Kwanini ligi ya Nigeria siyo bora?

Kwanini ligi ya Nigeria siyo bora?

Taifa kubwa, lina hela na linapenda mpira. Inakuwaje ligi ya Tz ni bora kuliko ya Nigeria? Naona wanigeria wengi kama wakenya. Kushabikia zaidi timu za Epl lakini ndani hawana club za maana. Shida yao nini?
Kwani kila taifa lazima liwe na ligi Bora ya football?? Kenya wao wanashinda medali za dhahabu kwenye mbio kila siku.
Nigeria muziki wao ni global, umefika kote duniani.
 
Taifa kubwa, lina hela na linapenda mpira. Inakuwaje ligi ya Tz ni bora kuliko ya Nigeria? Naona wanigeria wengi kama wakenya. Kushabikia zaidi timu za Epl lakini ndani hawana club za maana. Shida yao nini?
Mjomba, kama una kiasi fulani cha fedha nenda mwenyewe huko Nigeria ukafanye utafiti kuhusu hilo tatizo. Majibu utakayoyapata, yatakuwa ni msaada pia kwetu sisi hapa jukwaani.
 
Kwani kila taifa lazima liwe na ligi Bora ya football?? Kenya wao wanashinda medali za dhahabu kwenye mbio kila siku.
Nigeria muziki wao ni global, umefika kote duniani.
Lakini Nigeria na hata Kenya bado mpira wa miguu ni mchezo pendwa kwa wananchi. Tofauti na nchi kama India au Pakistan. Tulitegemea Wanigeria wawe na ligi bora kukidhi kiu ya hao mashabiki. Ukiwaangalia wana kila kitu cha kuwafanya wawe na ligi bora.
 
Lakini Nigeria na hata Kenya bado mpira wa miguu ni mchezo pendwa kwa wananchi. Tofauti na nchi kama India au Pakistan. Tulitegemea Wanigeria wawe na ligi bora kukidhi kiu ya hao mashabiki. Ukiwaangalia wana kila kitu cha kuwafanya wawe na ligi bora.
Siasa kama zinavyotumika simba na yanga huku kule ni Vice versa
 
Kwa bara la Africa na baadhi ya nchi huko mbele nafikiri WaNigeria ndio taifa lenye wananchi wake waliofanikiwa zaidi kwenye maisha.

Wananchi wa Nigeria mmoja mmoja wana uchumi mzuri sana.

Kwa hiyo WaNigeria wengi muda mwingi wamefocus kwenye kusaka utajiri iwe kwa njia yoyote ile lazima afanikiwe sana. Hata ikibidi atepeli. Na utapeli wa Nigeria ni wa darasani kabisa ni wa kiwango cha juu.

WaNigeria ndio watu wanaoongoza waliotawanyika ulaya na Marekani kote kusaka maisha. Na naweza kusema WaNigeria ndio watu wanaokula bata sana,ksbb uchumi wanao. Taifa lao limewatengenezea mazingira ya kufanikiwa.

Sisi wa juu hawapendi ufunguliwe kuanzia kwenye elimu mpaka kibiashara.

Na bahati nzuri sana kwa Mtanzania tungefunguliwa kuanzia kwenye Elimu iliyo bora. Elimu yetu ni duni sana.

Fikiria mpaka miaka hii watoto mpaka sasa wanafundishwa panzi ana miguu mingapi? Watoto wetu bado wanafundishwa kukariri kumjua kuanzia mtendaji wa kijiji mpaka mawaziri wote hadi waziri mkuu (wakati hawa haina haja ya kuwakariri atawakuta mtandaoni akiwahitaji,na bahati mbaya siku 2 tu wamebadirishwa,kuna haja gani ya kuwakariri?). Wakati huo huo watoto wa KiNigeria na Kenya wanafundishwa uzijue sheria ukiwa nchi nyingine tambua mipaka yako tambua uhuru wako. (Watanzania ni waoga sana wakiwa nje ya nchi,hata kama yuko full document) Elimu.

Mfano tukawekewa mazingira mazuri ya kodi nafuu za bidhaa kutoka nje zitakazoingizwa na Watanzania. Watanzania ni wachakalikaji sana. Watafutaji mno. Na bahati nzuri tuna bandari pia,tungekuwa na siasa Safi Watanzania wengekuwa #one kwenye maendeleo bara la Africa.

Tatizo letu ni CCM tu basi.
Kwa hiyo ccm wanafurahi sana kuona tunamaliza muda mwingi kwa kushabikia mpira sana kuliko kujitafuta suruhisho la maisha yetu. Ksbb ukiingia huko lazima uiguse serikali,lazima ihusike kwa asilimia kubwa kwenye kutengeneza huo unafuu.
 
Eeh mkuu hapo umegusa sna, kweli Nigeria wana talent nyingi lakini ligi yao haina utaratibu, wachezaji wao wote wanakimbilia Ulaya mapema sana. Ligi yetu ingawa hela ndogo lakini imara kwenye usimamizi, ndio maana wachezaji wetu wanakaa na kuendeleza timu za ndani. Hata hivyo, Nigeria bado wana ubora wa kimichezo, ni mazingira tu yanawapoteza. umemwaga
 
Eeh mkuu hapo umegusa sna, kweli Nigeria wana talent nyingi lakini ligi yao haina utaratibu, wachezaji wao wote wanakimbilia Ulaya mapema sana. Ligi yetu ingawa hela ndogo lakini imara kwenye usimamizi, ndio maana wachezaji wetu wanakaa na kuendeleza timu za ndani. Hata hivyo, Nigeria bado wana ubora wa kimichezo, ni mazingira tu yanawapoteza. umemwaga
Uongo wachezaji wetu wanauzika nje?
 
Back
Top Bottom