Kwanini kila kitu kizuri ni Rwanda tu?

Kwanini kila kitu kizuri ni Rwanda tu?

Nimekuwa najiuliza, iweje chochote kizuri inakuwa Rwanda ndio ya kwanza, mfano Gender equality Rwanda ndio ipo juu hata zaidi ya US, nchi yenye ajali za barabarani chache duniani mojawapo ni Rwanda, mji wenye usafi Afrika Kigali, nchi yenye mvuto wa uwekezaji ni Rwanda, nchi ya mwisho kwa rushwa East and Central Afrika ni Rwanda. Kuna mtu ameniambia kuwa sababu ni Rwanda ni nchi ndogo, lakini sio kweli kwani Burundi ni kubwa? Kwani Zanzibar ni kubwa? Kwa ujumla sithani kama kuna uhusiano kati ya udogo wa nchi na kuwa na mambo mazuri kwa karibu kila jambo. wadau labda ni kwanini mambo mazuri imekuwa Rwanda tu?

Ntakujibu Niko Rwanda, Mtamzania kutoka Moshi. hawatu Ni waadilifu, wama ari ya kazi na sip wanafiki. wanardhika na mishahara yako ma lijta sio sisi uswahili tu ma wizi. kila jumamosi ya mwisho wa mwezi kuamzia saa 1:00 asubuhi had I SAA 6:00 Ni mganda meaning usafi was mazingira kazi zote zinasama hata Lagame anashika ufagio.kwa nini usafi usipatikane? barabara kuu kila mita 200 traffic hapokei rushwa anakupata na kosa speeding chochote ana kitabu fine ulipe ndio uchukue gari humlipi yeye unaenda Bank ya karibu. Gender: wanawake was huku no wakasiri akiambiwa kazi yako Ni hii? Ni hiyo hadengui kama hao wetu.b
 
Hivi kwa akili ya kawaida hospital kama ya muhimbili zinatakiwa ngapi Tanzania ??
na rwanda zitatakiwa ngapi ??
shule rwanda zinahitajika ngapi na Tanzania zinahitajika ngapi ??
nimeshasema barabara ya mtwara tu mwanza ungeitapakaza rwanda nzima hadi chooni
udogo wa nchi unasaidia kasi ya maendeleo.
Hebu jiulize sisi tunaendelea au hatuendelei ??
mwaka 1961 kulikuwa na lami km ngapi sasa hivi ngapi ?? je zinaendelea kujengwa au bado ?? zimetosha au hazijatosha ??
1961 shule zilikuwa ngapi ??
1961 hospitali zilikuwa ngapi ??

Gharama ya kujenga barabara ya mwanza to mtwara ingetosha kumaliza matatizo ya shule na barabara rwanda nzima.

Jiulize mahitaji ya maji kwa watu 10 na watu 200 yanaweza kuwa sawa ??
Unaweza kuwapa laptop wanafunzi wa tanzania nzima ??
Kwa nini watu wanatekwa kwenye mabasi hayo mambo rwanda yapo ?
Ushawahi kusikia ujambazi wa hatari rwanda ??

Udogo wa nchi umesaidia sana na rais mwenyewe sio makini ki hivyo rwanda ilitakiwa iwe kati ya nchi zilizo vizuri kiuchumi

Hoja zako zote zinaweza kuwa valid kimahesabu lakini katika hali halisi haziwezi kuwa na mashiko kwenye kila situation.Katika ukuaji wa uchumi zinaweza kuwa na maana kama GDP inalingana ya nchi unazozilinganisha,kama population density inalingana/kukaribiana n.k wachumi wanajua zaidi. Tumekupa mifano ya Comoro na Burundi ukilinganisha na Rwanda,tena tuchukue mfano mzuri zaidi wa Burundi. Rwanda na Burundi zote zilipata uhuru kutoka kwa Ubelgiji mwaka 1962,zote zilikumbwa na machafuko ya kikabila kwa mara ya kwanza 1972,zote ziliingia tena kwenye machafuko makubwa zaidi miaka ya 90 (Burundi 1993,Rwanda 1994). Sasa kwa mambo yalivyo ni dhahiri uchumi wa Rwanda umeshamiri zaidi kuliko wa jirani zao Burundi unafikiri tofauti ni nini? Tuje kwa nchi yetu Tanzania,takwimu zinaonesha leo hii nchi ina wajinga (wasiojua kusoma na kuhesabu) wengi zaidi kwa asilimia kuliko miaka ya 80,uwezo wa nchi kujitegemea umepungua zaidi kuliko ilivyokuwa miaka ya 80 na vitu kibao viko hovyo sasa hivi kuliko vlivyokuwa miaka 20 baada ya uhuru.Think big mkuu!
 
