Kwanini kituo cha Mawasiliano kinaitwa Simu 2000?

Kwanini kituo cha Mawasiliano kinaitwa Simu 2000?

Keynez

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2007
Posts
3,621
Reaction score
6,512
Hili ni swali nimekuwa najiuliza muda mrefu ila sijapata mtu wa kunifahamisha.

Kwa nini kituo cha Mawasiliano kilichopo Sinza/Ubungo kinaitwa Simu 2000. Jina hilo limetokea wapi?

Na je kinatamkwaje, 'Simu Two Thousand' au 'Simu Elfu Mbili'?

Swali la mwisho, kwa nini pamoja na kuwa ndiyo jina rasmi la kituo kwa maana tiketi na mabasi yameandikwa hivyo, makondakta wanaonekana kupendelea zaidi jina la 'Ubungo Mawasiliano'?
 
nilishaga wahi kuuliza hili swali humu sijapata jibu mpaka leo
 
Hili ni swali nimekuwa najiuliza muda mrefu ila sijapata mtu wa kunifahamisha.

Kwa nini kituo cha Mawasiliano kilichopo Sinza/Ubungo kinaitwa Simu 2000. Jina hilo limetokea wapi?

Na je kinatamkwaje, 'Simu Two Thousand' au 'Simu Elfu Mbili'?

Swali la mwisho, kwa nini pamoja na kuwa ndiyo jina rasmi la kituo kwa maana tiketi na mabasi yameandikwa hivyo, makondakta wanaonekana kupendelea zaidi jina la 'Ubungo Mawasiliano'?
Eneo lililopo enzi zile lilihitwa UKUTA WA POSTA eneo lote la TCRA, School of Law na upande wa Aghakhan karibu na Petrol station yote ilikuwa mali ya Posta na Simu na miaka ya 2000 huko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni mapungufu makubwa ambayo saingine viongozi wanafanya!
Haileti maana sana ya moja kwa moja!

Mfano kuyaita mabasi ya “mwendo kasi” ni mapungufu makubwa!

Sababu inakinzana na swala la katazo la mwendo kasi unaosababisha ajali na maafa!


Sent using Jamii Forums mobile app
Ila kwa mabasi nakumbuka yalitumia jina la 'mabasi yaendayo haraka', ila watu somo halikuwaingia kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kulikua na kampuni ya simu iliyomilikiwa. Na mama Ana Mkapa iliyoitwa Simu 2000 ikitamkwa ( simu Two thousands) aliyoianzisha mwaka 2000....baada ya mkapa kumaliza muda wake nayo ikapotea kwenye ramani.
 
Nenda kawaulize lumumba wakupe majibu
du chadomo mnanifuata mpaka huku? nitakuwa siongelei siasa sasa maana balaa sasa lumumba ndiyo walipanga hilo jina? naona kunasehemu tumebishana wewe unaleta na huku siasa hujui wewe
 
Hili ni swali nimekuwa najiuliza muda mrefu ila sijapata mtu wa kunifahamisha.

Kwa nini kituo cha Mawasiliano kilichopo Sinza/Ubungo kinaitwa Simu 2000. Jina hilo limetokea wapi?

Na je kinatamkwaje, 'Simu Two Thousand' au 'Simu Elfu Mbili'?

Swali la mwisho, kwa nini pamoja na kuwa ndiyo jina rasmi la kituo kwa maana tiketi na mabasi yameandikwa hivyo, makondakta wanaonekana kupendelea zaidi jina la 'Ubungo Mawasiliano'?
Lile eneo lilikua linamilikiwa na kampuni/shirika la serikali liitwalo SIMU 2000 ambalo lilianzishwa kuhodhi mali za kampuni ya simu kama ilivyokuwa RALCO ambayo inahodhi mali ya kampuni ya reli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom