Kwanini Julius Mtatiro alienda CUF?

Kwanini Julius Mtatiro alienda CUF?

Joined
Jun 8, 2011
Posts
52
Reaction score
19
Julius Mtatiro ni jembe kwelikweli hili halina ubishi hata John Mnyika anafahamu ukweli huu, ila mpaka leo nashindwa kuelewa kwanini mpambanaji huyu hakujiunga na CHADEMA badala yake akatimkia CUF?
 
ndio mambo ya nitoke vipi?unaweza ukalamba kimeo na ndo yaliyomkuta jamaa.
 
We mtatiro bana...yan umeamua kutupia thread ili kupima upepo wa kauli yako ya jana kwa Mbowe?Tumeisoma gazetin...na umedhalilika kwel Muraaa...endelea kupma upepo umu jamvini
 
Noana ameamua kujifanyia analysis yake hapa!!! ajipange vizuri tu 2015 sio mbali sana tutakupa jimbo la Temeke
 
Tuambie kwanini ulienda cuf,sisi hatujui kwani we ni nani hata tufatilie details zako.
 
Julius Mtatiro ni jembe kwelikweli hili halina ubishi hata John Mnyika anafahamu ukweli huu, ila mpaka leo nashindwa kuelewa kwanini mpambanaji huyu hakujiunga na CHADEMA badala yake akatimkia CUF?

Anajuwa ule msemo "Mafahali............hawakai pamoja. Kashililah alikuwa huko huko na Zitto ndio hivyo mguu ndani mguu nje. Kama unakubali kuwa ana akili basi akili yake ilishamtahadharishja.
 
Nahisi huyu mleta thread ni Mtatiro mwenyewe! Anyway Mtatiro kwa kauli yako kuponda uamuz wa Kamanda Mbowe nimekuona kituko yani hufai.
 
na mtatiro angegombea pengine angepita bila kupingwa. tatizo ubungo myika alikuwa ashatengeneza jina. ila jamaa ni kichwa
 
Mtatiro ana jazba na bado anakosa umakini kiasi flani,anaweza kuwa anatumia nguvu sana zaidi ya brain

Na kwa nini useme hata Mnyika anakufahamu?ama unadhani Tanzania nzima ni Mnyika tu?acha kuendelea kumfikiria Mnyika kwani kiukweli jamaa ni zaidi yako ukubali usikubali
 
kwani anatoka kaskazini?
Nimesoma hapa nikawakumbuka kina Silinde, Mbilinyi Joseph,Wenje Hezekiah,Machemli,Meshack Opulukwa,Kasulumbayi,Nyerere!Je huo ndio ukaskazini unaozungumzia?Hongera sana kama ndivyo(Irony)
 
Binafsi namuona jamaa hafit pale CDM kutokana na hulka yake ya kuropoka na kusema bila kufikiri, huwezi kufananisha na mnyika hata kidogo mnyika ni mtu wa kufakari jambn ndipo afanye comments
 
Back
Top Bottom