Kwanini hifadhi ya fedha za kigeni imeshuka na dola imeadimika mtaani?

Mwande na Mndewa

JF-Expert Member
Feb 26, 2021
949
2,865
Jibu rahisi ni kwamba balance of payment haijakaa vizuri,tunachopeleka nje kina thamani ndogo kuliko tunachoingiza nchini kutoka nje,hivyo tunatoa dola (foreign currency) nyingi kuliko tunavyopokea,fikiria ununuzi wa mabehewa kwa ajili ya treni ya SGR unafanyika kwa fedha za kigeni,jibu lingine ni kupanda kwa bei za mafuta kumechangia,maana kama ulikuwa ukitumia dola milioni moja kuagiza lita X za mafuta baada ya kupanda utahitaji dola zaidi kuagiza kiasi kile kile,na jibu lingine Kama kutakuwa na usimamizi mzuri, kilimo pekee kinaweza kuleta mapinduzi katika biashara na kubadili thamani ya kubadili fedha.

Kama mazao yote yataongezwa thamani kabla hayajauzwa nje, nchi itapata fedha nyingi… unaweza ukaona hata madini tunayasafirisha yakiwa hayajaongezwa thamani, jambo ambalo si zuri kwa mustakabali wetu kiuchumi kama nchi,Kwa maoni yangu, sababu kwa nini export na import zina-corelate na thamani ya shilingi ni kwa sababu mara nyingi uchumi ukikua na kukomaa tunakuwa na bidhaa nyingi zenye ubora sana na kuna uwezekano zaidi wa watu wa nje kuzihitaji, na hivyo demand yake ya nje itaongezeka kwa kuwa tumekuza uchumi wetu kwa kutumia exports (exports led growth).

Ili sarafu (currency) yoyote ifanye kazi lazima kuwe na uaminifu (trust),lazima watumiaji waamini kwamba currency hiyo thamnani yake ni imara (stable),wasipoamini hivyo watapunguza matumizi yake au kuacha kabisa,na thamani yake itazidi kuporomoka,trust ni muhimu kwa currency yoyote,hata kama umei-peg kwa gold,lazima mtu aamini kwamba thamani ya gold haitashuka kamwe,Ili kitu chochote kitumike kwa ajili ya kubadilishana thamani,nilazima kitu hicho kiwe na guarantee of value,yaani ili mimi nikupe dhahabu wewe unipe yale makaratasi ya dollar,

Uhakika wa uthamani ni muhimu,ni lazima kuwe na guarantee some where kwamba nikipeleka hayo makaratasi nitapata thamani inayokaribiana na thamani ya dhahabu zangu,makaratasi hayo tumekubaliana yaitwe dollar,Without this guarantee no one would use the currency as the medium of exchange,tunaitumia dhahabu kama currency,sababu haina explicit guarantee ya value, lakini mtu atakuwa tayari kubadilisha bidhaa yake na dhahabu (Gold)kama anaamini kwamba baadaye atarudisha thamani yake kwa kuibadilisha hiyo gold na kitu kingine chenye thamani sawa na hiyo,kuna wakati chumvi ilitumika kama currency, kwa sababu wakati huo watu walikuwa wanaamini kwamba akibadilisha kitu na chumvi atarudisha thamani yake hapo baadaye.

Uwingi wa rasilimali tuliyojaaliwa Watanzania,hauwezi kudhani kiwango cha matumizi ya Dola nchini kikafikia kiasi cha kuwa na madhara kwenye uchumi wetu,sasa ukiona benki kuu imesema hifadhi ya dola imepungua(dola ndio tumekubaliana iwe kipimio) inamaanisha demand(hitaji) la dola ni kubwa kuliko supply(upatikanaji),hivyo expenditure ya forex (matumizi ya dola)ni makubwa,kumaanisha tunatumia (spend) kwa dola (forex) kuliko dola (forex) tunazoingiza,hii maana yake tuna import zaidi kwa kutumia dola (forex) kuliko export ya forex income zetu,hivi karibuni tumekuwa na miamala mingi(Telegraphic Transfers) kwa ajili ya kuagiza mizigo China na uturuki,

-Swali,
Kama Watalii na mikopo ya masharti nafuu vinaongezeka kwa nini fedha za kigeni zipungue?

