Kwahiyo Lowassa amekula fedha za kununulia madawa maana hakuna dawa mahospitalini? Kuna mahali sisi wananchi tumeruhusu kuchezewa akili. Hivi wewe Mkuu Technically, unaamini kwamba ajenda kuu ya taifa hili ni ufisadi na fisadi ni Lowassa? Huyu Mzee alijiuzulu kwa kashfa ya Richmond toka mwaka 2008. Sasa kama wewe na mimi tuna uchungu kweli na tunapiga vita ufisadi, hebu tupeane muda halafu turudi hapa tukiwa na orodha ya kashfa za ufisadi toka mwaka huo hadi leo tunapohadili. Halafu kashfa hizo tuone kama zinamhusisha nani. Na mwisho tuje na majibu ya ni kwanini serikali inayochukia ufisadi haimpeleki Lowassa mahakamani kwa ufisadi.Ufisadi ufisadi pesa zinazoliwa kupitia ufisadi zingeweza kununua dawa
Napendekeza hivyo kwa sababu nimekuwa nikitafakari na kupata wazo kuwa, serikali na CCM zinalitumia vibaya jina la Lowassa, na kadri nyie akina Technically mnaponasa katika propaganda zao ndipo serikali na CCM wanapopata fursa ya kufunika ufisadi mkubwa zaidi ambao unaendelea kulitafuna taifa hili zaidi ya miaka minane tangu Lowassa aondoke serikalini. Nimeona asubuhi umeandika "kutopelekwa mahakamani kwa Lowassa hakumfanyi awe msafi", come on..sasa kwa hoja hiyo hiyo wewe unapata wapi msukumo wa kuendelea kumwita Lowassa kuwa ni fisadi wakati chombo pekee kinachopaswa kuthibitisha ufisadi wake ni mahakama, ambako serikali ya CCM inashindwa kumpeleka?
Jiulize jambo hili: CCM sasa hivi hawamwiti Lowassa kuwa ni fisadi, umemsoma mzee Kinana akisisitiza tu kuwa Lowassa ni rafiki yake, huwasikii akina Mwakyembe wakisema kuwa Lowassa ni fisadi. Lakini subiri mwaka 2020! Sasa kwanini unakubali kuingia mkenge wa kutumika kwa gharama ya kulinda ufisadi mkubwa unaoendelea?