Stroke
JF-Expert Member
- Feb 17, 2012
- 39,981
- 51,082
Elimu yetu ya msingi hapa Tanzania haina tofauti sana na kwingine huko duniani.Kwa bara la Africa na baadhi ya nchi huko mbele nafikiri WaNigeria ndio taifa lenye wananchi wake waliofanikiwa zaidi kwenye maisha.
Wananchi wa Nigeria mmoja mmoja wana uchumi mzuri sana.
Kwa hiyo WaNigeria wengi muda mwingi wamefocus kwenye kusaka utajiri iwe kwa njia yoyote ile lazima afanikiwe sana. Hata ikibidi atepeli. Na utapeli wa Nigeria ni wa darasani kabisa ni wa kiwango cha juu.
WaNigeria ndio watu wanaoongoza waliotawanyika ulaya na Marekani kote kusaka maisha. Na naweza kusema WaNigeria ndio watu wanaokula bata sana,ksbb uchumi wanao. Taifa lao limewatengenezea mazingira ya kufanikiwa.
Sisi wa juu hawapendi ufunguliwe kuanzia kwenye elimu mpaka kibiashara.
Na bahati nzuri sana kwa Mtanzania tungefunguliwa kuanzia kwenye Elimu iliyo bora. Elimu yetu ni duni sana.
Fikiria mpaka miaka hii watoto mpaka sasa wanafundishwa panzi ana miguu mingapi? Watoto wetu bado wanafundishwa kukariri kumjua kuanzia mtendaji wa kijiji mpaka mawaziri wote hadi waziri mkuu (wakati hawa haina haja ya kuwakariri atawakuta mtandaoni akiwahitaji,na bahati mbaya siku 2 tu wamebadirishwa,kuna haja gani ya kuwakariri?). Wakati huo huo watoto wa KiNigeria na Kenya wanafundishwa uzijue sheria ukiwa nchi nyingine tambua mipaka yako tambua uhuru wako. (Watanzania ni waoga sana wakiwa nje ya nchi,hata kama yuko full document) Elimu.
Mfano tukawekewa mazingira mazuri ya kodi nafuu za bidhaa kutoka nje zitakazoingizwa na Watanzania. Watanzania ni wachakalikaji sana. Watafutaji mno. Na bahati nzuri tuna bandari pia,tungekuwa na siasa Safi Watanzania wengekuwa #one kwenye maendeleo bara la Africa.
Tatizo letu ni CCM tu basi.
Kwa hiyo ccm wanafurahi sana kuona tunamaliza muda mwingi kwa kushabikia mpira sana kuliko kujitafuta suruhisho la maisha yetu. Ksbb ukiingia huko lazima uiguse serikali,lazima ihusike kwa asilimia kubwa kwenye kutengeneza huo unafuu.
Hayo mapanzi yanasomwa kote duniani mkuu.
Usijarajie syllabus itabadilishwa ufundishwe namna ya kufanya kazi takukuru au benki kuu hapana.
Lengo la formal education ukiachana na ajira ni kukuwezesha kufikiri vyema.
Yale mahesabu na na madude mengine yalilenga kuusaidia ubongo wako kutanuka.
Sasa kama wewe ulikuwa kasuku hutaona faida ya elimu na utazeeka ukilaumu serikali.