Anadharau wasomi sababu hawana pesa kama yeye na hao wasomi wameshindwa kuonyesha usomi wao na wamefanya siasa kama ajira, wakati Musukuma siasa ni kijiwe chake cha kupiga dili za kitapeli, kutokana na jeuri yake hata mawaziri wanamuogopa, jeuri yake ya pesa inamfanya apate vibali mbalimbali kama vya kuagiza au kuuza michele nje, kupata viwanja vya kujenga apartments sehemu azitakazo kutoka kwa watawala ambao wanamuogopa kwa kuhusu kuwa anaweza kuwa blackmail. Musukuma ana ukwasi mkubwa wa pesa lakini sidhani kama analipa kodi. Musukuma ni mhuni tu ila ni mjanja wa kujigeuza, huyu mwanzoni wakati wa kinyang'ang'anyiro cha kumpata raisi alikuwa kundi la Lowasa akiwa na akiwa na akina Kingunge ,Tibaijuka,Awesu na nakumbuka wakati wa mkutano wa Lowasa uwanja wa Sheikh Amri Abeidalikuwa wa mwisho kufika na akashuka na helicopter uwanjani, lakini baada ya kuona upepo umebadirika akjigeuza na kuwa mfuasi kindakindaki wa Jiwe na baada ya Jiwe kutwaliwa kageuka chawa wa mama! Huyo ndio Musukuma yeye yupo kuchumia tumbo lake.