Kwanini Idadi Kubwa Ya Walokole Ni Maskini?

Kwanini Idadi Kubwa Ya Walokole Ni Maskini?

Status
Not open for further replies.
Wakuu Habari!
Huwa Na Jiuliza Kuna Uhusiano Gani Kati Ya Umaskini Na Ulokole, Kwani Nina Ndugu Yangu Kabla Ya Kuokoka Alikuwa Na Kibato Kizuri Tu, Na Gari Na Nyumba Nne. Lakini Baada Ya Kuokoka Amefilisika Kabisa Ameuza Gari Na Nyumba Mbili. Sasa Anashindwa Hata Kuwasomesha Watoto Wake Yaani Amechoka.
Swali La Kujiuliza Kwanini Idadi Kubwa Ya Watu Wanaojiita WALOKOLE Ukiingalia Maisha Yao Ni Duni Lakini Sio Wote. Sasa Kuna Uhusiano Gani Kati Ya Ulokole Na Umaskini?

Walokole walio na maisha duni ni waumini(kondoo) lakini si viongozi wao (wachungaji). Kwa nini? Kwa sababu kama Yesu alivyosema ni kwamba wanachunwa ngozi wakiwa hai. Hawana ujuzi sahihi wa neno la Mungu kwa hiyo wanatumiwa kama vitega uchumi bila wao kujijua. Viongozi wao wanaishi maisha ya juu na ya kifahari wakati wao hawajui kesho watakula nini.
Kwa moyo mweupe kabisa wanafikiri sadaka wanazotoa zinaenda kuendeleza kazi ya Mungu kumbe zinaenda kutajirisha watu. Mungu anaona na anawaonea huruma kwa jinsi wanavyochunwa ngozi wakiwa hai. Yesu anatoa shauri hili lenye upendo kwa hao kondoo wanaoteseka:
"Tokeni kwake watu wangu ikiwa hamtaki kushiriki pamoja naye dhambi zake na ikiwa hamtaki kupokea sehemu ya mapigo yake"
 
Walokole walio na maisha duni ni waumini(kondoo) lakini si viongozi wao (wachungaji). Kwa nini? Kwa sababu kama Yesu alivyosema ni kwamba wanachunwa ngozi wakiwa hai. Hawana ujuzi sahihi wa neno la Mungu kwa hiyo wanatumiwa kama vitega uchumi bila wao kujijua. Viongozi wao wanaishi maisha ya juu na ya kifahari wakati wao hawajui kesho watakula nini.
Kwa moyo mweupe kabisa wanafikiri sadaka wanazotoa zinaenda kuendeleza kazi ya Mungu kumbe zinaenda kutajirisha watu. Mungu anaona na anawaonea huruma kwa jinsi wanavyochunwa ngozi wakiwa hai. Yesu anatoa shauri hili lenye upendo kwa hao kondoo wanaoteseka:
"Tokeni kwake watu wangu ikiwa hamtaki kushiriki pamoja naye dhambi zake na ikiwa hamtaki kupokea sehemu ya mapigo yake"

Ndio Mkuu Nimezungumzia Waumini Wao Na Sio Wachungaji Wao. Lakini Si Wote
 
Acheni kuleta mistari ya biblia Jibuni sealing la mtoa mada
Sio tu walokole. Waangalie wote wanaojifanya wanaijua dini sana
Ni maskini wakubwa
Mkuu lazima wakwambie maneno wanayosimamia
 
2po walokole wenye ela tumenyamaza siri kubwa ni kumtolea MUNGU kwa uaminifu atakubariki si kweli kabsa kua walokole ni maskini....
 
2po walokole wenye ela tumenyamaza siri kubwa ni kumtolea MUNGU kwa uaminifu atakubariki si kweli kabsa kua walokole ni maskini....

Mpo Wachache Sana Kama Ni Asilimia Ni 15 Kati Ya 100
 
Mtu wa dini yeyote akiiva sana kwenye mambo ya dini jua umaskini anaukakaribia pia PERIOD

Kwanini masheikh wengi wameishia primary.!?
 
wanashindwa kuchanganua uhalisia wa mambo na mambo ya kusadikika.... penye kuwa halisi wao wanakuwa kusadikika ndo tatizo....
 
Shetani mpinga wokovu yupo JamiiForums leo. Maombi yanahitajika ili kuweka mambo sawa. Ila mkae mkijua kwa Yesu hakuna umaskini, waliookoka ambao ni masikini wajichunguze kama kweli wameokoka
 
michango yote ile ya kuchangia suti ya baba mchungaji, kununu gari la mke wa mchungaji, fungu la kumi unapangiwa kiasi .....utabaki mtu???
ndo maana unaona walio juu wananunua mihama we unapukutika tu kwa imani ya kijinga...

Mungu tunaamini yupo ila wenzetu kwakweli wanaipeleka imani kuliko hata MUNGU alivyosema
 
2po walokole wenye ela tumenyamaza siri kubwa ni kumtolea MUNGU kwa uaminifu atakubariki si kweli kabsa kua walokole ni maskini....

naomba unisaidie hela ya kula leo tu
 
Wanamchangia FLORA mbasha saa ngapi watatajirika?? mil 9???
Mwenzao anatanua wao wanakufa njaa.
 
Ni sababu ya kubadilisha mfumo wa maisha yake ya awali. Na kuamini kuwa Mungu atampa hata asipofamya kazi na kila jumapili kutoa michango kanisani. Hivyo anakuwa anatoa bila ya kuingiza.
 
Kwa habari ya umaskini wa kipato tunashuhudia kimaandiko pale Paulo alipowakumbusha Wakorintho akisema:-
“Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.” (2.Kor.8:9)
 
Shetani mpinga wokovu yupo JamiiForums leo. Maombi yanahitajika ili kuweka mambo sawa. Ila mkae mkijua kwa Yesu hakuna umaskini, waliookoka ambao ni masikini wajichunguze kama kweli wameokoka

Umeona eee!! Hii itakuwa roho ya mpinga Kristo.Inataka kuwakatisha watu tamaa.
 
Sio ajabu hata Zakayo yule mtoza ushuru aliyekuwa tajiri baada ya kuonana na Yesu aliitwa kachoka kama ulivyosema. Lakini ukweli aliujua mwenyewe na Mungu wake....

Soma LUKA 19:5-8

5Yesu alipofika pale chini ya huo mkuyu, akatazama juu, akamwambia, "Zakayo, shuka upesi, kwa maana leo nitakuwa mgeni nyumbani kwako!" 6Hivyo Zakayo akashuka upesi, akamkaribisha Yesu nyumbani kwake kwa furaha kubwa.
7Watu wote walioona, wakaanza kunung'unika wakisema, "Amekwenda kuwa mgeni wa ‘mtu mwenye dhambi.' "
8Lakini Zakayo akasimama na kumwambia Bwana, "Tazama, Bwana! Sasa hivi nusu ya mali yangu ninawapa maskini, nami kama nimemdhulumu mtu ye yote kitu cho chote, nitamrudishia mara nne ya hicho kiwango."
 
Mtu wa dini yeyote akiiva sana kwenye mambo ya dini jua umaskini anaukakaribia pia PERIOD

Kwanini masheikh wengi wameishia primary.!?
Hao tusiongelee hapa, tujadili hoja iliyoletwa kwanza.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom