Kwanini mahakama ya mafisadi haipelekewi ufisadi wa zamani?

ng'adi lawi

JF-Expert Member
Sep 27, 2014
2,956
1,114
Hivi karibuni tuliambiwa kuwa mahakama mpya ya mafisadi haina kesi za kutosha zilizofunguliwa hapo. Hivi kwa nini watuhumiwa wote wa kashfa zote zilizojadiliwa bungeni kuanzia EPA, Richmond, Meremeta, Tangold, Jairo, Radar na Escrow hawapelekwi huko? Ni ushahidi hautoshi au serikali inaogopa watu fulani? Ni vema wahusika wapelekwe huko ili kuonyesha nia thabiti ya serikali kupiga vita ufisadi. Ni heri washinde kesi kuliko kutopelekwa kabisa. Vinginevyo hakukuwa na haja ya kuwa na mahakama hiyo.
 
Hivi karibuni tuliambiwa kuwa mahakama mpya ya mafisadi haina kesi za kutosha zilizofunguliwa hapo. Hivi kwa nini watuhumiwa wote wa kashfa zote zilizojadiliwa bungeni kuanzia EPA, Richmond, Meremeta, Tangold, Jairo, Radar na Escrow hawapelekwi huko? Ni ushahidi hautoshi au serikali inaogopa watu fulani? Ni vema wahusika wapelekwe huko ili kuonyesha nia thabiti ya serikali kupiga vita ufisadi. Ni heri washinde kesi kuliko kutopelekwa kabisa. Vinginevyo hakukuwa na haja ya kuwa na mahakama hiyo.
Magu alishadeclare kuwa hawezi kufukua makaburi tena maana mengine anaweza kushindwa kuyafukia
 
Sheria hairudi nyuma kikatiba huenda mbele. Matarajio ya watuhumiwa ni kuhukumiwa kwa sheria zilizokuwepo siyo zijazo

Uamuzi was sheria ianze kutumika lini ni wa wabunge kutegemea maslahi ya taifa na kama nia na madhumuni ni kuadhibu wahalifu na kuwa funzo na tishio kwa wahalifu watarajiwa. Kuna kitu kinaitwa 'with retrospective effect' - kuanzia kipindi kosa au tukio lilipotendeka.
 
Uamuzi was sheria ianze kutumika lini ni wa wabunge kutegemea maslahi ya taifa na kama nia na madhumuni ni kuadhibu wahalifu na kuwa funzo na tishio kwa wahalifu watarajiwa. Kuna kitu kinaitwa 'with retrospective effect' - kuanzia kipindi kosa au tukio lilipotendeka.

..KWELI.

..SOKOINE alikamata watuhumiwa kwanza, halafu bunge likapitisha sheria ya kuanzisha mahakama ya wahujumu uchumi.
 
Back
Top Bottom