Jibu ni rahisi sana... Je inawezekana kwa mtoto wa mfalme kuwa masikini?. Alie-okoka anakuwa mwana wa Mungu. hivyo Kwenye ulimwengu wa Kiroho yeye ni "prince" na ulimwengu wa Kimwili yeye Ni "mfalme".
kwamaana imeandikwa "Kwake Yeye aliyetupenda na ambaye ametuweka huru kutoka katika dhambi zetu kwa damu Yake,
akatufanya sisi kuwa ufalme na makuhani, tumtumikie Mungu Wake ambaye ni Baba yake. (ufunuo.1:5-6)" na pia imeandikwa "Lakini ninyi ni taifa teule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu la Mungu, mlioitwa ili kutangaza sifa Zake Yeye aliyewaita kutoka gizani mkaingie katika nuru Yake ya ajabu. (1peter.2:9)"
KWANINI WENGI WANAOKOKA WANAKUWA MASIKINI?
Yesu mwenyewe alisema "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hadi sasa, Ufalme wa Mungu hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka" (mathayo:11:12). Kwahiyo mtu akitaka kuokoka lazima aamue kwelikweli... kwamaana wokovu hupatika kwa nguvu. Na baada ya mtu kuamua kuokoka hapo ndio shetani nae huanza kazi yake kuhakikisha anarudi kwake (kwahiyo kila ambae hajaokoka bado ni washetani)
Kwanza mtu anaeokoka huyo ndie wa Kristo kwani Kuokoka ni Kubatizwa kwa Roho Mtakatifu (sio kama huko kubatizwa kwa maji). Pia mtu ambae hataki kuokoka yeye Bado ni washetani kwamaana imeandikwa "Yeyote asiye na Roho wa Kristo yeye sio wa Kristo (warumi.8:9)"
MAPIGO MATAKU KWA KUTOKA KWA SHETANI DHIDI YA ANAEOKOKA
Mtu akiokoka na kama ni mvivu wa kusoma neno mara nyingi hupigwa mapigo haya matatu na shetani ili awe mfano mbaya kwa wenzake na hivyo wenzake wengi wakatae wokovu/kuokoka.
PIGO LA 1.
Shetani atamdanganya alieokoka na kumfanya mtu huyo adhani utajiri ni dhambi... (hivyo wengine huishia kuuza mali zao na kukubali kuwa masikini)
Mlokokole huyo anaweza kudanganywa kwasabu Halijui NENO vizuri na hajui kuwa imeandikwa "Kwa maana mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo,
kwamba ingawa alikuwa tajiri, kwa ajili yenu alikubali kuwa maskini, ili kwa umaskini Wake ninyi mpate kuwa matajiri.(2korintho.8:9)"
Kwa mwana wa Mungu pesa zote anazomiliki ni za Mungu na kwaajiri ya kutimiza mapenzi ya Mungu. Lakini kwa mtu wa shetani utajiri wote ni wake na kwa ajili ya mapenzi yake wala sio ya mungu. kwahiyo mtu wa shetani ameweka tumaini lake kwenye hela hivyo mtu kama huyo ni mwabudu pesa na watu kama hawa ndio Yesu alisema "ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu"
PIGO LA 2.
Shetani anamdanganya na kumfanya mtu aanze kuimba na kusema masuala ya siku za mwisho mda wote
Yote hii ni kwasabu mtu huyo hajui kuwa siku za mwisho zilisha anza tangu siku ya Pentekoste pale ambapo Roho Mtakatifu alimwaga duniani. kwani imeandikwa "
Katika siku za mwisho, asema Bwana, nitamimina Roho wangu juu ya wote wenye mwili"(matendo.2:17).
KWAHIYO MPAKA TUNA MIAKA 2014 YA SIKU ZA MWISHO. Lakini asielijua hili hadanganywa na shetani kiasi kwamba anakuwa mvivu na kutofanya kazi akizani sasa ndio siku za Mwisho. ndio maana Pualo alisema "asiefanya kazi na asile"
PIGO LA 3. Ni mtu baada ya kuokoka tu ghafla huanza kuhubiri injili pasipo mpangilio wowote na kila mahali...
mtu huyo mlokole mpya hufanya hivyo kwasababu bado hajasoma kuwa imeandikwa "
Kuna wakati kwa ajili ya kila jambo, nayo majira kwa kila tendo chini ya mbingu: (mhubiri.3
🙂" na tena mbele kidogo imeandikwa "kuna wakati muafaka na utaratibu wa kila jambo (mhubiri.8:6)"
Hivyo mtu huyo huonekana kanakwamba amechanganikiwa baada ya kuokoka... na kwanjia hiyo watu huishia kudharau wokovu hadi wengi wao wanakufa pasipo wokovu. THIS IS BIG LOSS kwamaana imeandikwa "mwandamu amewekewa kufa mara moja tu na baada ya kufa akabili hukumu ( angalia waebrania.9:27)". kwahiyo atakaekufa bila ya wokovu atahukumiwa.
MTU KUWA MASIKINI NI KWASABABU HALIJUI NENO VIZURI. na hapo ndioo shetani anaamuwa kupatumia vizuri kwani anaeokoka katika nyakati za mwanzo huwa halijui neno vizuri.
Kuna silaha za Mungu 6 (waefeso.6:10-18)
1. Kweli
2. Haki
3. injili ya amani
4. imani
5. wokovu/kuokoka (waefeso.6:17)
6. upanga wa Roho ambao ndio neno.
Yote haya YAKO chini ya msingi wa moambi
ALIEOKOKA ANAZO SILAHA ZOTE 5 yaani kuanzia ya 1-5 lakini hiyo silaha ya sita hupatikana kwa kusoma Neno la Mungu (biblia).
Kwahiyo UKIONA MTU NI AMEOKOKA HALAFU ANAKUWA MASIKINI UJUE HILO NI PIGO LA SHETANI KWASABABU HUYO ALIEOKOKA HALIJUI NENO VIZURI. Yaani mtu huyo bado hana hiyo silaha ya Sita.