Hakuna ndege itabeba pesa kuleta Tanzania,zaidi ya mzungu kuja na briefcase mkononi na kukabidhi hundi (cheque) ya benki yao uko ulaya na pesa hizo zitahamishwa kama shilingi pale hitaji linapotokea, kama madolari ya mikopo yangebebwa na meli na kuingizwa katika mzunguko wetu wa fedha,basi zingeweza kusababisha upatikanaji wa dola katika soko letu la fedha,hivyo kuongezeka thamani shilingi yetu,fedha za mikopo ziingiapo kwenye mzunguko,zinasaidia kupunguza uhaba wa dola na kusababisha dola kuuzwa kwa bei nafuu na kuchangia kupandisha thamani ya Shilingi,leo dola moja ya Marekani inanunuliwa kwa shilingi 2,370 pengine January dola moja inaweza kununuliwa kwa shilingi 2,400

Uchumi wetu ukikomaa,uzalishaji ukaongezeka hata kama ni kwa ajili ya mahitaji ya ndani tu, ajira zikaongezeka, etc, hata kama exports hazitapanda kihivyo kuna uwezekano wa thamani ya shilingi kupanda,Hayati Rais Magufuli walau alithubutu kupigia kelele viwanda viwanda viwanda,agenda ya viwanda kwa sasa nayo imekufa na dira ya nchi hatuelewi ni ipi,naamini tuna tatizo sehemu ujamaa ulituathiri kama taifa,angalia hata mtanzania anavyotembea barabarani kwanza anasalimia kila mtu na wakati huo anatembea kwa kuburuza miguu yaani hayupo faster kabisa,not smart at all,tupo kiujanja ujanja tu kama sungura,

Nimalizie kwa kusema sisi ndio shilingi kwa maneno mengine dollarisation has created weak demand for Tsh.sijui tunafeli wapi,kushuka kwa uchumi na pesa kukosa thamani itapelekea people shunning away from Tshs,inamaana Tsh is becoming cheaper na ndio matokeo yanayoonekana,itapelekea inflation na effect ya inflation in the end consumer wanaloose appetite ya local currency.If the worse comes to the worse,itakuja watu wanaanza kubadilishana vitu kuepuka kutumia madafu,Je, utapendekeza tuweke sheria kwamba watu hawaruhusiwi kubadilishana vitu?mliopewa dhamana ya uchumi wetu, kindly solve the core problems,tusisubiri madhara ya inflation,Case study Zimbabwe.

Nikiishia hapa, Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854

-Bachelor of Business Administration in International Business.

-Master of Leadership and Management.

Recent Publication;-
-Assessment on the effect of Micro-Financing on Poverty Reduction.
 
Nimeusoma huu Uzi wore umetoa ufafanuzi mzuri-hasa katika ambitious projects zinazofanywa na viongozi wetu zinazochangia kupeleka hela nje kutokana na wakandarasi hizo kufanywa na wazawa.
Hata hivyo, katika muda huu Nchi mbalimbali duniani zimetokea kupunguza kuweka akiba zao katika USD na kupunguza kutumia $ katika ununuzi wa bidhaa na huduma hii imetokana na mgogoro kati ya Russia & NATo.kwa hiyo ni vyema kujua sababu halisi kutokana kwenye taarifa ya B.O.T.

Vilevile,Serikali ya USA imepunguza ugavi wa notes zake-notes nyingi zinazo printiwa wakati huu zinapelekwa Ku isaidia Ukraine dhidi ya Russia,kama ni mfatiliaji mzuri Mr.Putin alilionhelea hili.Kumbuka USD inatumika Dunia nzima kama notes nyingi zikipekwa huko Ukraine maana yake ugavi wa USD sehemu zingine zitapungua-na yeye hawezi kuongeza kiwango cha notes maana atasababisha matatizo ya kiuchumi Nchini mwake.

My point is inawezekana Nchi ikawa na uhaba wa fedha za kigeni hapa tunazungumzia USD but kwa wakati huu sababu isiwe kushuka kwa production Bali hicho nilichokisema hapo juu.
 
Kama hatuzalishi chochote na tunaagiza tu karibu kila kitu hii hali lazima itukute. Na bado. Walio madarakani hawaonyeshi jitihada zozote za kututoa kwenye mkwamo wa kuagiza kila kitu, na hawawezi maana wamegawana hizo biashara za kuimport vitu. Inabidi feasibility ya kuback pesa yetu na gold iangaliwe, maana yanaweza kutukuta ya Zimbabwe.
 
Nikiangalia shilingi ya UGANDA naona ya kwetu bado hatupo pabaya
kilichopo wanaojiitaga wasomi wetu wa uchumi wafanye jambo kuokoa jahazi tusizame tuone uwezo wao sio kujiita wasomi bila vitendo
 
Nashauri pesa zinazotumwa na ndugu zetu wa diaspora zipunguziwe au kuondolewa makato na matozo ili kuwapa hamasa na motisha kutuma zaidi na kuchangia pato la taifa.
(Sina uhakika huwa zinatozwa au kukatwa kiasi gani!)
 
Nichangie hoja kwa .mtazamo tofauti. Wengi wanachukulia uchu.mi kuwa ni sawa na kujenga nyumba ikikamilika basi umenaliza kila kitu, sio hivyo kabisa. Uchumi kuyumba au flactuate ni kawaida kwa chumi zote dunia nzima hata kwa mataifa yaliyoendekea kama USA, UK nk. Hivyo siku zote parameters za uchumi zitabadilika badilika kutegemea hali na si suala la kukimbilia kulaumu kuwa fulani hakufanya hivi au vile. Mfano vita vya Urusi na Ukraine peke yake vimeleta athari kwa mataifa ya dunia nzima yasiyohusika kwa lolote na vita hivyo.

