Kwanini hili jambo halifanyiki mjini?

Kwanini hili jambo halifanyiki mjini?

aise

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2018
Posts
7,459
Reaction score
20,963
Nyumbani kule kijijini kuna vikundi vinaitwa "vikundi vya maafa na kusaidiana"
Hivi ni vikundi unaweza kukuta kijiji kizima kuna kikundi kimoja au viwili.
Familia karibia zote wamejiunga, awe mwalimu au mkulima.

Ada ya kujiunga kwa mwanachama mgeni ni Tsh 2,000 tu.

Wanachama wake pindi mwanakijiji apatapo tatizo, hukusanyika na kuchanga kila mtu sh 500,
Hii mia tano ukizidisha kwa wanakijiji wote inapatika hela nyingi sana ambayo kwa kawaida inatosha matibabu na ghalama zingine.

Changamoto yake ni pale mwaka unaisha na kwenye familia yenu hakuna anayeugua, kwahiyo nyie itakuwa ni mwendo wa kuzitoa 500 kila ngoma ikilia.
Ila siku ukipatwa na matatizo lazima uyasahau machungu yote,
Maana kijiji chote watakuchangieni.
Kwanini hili jambo halipo mjini?
 
Mjini yapo mkuu kama hamna anza kumobilize watu mfanye ivo kwa mtaa wako.
 
Mjini tunatumia whatssap kama haupo ni wewe ndio tatizo.
 
Kwasababu UAMINIFU ni Changamoto.

Trust issues.
 
Kwasababu UAMINIFU ni Changamoto.

Trust issues.

Mkuu, hata kijijini uaminifu ni changamoto.
Ila kwa kijijini watu ambao sio waaminifu hata wao hawachangiwi.
Kwa kawaida mtu anayejitoa sana kwenda kutoa 500 katika kila ngoma inapopigwa, basi huyu siku akipata tatizo au familia yake ikipata tatizo anakuwa na hazina yake tayari ameiweka kwa wanakijiji, watamiminika wengi kuja kutoa michango.
 
Kwahiyo kama familia haipati majanga unaombea ili tu uchangiwe?

La hasha! Hiyo ni kama BIMA tu.
 
Ishi na watu vizuri mkuu.
Mjini yapo tena tumeboresha binafsi ninavyo vitatu kimoja tupo watu 35 kila harusi haijalishi ni machozi ama furaha mchango ni elfu30
Sikwambii hivi vingine😃😃
 
Ishi na watu vizuri mkuu.
Mjini yapo tena tumeboresha binafsi ninavyo vitatu kimoja tupo watu 35 kila harusi haijalishi ni machozi ama furaha mchango ni elfu30
Sikwambii hivi vingine
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom