simai alipoona anakwenda kutumbuliwa kwa mgogoro uliokuwepo akaamua kujitumbua; kwani tupende kutumbua tusipende pia wateule wetu wanapotushtukia wakaamua kujitumbua?Who knows tomorrow, may be ungemtumbua ungedestroy future yake! May be huyu ndiye Rais ajaye.....kwanini tusiamini kwamba huyu mfanyabiashara yupo sahihi kujitumbua?

Tusipende sana kuwadhalilisha waliopo chini yetu maana hata ninyi wapo waliovumilia mapungufu yenu huko mlipotoka. Heshima ni kitu kikubwa kuliko any development we can make. We need to align our strategies and humanity/respect to others
 
Nje ya mada! Wazanzibar nao wanafanya biashara ya pombe?

Si kosa pia kama ameiina fursa inayolipa zaidi na akaamua kuichangamkia. Labda angeifanya hiyo biashara akiwa na madaraka ya Uwaziri ingeweza kuleta minong'ono.
 
Utawala wetu tumerithi itikadi za Kifalme toka Uingereza na Oman.

Kilichobadilika ni kwamba madaraka ya kifalme yamehamishiwa kwa rais.

Mfalme anapenda kusujudiwa, kuabudiwa na hana baya mbele ya wateule wake na raia kwa ujumla.
 
Nje ya mada! Wazanzibar nao wanafanya biashara ya pombe?

Si kosa pia kama ameiina fursa inayolipa zaidi na akaamua kuichangamkia. Labda angeifanya hiyo biashara akiwa na madaraka ya Uwaziri ingeweza kuleta minong'ono.
Ni biashara ya Simai enzi na enzi
 
Utawala wetu tumerithi itikadi za Kifalme toka Uingereza na Oman.
Mniwie radhi kwa kutoka kidogo nje ya mada...ni hivi

Ni mengi tumerithi. Lakini tunaweza kuviacha.

Jana nikiwa nasikiliza Hotuba ya Jaji Ibrahim Hamisi Juma, nilimsikia akisema kitu kilichonikera.

Hatahivyo, kilinipeleka kufanya tafiti fupi, na huko nikakutana na kitu kinasema

"This view may be influenced by colonialsm, imperialism, or ethnocentrism, which often assume the superiority of one culture or civilization over another'


Ikanipeleka mbali zaidi, yutub..nikamkuta Profesori P.L.O akiwapasha wanaijeria akasema, na namnukuu kiunagaubaga na kutafsiri kwa Kiswahili...


" Wapo watu wanatumia miaka sita kusoma Vyuo vikuu vyetu hapa Afrika, na wakimaliza huwasikii,(aki maanisha tunawadharau)halafu anaenda kwenye kozi ya mda wa wiki mbili Harvard.

Na, mda mwingi akiwa huko huwa anakunywa chai kafeteria, akirudi, wanamwita Alumni wa Harvard" ...mwisho wa kunukuu



Point ni tunajidhalilsha wenyewe kwa kuona kwamba tunakosea kila kitu.

Na kwamba masuluhisho ya matatizo yetu yatatokea nchi zilizoendelea-Rome was not built overnight! It is through trial and tribulation. Nasi tupitie huko.

La kutafakari:

kama unaamini kwamba matendo mengi yapo kwenye Genes au DNA, utaumiza kichwa kila siku kufikiria kuwa kutakuwa na mabadiliko Ikiwa tutafanya yale ya wenzetu.

Kila mtu na yake.

Let us brace our cultures, customs and traditions tuone kama mambo haya hayatakuja kunyooka.

Tumeshuhudia haya 2015-2021. it can be done.

Kweli tumerithi vingi na tunao uwezo wa kuviacha na kufanya tunayo yaweza.
 
Mara nyingi Mteule wa Rais akiwaza na kutaka kutekeleza mambo kwa uwezo wake wa kufikiri lazima atumbuliwe au aonywe. It's like kuteuliwa ni sehemu yakuua maono binafsi ya mwanasiasa badala yake anapaswa kusifia tu.

Nimeona namna Simai alivyodhalilishwa leo, kwamba alitaka aendeleze biashara yake ya pombe nikajiuliza kama anauza pombe ameanza leo? Wakati anateuliwa alikuwa auzi hizo pombe
Lakini pia wakati amejiuzulu alimshukuru Mhe. Rais na akaeleza kwamba ameshindwa kutekeleza maono yake kwa wananchi. Leo badala ya pongezi ameonekana adui na si mzalendo kwa sababu tu alizungumza na vyombo vya habari.

Katika hali ya kawaida nani anafahamu huu moshi ulivyofukuta huko ndani?Je, kama Simai aliona asipowahi ataonekana kwenye vyombo kutumbuliwa? Politics and personality requires timing at right time. Means Simai alipoona anakwenda kutumbuliwa kwa mgogoro uliokuwepo akaamua kujitumbua; kwani tupende kutumbua tusipende pia wateule wetu wanapotushtukia wakaamua kujitumbua?Who knows tomorrow, may be ungemtumbua ungedestroy future yake! May be huyu ndiye Rais ajaye.....kwanini tusiamini kwamba huyu mfanyabiashara yupo sahihi kujitumbua?

Tusipende sana kuwadhalilisha waliopo chini yetu maana hata ninyi wapo waliovumilia mapungufu yenu huko mlipotoka. Heshima ni kitu kikubwa kuliko any development we can make. We need to align our strategies and humanity/respect to others
Umeona namna Katiba mpya inavyohitajika sana sasa?
 
Back
Top Bottom