Tatizo la kiuchumi linapotokea au kugundulikac kwanza wachumi huanza na kuangalia sababu na ukubwa wa tatizo pili huanua mitigation measure ipi inafaa zaidi , lakini measures zingine zinahitaji kushughulikiwa kiutawala na zingine inabidi kwanza miswada ipelekwe bungeni kupitishwa; uponyaji au upunguzaj madhara hutegemea kuna uharaka kiasi gani tangu kugundua tatizo hadi kulipatia tiba tatizo,, wenzetu wa nchi zilizoendelea tatizo hugundulika mapema sana kwa sababu wana mfumo imara wa kucapture data hivyo mitigation measure hufanyika haraka sana ( hili sio suala la kulaumu kwani ni la kiuwezo zaidi na uwezo hatulingani).

Lakini wakati wa implementation kutibu tatizo inafuatiwa na kuangalia kwa karibu matokeo ya uponyaji kama unaenda ilivyokusudiwa. Pia hatua za uponyaji huibua pia madhara mengine kiuchumi hivyo huandaliwa hatua zingine za kutibu sideeffect za tiba kubwa mfano ukichukua hatua za kushusha inflation tatizo la ajira huongezeka (sideeffect). Kwa ufupi masuala ya kiuchumi kila wakati litatokea hili utafanya vile ukifanya vile litatokea lingine hivyo hakuna kumaliza kazi kama vile kujenga nyumba tofauti na watu wanavyolaumu au kufikiria.

Kuna wakati fedha za kigeni huingia nchini kwa wingi na kuna wakati uingiaji wa fedha hupungua sana, mfano wakati wawekezaji wanaleta mitaji nchini kuanzisha uwekezaji au wakati wa msimu wa kuuza mazao kama korosho, pamba nk fedha za kigeni huwa nyingi na demand ya shilingi huwa juu hivyo thamani ya shilimgi dhidi ya dola huimarika. Kuna wakati fedha za kigeni hutoka nje zaidi mfano hao wanaoitwa wawekezaji kama wamewekeza katika bidhaa zinazouzwa ndani tu au ndani zaidi kama sukari , mafuta ya kula, pipi, icecream nk wanaposafirisha faida kwenda makwao kwa ajili ya kulipa wanahisa wao/ wamiliki hapo demqnd ya fedha za kigeni huwa juu na matumizi huwa makubwa na pesa ya kurepatriate faida makwao hutegemea fedha iliyouzwa pamba, kahawa , korosho nk hivyo lazima akiba ya fedha za kigeni itaathirika.

Humu kuna watu wanapigia debe sana viwanda lakini mimi nasena viwanda sio suluhisho bali vinaweza kuwa tatizo zzidi kama viwanda hivyo vinamilikiwa na wageni. Nchi inaweza kuuza malighafi na bado ikapata fedha nyingi za kigeni kuliko hicho mnachosemq kuongeza thamani mazao. Australia wanauza zaidi malighafi iron ore zaidi na natural resources zingine na mazao ya kilimo na mifugo lakini GDP yao ni USD Trillion moja na ushee wakati ni nchi yenye idadi ndogo ya watu kuliko Tanzania. Nchi nyingine ni New zealand nayo inauza mazao hayohayo ya kilimo lakini wako vizuri. Uchumi hauendeshwi kwa, amri za marufuku kuzuia watu kuuza nje kwa kisingizio cha kuongeza thamani. Kwanza hizo bidhaa zako unazotaka kuongeza thamani zina ubora wa kushindana na bidhaa za nje, bei yake ni nafuu hadi unafikisha sokoni? Kumbuka bei ya umeme tu inakutoa kwenye ushindani kiuzalishaji. Una teknolojia ya kutengeneza hizo bidha? Eti kuna mtu anasema mqdini tuyaongezee thamani! Wewe unaweza kugeuza hayo madini kuwa mashine au items mbalimbali? Umaweza kutumia madini ya colbat kutengeneza simu au laptop? Unaweza kutumia almasi kutengeneza mashine ya kuchimbia mafuta kwa mfano? Uchumi sio mwendo wa kulaumu tu na kukurupuka kimaamuzi.

Nb: miradi mingi inayosifiwa sasa kuwa ni uwekezaji wenye kuongeza ajira na mapato huko mbeleni ni kilio upande wa fedha za kigeni na itachangia sana kuongeza pressure kwenye outflow ya dillar.
 
Nikiangalia shilingi ya UGANDA naona ya kwetu bado hatupo pabaya
kilichopo wanaojiitaga wasomi wetu wa uchumi wafanye jambo kuokoa jahazi tusizame tuone uwezo wao sio kujiita wasomi bila vitendo
Naona hata TZS imestabilize dhidi ya KES kwa mieizi hii mitatu au minne mfululizo.
 
Back
Top Bottom