Hoja zako zote zinaweza kuwa valid kimahesabu lakini katika hali halisi haziwezi kuwa na mashiko kwenye kila situation.Katika ukuaji wa uchumi zinaweza kuwa na maana kama GDP inalingana ya nchi unazozilinganisha,kama population density inalingana/kukaribiana n.k wachumi wanajua zaidi. Tumekupa mifano ya Comoro na Burundi ukilinganisha na Rwanda,tena tuchukue mfano mzuri zaidi wa Burundi. Rwanda na Burundi zote zilipata uhuru kutoka kwa Ubelgiji mwaka 1962,zote zilikumbwa na machafuko ya kikabila kwa mara ya kwanza 1972,zote ziliingia tena kwenye machafuko makubwa zaidi miaka ya 90 (Burundi 1993,Rwanda 1994). Sasa kwa mambo yalivyo ni dhahiri uchumi wa Rwanda umeshamiri zaidi kuliko wa jirani zao Burundi unafikiri tofauti ni nini? Tuje kwa nchi yetu Tanzania,takwimu zinaonesha leo hii nchi ina wajinga (wasiojua kusoma na kuhesabu) wengi zaidi kwa asilimia kuliko miaka ya 80,uwezo wa nchi kujitegemea umepungua zaidi kuliko ilivyokuwa miaka ya 80 na vitu kibao viko hovyo sasa hivi kuliko vlivyokuwa miaka 20 baada ya uhuru.Think big mkuu!
unaongelea kisomo cha ngumbalu, wakati wakisema 90 % ya wa TZ ni wasomi kwakuwa wanajua aa, be, che walizosoma chini ya mwembe!
Hivi uchumi hauangalii ubora kulinganisha na wingi?
Watanzania waliopata shahada ya tatu 2013 pekee kila mtaa wa kigali wangegawiwa mmoja na kutosha.
 
nimepitia comment nyingi kweli kunawatu hawaku stahili kuwa humu jf kabisa we mtu amekomaa tu udogo wa nchi udogo wa nchi huu ni upuuzi Malawi je Burundi je Togo je hivi kwa nini watu wanaungana? mfano EA watu ni rasilimali ndo maana US walipoungana nchi ikawa vile China etc ona Uk ni kadogo lakini ni super power fikiria wewe au tuombe watolewe humu jf
 
nimepitia comment nyingi kweli kunawatu hawaku stahili kuwa humu jf kabisa we mtu amekomaa tu udogo wa nchi udogo wa nchi huu ni upuuzi Malawi je Burundi je Togo je hivi kwa nini watu wanaungana? mfano EA watu ni rasilimali ndo maana US walipoungana nchi ikawa vile China etc ona Uk ni kadogo lakini ni super power fikiria wewe au tuombe watolewe humu jf

Dar ingekuwa nchi ingekuwa tajiri kuliko zote Afrika, ikiwa na GDP ya hatari.
 
Kitu gani kizuri kinatoka rwanda?? Kama nin??
 
unaongelea kisomo cha ngumbalu, wakati wakisema 90 % ya wa TZ ni wasomi kwakuwa wanajua aa, be, che walizosoma chini ya mwembe!
Hivi uchumi hauangalii ubora kulinganisha na wingi?
Watanzania waliopata shahada ya tatu 2013 pekee kila mtaa wa kigali wangegawiwa mmoja na kutosha.

Nimekuelewa kidogo sana ndugu pleo jaribu kurudia editing. Sawa inaweza kuwa "wasomi" hao unawasema wewe wa chuo kikuu wameongezeka sana kwa idadi lakini kundi la wajinga pia limezidi kukua kuliko ilivyokuwa hapo niaka ya 80 kama nilivyoeleza. Ili nchi iendelee haiitaji madigrii mengi mkuu,usishangae kuambiwa nchi fulani ipo juu kielimu na ikawa inazidiwa na Tanzania kwa idadi ya "madigrii" inaweza kuwa wananchi wake asilimia kubwa (tuseme 90%) wamefika angalau form four tu na ikawa nchi ya kupigiwa mfano,kuliko nchi yenye madigrii asilimia tuseme 20% ya wananchi na 50% mbumbumbu.
 
Last edited by a moderator:
Dar ingekuwa nchi ingekuwa tajiri kuliko zote Afrika, ikiwa na GDP ya hatari.

Unaongea hivyo ukiwa na data za sensa ya 2012 au unaongea tu kutoka hewani? Tafuta GDP za Cairo,Capetown,Jo'burg,Luanda linganisha na Dar then urudi tujadili.
 
nimepitia comment nyingi kweli kunawatu hawaku stahili kuwa humu jf kabisa we mtu amekomaa tu udogo wa nchi udogo wa nchi huu ni upuuzi Malawi je Burundi je Togo je hivi kwa nini watu wanaungana? mfano EA watu ni rasilimali ndo maana US walipoungana nchi ikawa vile China etc ona Uk ni kadogo lakini ni super power fikiria wewe au tuombe watolewe humu jf

Nafikiri itabidi members wafanyiwe aptitude test,teh teh teh
 
Unaongea hivyo ukiwa na data za sensa ya 2012 au unaongea tu kutoka hewani? Tafuta GDP za Cairo,Capetown,Jo'burg,Luanda linganisha na Dar then urudi tujadili.

> nchi ndogo = uwezekano mkubwa wa kuwa na maendeleo.
 
marekani wameanza kujitegemea lini kama taifa ??

Hivi unajua nchi karibu zote za ulaya ni kama mkoa tu hapa Tanzania ndio maana wameweza kuendelea haraka nchi kama ubeligiji ina watu milioni nane kama ingekua Tanzania watu milioni ningeweza kuwakumbuka hata robo tatu ya wakazi wa nchi nzima

asilimia kubwa ya nchi zenye eneo kubwa ni masikini hutaki unakuja na fact sio ubishani

Naona una jitahid sana kutetea hv huu ukubwa Wa nchi yetu ndan yake kuna madin,mbuga,milima,gesi,bandari vitu hv vimetusaidiaje kuendeleza nchi hii usiwe na mawazo kuwa ukubwa Wa nchi ndo utufanye kula rushwa,kuja viwanda,kusafirisha meno ya tembo,kuwa weka viongozi mafisadi viporo kuwaacha kina chenge wasubili kupiga deal lingine

Kama n ukubwa wa nchi na idadi ya watu Leo China wangekuwa maskin wa kutupwa wamepata Uhuru 49 na sisi 61 tofaut ni miaka 11 tu lkn walipo Leo n sir yako

Kaka kubali tu kuwa rwanda uko juu kwa sababu ya uongoz makin sio kama sisi kuchekeana tu suala la udogo wa nchi ni facta ndogo sn, ninashukuru rasilimali nyingi tulizonazo wao hawana wangekuwa nazo Leo tungezid kuoneana aibu
 
Ukiwa na chumba kimoja ni rahisi kukisafisha kila siku, tofauti na ukiwa na hekalu.

Leo chumba imekuwa n nchi? Kna mifano humu jf, anyway ngoja nitembelee mfano wako huo huo haya TZ ni hekalu lenye watu million 43 wanashindwaje kufanya usafi kila siku
 
Nimekuelewa kidogo sana ndugu pleo jaribu kurudia editing. Sawa inaweza kuwa "wasomi" hao unawasema wewe wa chuo kikuu wameongezeka sana kwa idadi lakini kundi la wajinga pia limezidi kukua kuliko ilivyokuwa hapo niaka ya 80 kama nilivyoeleza. Ili nchi iendelee haiitaji madigrii mengi mkuu,usishangae kuambiwa nchi fulani ipo juu kielimu na ikawa inazidiwa na Tanzania kwa idadi ya "madigrii" inaweza kuwa wananchi wake asilimia kubwa (tuseme 90%) wamefika angalau form four tu na ikawa nchi ya kupigiwa mfano,kuliko nchi yenye madigrii asilimia tuseme 20% ya wananchi na 50% mbumbumbu.

Tunahitaji wenye upeo wachache wakuanzisha mchakato wa maendeleo wakipata nguvu kazi ya nafuu zaidi, kinyume chake soko la ajira litakuwa ghali tutapata ukinzani wa kuuza.
Hivyo mzania umebadilishwa kuendana na uhitaji halisi.
 
Last edited by a moderator:
mkuu bora umeliona hilo kuna watu hawaelewi ni rahisi kuitawala na kuiongoza rwanda kuliko Tanzania
kwa kutumia akili ya kuitawala rwanda ni vigumu kuitawala Tanzania

M0 11 leo naona unashusha hadhi yako kwa posts zako Mkuu naamin hukutulia ukawaza kdgo then ukaanza kupost hv rwanda ni rais kuiongoza? Nchi ina kabila 2 zenye uhasama, imetoka vitan,haina rasilimali za kutosha, hawana bandari ya kupokea mizigo toka ulaya,usalama sio mzuri hata reli hakuna, zao kuu la biashara hata halijulikani nchi ya namna hii unaitawala VP

Njoo TZ kwenye maziwa na asali, wana dhahabu hao,wanyama sasa,eeh na bandari ipo,reli oyeee, makabila full, bunge lake lina kipaji wanatunga katiba hata km wengine wamesusa hawa sasa ndo rahisi kuwatawala
 
Naona una jitahid sana kutetea hv huu ukubwa Wa nchi yetu ndan yake kuna madin,mbuga,milima,gesi,bandari vitu hv vimetusaidiaje kuendeleza nchi hii usiwe na mawazo kuwa ukubwa Wa nchi ndo utufanye kula rushwa,kuja viwanda,kusafirisha meno ya tembo,kuwa weka viongozi mafisadi viporo kuwaacha kina chenge wasubili kupiga deal lingine

Kama n ukubwa wa nchi na idadi ya watu Leo China wangekuwa maskin wa kutupwa wamepata Uhuru 49 na sisi 61 tofaut ni miaka 11 tu lkn walipo Leo n sir yako

Kaka kubali tu kuwa rwanda uko juu kwa sababu ya uongoz makin sio kama sisi kuchekeana tu suala la udogo wa nchi ni facta ndogo sn, ninashukuru rasilimali nyingi tulizonazo wao hawana wangekuwa nazo Leo tungezid kuoneana aibu

TZ ingegawanywa kwenye majimbo, maendeleo kulingana na rasilimali ungeyaona na kwa kuwa jimbo ni kama nchi ndani ya nchi, hivyo nchi kubwa inagawanywa kwenye vi_inchi vidogo vinavyoweza kutawaliwa kwa urahisi ndio maana tunasumbuliwa na hata Msumbiji.

Marekani ni ndogo kuliko Afrika lakini ina majimbo karibu sawa na idadi ya nchi za Afrika, S.A, China, Uingereza n.k. Wanatumia mifumo inayokaribia kuiita kwa ujumla kama mifumo ya majimbo.

Hivyo siri ni kuwa na utawala wa eneo dogo kusimamia eneo dogo kama Rwanda kupata maendeleo.
 
Hivi kwa akili ya kawaida hospital kama ya muhimbili zinatakiwa ngapi Tanzania ??
na rwanda zitatakiwa ngapi ??
shule rwanda zinahitajika ngapi na Tanzania zinahitajika ngapi ??
nimeshasema barabara ya mtwara tu mwanza ungeitapakaza rwanda nzima hadi chooni
udogo wa nchi unasaidia kasi ya maendeleo.
Hebu jiulize sisi tunaendelea au hatuendelei ??
mwaka 1961 kulikuwa na lami km ngapi sasa hivi ngapi ?? je zinaendelea kujengwa au bado ?? zimetosha au hazijatosha ??
1961 shule zilikuwa ngapi ??
1961 hospitali zilikuwa ngapi ??

Gharama ya kujenga barabara ya mwanza to mtwara ingetosha kumaliza matatizo ya shule na barabara rwanda nzima.

Jiulize mahitaji ya maji kwa watu 10 na watu 200 yanaweza kuwa sawa ??
Unaweza kuwapa laptop wanafunzi wa tanzania nzima ??
Kwa nini watu wanatekwa kwenye mabasi hayo mambo rwanda yapo ?
Ushawahi kusikia ujambazi wa hatari rwanda ??

Udogo wa nchi umesaidia sana na rais mwenyewe sio makini ki hivyo rwanda ilitakiwa iwe kati ya nchi zilizo vizuri kiuchumi

Hv mo 11 kaenda WAP kuna MTU kaiba akaunti yake anatupostia pumba tupu mo 11 njoo umkamate
 
TZ ingegawanywa kwenye majimbo, maendeleo kulingana na rasilimali ungeyaona na kwa kuwa jimbo ni kama nchi ndani ya nchi, hivyo nchi kubwa inagawanywa kwenye vi_inchi vidogo vinavyoweza kutawaliwa kwa urahisi ndio maana tunasumbuliwa na hata Msumbiji.

Marekani ni ndogo kuliko Afrika lakini ina majimbo karibu sawa na idadi ya nchi za Afrika, S.A, China, Uingereza n.k. Wanatumia mifumo inayokaribia kuiita kwa ujumla kama mifumo ya majimbo.

Hivyo siri ni kuwa na utawala wa eneo dogo kusimamia eneo dogo kama Rwanda kupata maendeleo.

the say sina la kuongeza hapa
udogo wa nchi umesababisha vinchi vingi vya ulaya kuendelea kwa haraka
umetaja ujerumani sawa ila hapo mwanzo zilikuwa mbili
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom