Kwanini Ikulu inaendelea kuudanganya ulimwengu?

Kwanini Ikulu inaendelea kuudanganya ulimwengu?

Kichwa cha mada hii kinasema, "Kwanini Ikulu inaendelea kuudanganya ulimwengu?"

Tafsiri ya kichwa hicho ni kuwa taasisi ya urais imeendelea kuudanganya ulimwengu kuhusu ukweli huo wa mapinduzi tangu yalipotukia,
yericko nyerere labda hujanielewa. haya ndo mwl. nyerere aliyokuwa akihubiri kwa zaidi ya miaka 21, na hawa wanachofanya ni kurudia tu yale aliyoyaasisi mwl. ukisema kwa nini ikulu inaendelea kuudanganya ulimwengu unamaanisha mwalimu nyerere alidanganya ulimwengu? maana hawa wanaendeleza alichokuwa akikifanya mwalimu.
Acha kumumunya maneno/kupindisha maandishi. swali langu lipo straight forward.
 
Post yako umeiweka kisiasa zaidi. Unaposema ikulu imedanganya unamaanisha ikulu ipi ikulu ya magogoni au ikulu ya zanzibar. Sherehe za mapinduzi muhusika ni raisi wa zanzibar. Kumbuka Tanzania ni muungano wa nchi mbili Tanganyika na zanzibar, Na mapinduzi yalifanyika kabla ya muungano hivyo taarifa yoyote itakayotolewa na ikulu ya magogoni kuhusu mapinduzi fahamu kuwa kwa asilimia mia moja imeletwa na raisi wa zanzibar. Hivyo kama kweli ulitaka tuchangie mada yako then ungeandika. IKULU YA ZANZIBAR YAIDANGANYA IKULU YA MAGOGONI KUHUSU UKWELI WA HISTORIA YA MAPINDUZI.

Yaani ulichokipost ni sawa na mkenya aje hapa aseme nyerere hakupigania uhuru. sisi kama watanganyika tuna historia yetu, na wao kama wazanzibari wanahistoria yao. Misingi ya kutugawa inakuja hapo. Wazanzibari wenyewe wanaamini na katika sherehe wameeleza karume ndiye baba na muasisi wa nchi yao Raisi JK kasema hivyo hivyo kama walivyosema wao, HAPO KUDANGANYA KUNATOKEA WAPI?
NOTE: Napata shida sana ku imagine Tanzania itakavyokuwa siku chama chako kikishika nchi. Kama mawazo yenu yenyewe ndiyo haya, mtavuruga sana amani, upendo, umoja na mshikamano uliojengeka miongoni mwetu.

Pole mkuu wangu kwakukukwaza katika mada hii,

Nimeandika hoja hii kwakuweka ambato lenye kuakisi lengo tajwa,

Tume fursa yako soma na kutafakari, utaona kuwa ikulu ninayoisema ni ipi,

Jamhuri ya watu wa Tanzania ni muunano wa nchi mbili, Tamko la rais wa Tanzania ni tamko la nchi nzima haijalishi kalipata toka wapi, jambo muhimu nikuwa tamko la jamhuri,

Ukiisoma mada hii kwa utulivu na adabu utaona uhalisia wake, kwakuwa haina uhusiano wowote na Chadema.

Lakini siasa za chadema na ccm zimekuathiri sana ndugu yangu, kila kitu unakiangalia kwajicho hilo tu.
 
yericko nyerere labda hujanielewa. haya ndo mwl. nyerere aliyokuwa akihubiri kwa zaidi ya miaka 21, na hawa wanachofanya ni kurudia tu yale aliyoyaasisi mwl. ukisema kwa nini ikulu inaendelea kuudanganya ulimwengu unamaanisha mwalimu nyerere alidanganya ulimwengu? maana hawa wanaendeleza alichokuwa akikifanya mwalimu.
Acha kumumunya maneno/kupindisha maandishi. swali langu lipo straight forward.

Ni ikulu hiyo iliyokuwa chini ya Mwalimu ndio iliyoasisi uongo huo,

Sasa ninahoji kuwa, kwanini Ikulu inaendelea kuudanganya ulimwengu?
 
Mkuu,

Kwanza habari za siku,

Hapa katika mada hii kinachotutenga ni tafsiri ya lugha tu,

"Uasisi wa mapindizi"

Kwakawaida neno uasisi husimama baada ya kitu kutukia, na hapo ndipo ndipo huanza kusomwa kuwa uasisi.

Katika dhana ya mapinduzi ya Zanzibar John Okello ndiye muasisi, haijalishi aliukuta wapi mpango wa mapinduzi, jambo kuu ni kuwa yeye ndie aliongoza mapinduzi hadi 12/01/1964 na tukio zima likatukia.
Habari zangu mzima...heri ya mwaka mpya!! Kama hoja yako ndiyo hiyo basi niseme tu ndugu yangu yakupasa lugha yetu uipigie jaramba kwa maana inakupiga chenga! Angalau ungekuwa sahihi lau kama ungesema alipanga; lakini kuasisi; la hasha!!Kuasisi ni kuanzisha kitu; na inaswihi kabisa kwamba jambo fulani muasisi akawa ni mwingine, mpangaji ni mwingine, mtekelezaji ni mwingine n.k! Sina shaka hata kidogo kwamba Okello si muasisi lakini anaweza kuwa ndie aliyepanga lakini nalo halina uhakika wa 100%...jambo pekee lisilo na shaka yoyote ni kwamba alitekekeleza mapinduzi yale yaliyoyoondosha utawala wa Sultan.
 
Habari zangu mzima...heri ya mwaka mpya!! Kama hoja yako ndiyo hiyo basi niseme tu ndugu yangu yakupasa lugha yetu uipigie jaramba kwa maana inakupiga chenga! Angalau ungekuwa sahihi lau kama ungesema alipanga; lakini kuasisi; la hasha!!Kuasisi ni kuanzisha kitu; na inaswihi kabisa kwamba jambo fulani muasisi akawa ni mwingine, mpangaji ni mwingine, mtekelezaji ni mwingine n.k! Sina shaka hata kidogo kwamba Okello si muasisi lakini anaweza kuwa ndie aliyepanga lakini nalo halina uhakika wa 100%...jambo pekee lisilo na shaka yoyote ni kwamba alitekekeleza mapinduzi yale yaliyoyoondosha utawala wa Sultan.

Mkuu Nimekusoma vizuri tatizo la huyu kijana anajitoa ufahamu tu! hili darasa tulishamfundisha muda mrefu lakini chuki ndio zinamsumbia.
 
Ni ikulu hiyo iliyokuwa chini ya Mwalimu ndio iliyoasisi uongo huo,

Sasa ninahoji kuwa, kwanini Ikulu inaendelea kuudanganya ulimwengu?
ninachokiona ni kuwa JK hataki kuonekana amebadilisha chochote kile alichokiasisi mwl nyerere. ndo maana hata suala la serikali 3 inakuwa ngumu kwake kumeza kwa dhana hiyohiyo japokuwa kila kitu kipo wazi kuwa wananchi wanataka serikali 3.
 
Habari zangu mzima...heri ya mwaka mpya!! Kama hoja yako ndiyo hiyo basi niseme tu ndugu yangu yakupasa lugha yetu uipigie jaramba kwa maana inakupiga chenga! Angalau ungekuwa sahihi lau kama ungesema alipanga; lakini kuasisi; la hasha!!Kuasisi ni kuanzisha kitu; na inaswihi kabisa kwamba jambo fulani muasisi akawa ni mwingine, mpangaji ni mwingine, mtekelezaji ni mwingine n.k! Sina shaka hata kidogo kwamba Okello si muasisi lakini anaweza kuwa ndie aliyepanga lakini nalo halina uhakika wa 100%...jambo pekee lisilo na shaka yoyote ni kwamba alitekekeleza mapinduzi yale yaliyoyoondosha utawala wa Sultan.

Naaam,

Mkuu naomba nikuulize swali moja tu,

Nani muasisi/waasisi wa uhuru wa Tanganyika?
 
ninachokiona ni kuwa JK hataki kuonekana amebadilisha chochote kile alichokiasisi mwl nyerere. ndo maana hata suala la serikali 3 inakuwa ngumu kwake kumeza kwa dhana hiyohiyo japokuwa kila kitu kipo wazi kuwa wananchi wanataka serikali 3.

Huo ndio utawala msonge,
 
anuani imeandikwa kingereza habari imeandikwa kiswahili. kweli hata ikulu hawajielewi
 
Mkuu hata we umedanganya na ALBERTmsando aka kuumbua kwenye instagram cc Ritz
 

Attachments

  • 1389996086380.jpg
    1389996086380.jpg
    93.3 KB · Views: 90
Last edited by a moderator:
Mapinduzi ya Zanzibar yaliongozwa na Sheikh Abedi Amani Karume.

Kuongoza ni kupanga mikakati na kuwaachia wengine watekeleze.

Tuyaenzi Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar na kuenzi matokeo chanya ya Mapinduzi hayo ambao ni Muungano wetu adhimu ulituzalishia taifa moja tuu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kule Zanzibar wao wana msemo wao was
Mapinduzi Daima
Na sisi Watanzania katika umoja wetu tunasema kwa kauli moja
Tutaulinda Muungano kwa gharama yoyote, na hata kama gharama yenyewe ni kutengua demokrasia kama ilivyofanyika kwenye uchaguzi wa Zanzibar, for the sake of union, demokrasia na itenguliwe! .

Nawatakia mapumziko mema ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Paskali
 
Mapinduzi ya Zanzibar yaliongozwa na Sheikh Abedi Amani Karume.

Kuongoza ni kupanga mikakati na kuwaachia wengine watekeleze.

Tuyaenzi Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar na kuenzi matokeo chanya ya Mapinduzi hayo ambao ni Muungano wetu adhimu ulituzalishia taifa moja tuu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kule Zanzibar wao wana msemo wao was
Mapinduzi Daima
Na sisi Watanzania katika umoja wetu tunasema kwa kauli moja
Tutaulinda Muungano kwa gharama yoyote, na hata kama gharama yenyewe ni kutengua demokrasia kama ilivyofanyika kwenye uchaguzi wa Zanzibar, for the sake of union, demokrasia na itenguliwe! .

Nawatakia mapumziko mema ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Paskali
Umeamua kuchagua kundi lako mkuu?
 
mapinduzi yaliongozwa na okelo lakini kwa vile siasa ndio huongoza nhi ikabidi kiongozi wa asp ndio kuongoza nchi.
 
Back
Top Bottom