Kwanini Lowassa anawapoteza vijana CHADEMA?

1.Mgombea wa urais wa kudumu kupitia UKAWA.
2.Mtoa pesa na mdhamini wa chama.
3.Mtu mwenye heshima na anaenyenyekewa kuliko wote CDM.
4.Mjumbe wakamati kuu CDM.

Need i say more ?

mimi naona mapovu tu hapa hana cheo chochote.
 
Mpaka kuwafunika wapigania chama kama wakina Mwalimu.

Mpaka kuwapoteza wakina Wenje wamekosa nguvu ya kupambana na kutetea wananchi.

Baada chadema impe cheo mtu kama Vincent Nyerere wao wanaangaika na mtu ambaye ana makando kando ya ufisadi.

Timu ya vijana kama Vincent Nyerere,Wenje,Kiwia wangeweza kujenga chama maana hawapo bungeni lakini sio Lowassa huyo ninayemjua.

Hivi toka lini Lowassa na &com aliowaacha ccm wameacha ufisadi?

Lowassa apumzike na yeye asiwe muongo na mtu wa kubadilika alituhaidi mwenyewe kuwa akishindwa uchaguzi ataenda kuchunga ngombe .

Sasa mtu ambaye anashindwa kutimiza tu ahadi ndogo kama hii anawezaje kuaminiwa kupewa nchi?..

Lazima tuambiane ukweli kuwa mtu kutopelekwa mahakamani sio kigezo cha kutokuwa fisadi.

Acha vijana wanaoaminika wafanye Kazi .

Jibu la mjinga ni kimya. Kwa busara na wekima alizonazo lowassa Ataka Kimya• mwisho wa siku mnamuandika tena kwa lingine # safi sana kwa style yako mheshimiwa Lowassa kimya chako kinawapa maswali mengi
 
Hakushindwa uchaguzi ila Sisiem ilipora matokeo na kugeuza kibao kuwaweka ndani vijana waliokuwa wanakusanya matokeo mpaka juzi wamefuta kesi.

Msitegemee kuwa LOWASSA atakuja kuwa Rais wa nchi hii. Tafuteni mtu mwingine atakayeweza kukiwakilisha vyema chama. Akisimama Lowassa, mjue wazi kuwa mtashindwa. Lowassa tayari ameshaanza kutoa pongezi nyingi kwa mh.Rais Magufuli. Kwa hiyo image ya Chadema ndiyo hivyo inaondoka. Msemaji wa chama amebaki mtu mmoja tu Lowassa wakati kweli chama kilikuwa na vijana na wazee wengi tu wenye uwezo wa kujenga hoja na ambao walipambana hadi kuijenga Chadema kuwa imara. Tuliondoka ndani ya Chadema kutokana na ujanjaujanja wa mwenyekiti kubadiri gia angani. Tuliondoka tukiwa tumesononeka sana kutokana na ujio wa Lowassa ndani ya chama.
 
Kwani wengine wamekatazwa? Hata akijenga Lowassa wewe kinakuuma nini? Ulishasema unamchukia sana sasa hiki ulichoweka ni kinyaa tupu!!!
Sio kukatazwa tu na kufumbwa midomo ajenda kuu ni kupambana na ufisadi sasa hata wakitoka hawawezi kuiongelea.
 
Jibu la mjinga ni kimya. Kwa busara na wekima alizonazo lowassa Ataka Kimya• mwisho wa siku mnamuandika tena kwa lingine # safi sana kwa style yako mheshimiwa Lowassa kimya chako kinawapa maswali mengi
Ukimya unamaanisha uhalifu
 
Msitegemee kuwa LOWASSA atakuja kuwa Rais wa nchi hii. Tafuteni mtu mwingine atakayeweza kukiwakilisha vyema chama. Akisimama Lowassa, mjue wazi kuwa mtashindwa. Lowassa tayari ameshaanza kutoa pongezi nyingi kwa mh.Rais Magufuli. Kwa hiyo image ya Chadema ndiyo hivyo inaondoka. Msemaji wa chama amebaki mtu mmoja tu Lowassa wakati kweli chama kilikuwa na vijana na wazee wengi tu wenye uwezo wa kujenga hoja na ambao walipambana hadi kuijenga Chadema kuwa imara. Tuliondoka ndani ya Chadema kutokana na ujanjaujanja wa mwenyekiti kubadiri gia angani. Tuliondoka tukiwa tumesononeka sana kutokana na ujio wa Lowassa ndani ya chama.
utakuwa masalia ya Dr Mihogo, pole sana siasa ni kugawana
 
Sio kukatazwa tu na kufumbwa midomo ajenda kuu ni kupambana na ufisadi sasa hata wakitoka hawawezi kuiongelea.
Nani kakwambia ajenda kuu iwapasayo watanzania ni ufisadi? Watu kwa watoto wanakufa huko kwa kukosa dawa hospitali umasikini umetopea waache kuongelea hayo? Ufisadi si mlimsifu Magufuli kaumaliza sasa mnataka nini? Chama chenu ACT hamuwezi kuichukua hiyo ajenda?

Wewe kinyaa kabisa!!
 
Nani kakwambia ajenda kuu iwapasayo watanzania ni ufisadi? Watu kwa watoto wanakufa huko kwa kukosa dawa hospitali umasikini umetopea waache kuongelea hayo? Ufisadi si mlimsifu Magufuli kaumaliza sasa mnataka nini? Chama chenu ACT hamuwezi kuichukua hiyo ajenda?

Wewe kinyaa kabisa!!
Ufisadi ufisadi pesa zinazoliwa kupitia ufisadi zingeweza kununua dawa
 
Sawa unachosema ila naona unaweza ukawa "popo au ndumila kuwili". Hujitambui wala hujui unachotetea katika nchi hii na huna mbele wala nyuma.

Chama amenunua kutoka mikononi mwa waliokuwa wanamiliki tangu mwaka jana, sahizi anatambulishwa na kunapata uzoefu ili uchaguzi wa ndani achukuwe usukani 2017/18.

EL anajulikana ni mwizi na wakubwa wako wanajua kuliko wewe. Wengi mlioko huko mmebaki kulilia mikate yenu, siku ziende. Mbowe anazidi kuwalamba akili zenu na maisha, mmebaki mnahaha tu mitandaoni, huku mkimtetea wakati amewauza na kuwafanya misukule.

Kumfundisha kuendesha gari mwenye gari, haina maana umekuwa tajiri zaidi yake. Subiri kipigo cha 2020 kwa kutanguliza huyu mwizi.
tatizo unaleta ushabiki...unachokiandika hakiwez kuwa na maana
 
Hakushindwa uchaguzi ila Sisiem ilipora matokeo na kugeuza kibao kuwaweka ndani vijana waliokuwa wanakusanya matokeo mpaka juzi wamefuta kesi.



Nashanga bado unamawazo kama hayo sijawahi sikia mtu anashinda urais lakini anasambaratishwa kwa wabunge (67%ccm ) na kwa madiwani ( zaidi 70% ccm) .
 
Toka Jana naupita huu Uzi kumbe wa ovyo ivi??!!sijaona cha maana cha kumsema lowasa kama n mjumbe wa chama.
 
Baadhi ya mashahidi wa tuhuma dhidi yake walikwishatangulia mbele za haki sasa hapo kuna kesi kweli.
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom