Kwanini JWTZ isipewe kazi ya kupigana na vita ya adui njaa?

Nchi hii haina njaa. Au hamjasikia jana kwenye vyombo vya habari kwamba mkoa wa Rukwa umewasilisha rasmi jana barua serikalini ukiomba uruhusiwe kuuza mazao yake nchi jirani? Kwa mujibu wa taarifa hiyo, zaidi ya tani 170000 za mahindi ziliuzwa mwaka jana na zimebakia zaidi ya tani 150000 na bado mavuno mengine zaidi yanakuja July. Kama kuna eneo lina njaa Tanzania, basi wakanunue mahindi Rukwa.
 
Nchi hii haina njaa. Au hamjasikia jana kwenye vyombo vya habari kwamba mkoa wa Rukwa umewasilisha rasmi jana barua serikalini ukiomba uruhusiwe kuuza mazao yake nchi jirani?

Kwa Rukwa mbona ni kila mwaka mkuu sasa jiulize na tafakari zaidi kwa nn kuuza mazao nje mpaka kitolewe kibari.Je hilo ndo soko huria ? kwa nn kila mwaka tunasikia marufuku za watu wasiuze mahindi ya kuchoma?Na kwa nn iliwekwa marufuku ya kuuza mazao nje?
 
waberoya - watu wengi hawaelewi - wanafikiri jeshi ni kuvaa magwanda na minyota mabegani
hawajui jeshi lazima liwe mfano kwenye nyanja za Uchumi, Ufundi, Mawasiliano, Elimu, Utabibu, Utafiti nk
Jeshi letu lipo lipo tu - eti wanangojea vita ije - isipokuja? hiyo bajeti ya bilioni zote hizo kwa mwaka inatoka kwa nani?

Majeshi yote duniani muda wa amani wanatumia kuweka nguvu katika masuala kama hayo na mengine ambayo waberoya kafafanua zaidi.

Mfano kama tunataka mapinduzi ya kilimo - kwa nini tusitumie jeshi letu liwe mfano? its true nchi za wenzetu majeshi yamekuwa yanatangulia then wananchi wanafuata nyuma - na ndiyo maana jeshi letu linaitwa JESHI LA WANANCHI.
 
Mimi nashauri Jeshi lipewe kazi ya TRL(Tanzania Railways Limited), maana shirika hili linayumba mno, Jeshi litaweza kuchonga vipuri kutumia Kampuni yake ya Nyumbu, wahujumu wa Reli wataogopa kwa vile reli itakuwa kampuni tanzu ya jeshi.

Hili tatizo la reli ya kati Tanzania naweza kuifananisha na vita kamili, maana inaleta madhara kwa uchumi wa Tanzania ktk sekta zote pamoja na kilimo.

Wakati wa vita kuu ya kwanza na ya pili ya dunia, Uingereza ilikabidhi network zote za reli kwa jeshi lake la ulinzi ili kuleta ufanisi kushinda vita. Tanzania sasa ina vita ya kiuchumi, hiyo ni sahihi jeshi kupewa uendeshwaji wa reli.
 
waberoya - watu wengi hawaelewi - wanafikiri jeshi ni kuvaa magwanda na minyota mabegani
hawajui jeshi lazima liwe mfano kwenye nyanja za Uchumi, Ufundi, Mawasiliano, Elimu, Utabibu, Utafiti nk
Jeshi letu lipo lipo tu - eti wanangojea vita ije - isipokuja? hiyo bajeti ya bilioni zote hizo kwa mwaka inatoka kwa nani?

Majeshi yote duniani muda wa amani wanatumia kuweka nguvu katika masuala kama hayo na mengine ambayo waberoya kafafanua zaidi.

Mfano kama tunataka mapinduzi ya kilimo - kwa nini tusitumie jeshi letu liwe mfano? its true nchi za wenzetu majeshi yamekuwa yanatangulia then wananchi wanafuata nyuma - na ndiyo maana jeshi letu linaitwa JESHI LA WANANCHI.

Asante mkuu kwa kupigilia msumari, tena nasikia jeshini kuna vijana wengi, just Imagine unamwajiri kijana ana miaka 30 mpaka anagonga 55 anashika mtutu tu na kufanya mazoezi.

Tatizo jeshi limekuwa sehemu ya siasa na sio professionals.
 
Back
Top Bottom