Kwanini hatuna sera ya kugharamia matibabu kwa magonjwa yaliyoshindikana kutibiwa hapa nchini?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,372
Siku 3 au 4 zilizopita niliona kupitia Star tv mtoto mdogo akiwa na uvimbe mkubwa sana usoni uvimbe ambao matibabu yalishindika kufanyika hapa ndani ya nchi.

Kwa mujibu wa Star tv,mtoto huyo alitibiwa hospitali ya mkoa Mbeya,hospitali ya kanda na baadae hospitali ya Taifa Mhimbili ambako nako matibabu yake bado yalishindikana na anatakiwa kupatiwa matibabu nje ya nchi.Kwa waliomuona mtoto huyo bila shaka watakubaliana nami kuwa picha ile inasikitisha na kuumiza sana.

Mtoto huyo anaehangaika na mama yake kujitokeza katika vyombo vya habari kuomba msaada wa fedha ni mfano tu wa watanzania wengi ambao wamekuwa wakijitokeza katika vyombo vya habari kuomba msaada wa wasamaria wema katika kugharamia matibabu yao ndani na nje ya nchi.

Jambo hili huwa linaniumiza sana na nakumbuka niliwahi kuliongelea hapa JF siku za nyuma. Kinachonisikitisha na kuniumiza ni kuona watanzania hawa wanaoteseka na maradhi haya wakijitokeza mbele ya camera ili tu kuomba msaada wa fedha ili hali serikali yao ipo!Serikali ni kwanini inashindwa kuwa na sera ya kugharamia matibabu ya watu wake kwa magonjwa yaliyoshindikana kutibiwa hapa nchini?

Haingii akilini kuona Raisi,Raisi Msaafu,Makamu wa Raisi Mstaafu, Waziri Mkuu,Waziri Mkuu Mstaafu,Mawaziri,Wabunge na Vigogo wengine Serikali wakitibiwa nje ya nchi wakati mwananchi masikini akiteseka kwa maradhi huku akiomba msaada wa matibabu kutoka Taasisi na watu binafsi ili kuokoa maisha yake. Tukumbuke serikal ndio yenye wajibu wa kujenga hospitali na pia kutoa ruzuku kwa hospitali hizi ili mwananchi wake apate huduma bora za afya na kama imeshindwa basi serikali ndio ina wajibu wa kumgharamia mtanzania huyu apate matibabu popote pale ndani na nje ya nchi.

Pamoja na kuwepo utaratibu wa "cost sharing" katika hospitali za umma, watanzania wengi hawana bima za afya, hawamudu gharama kubwa za matibabu kwa baadhi ya magonjwa na hata matumizi ya Bima za kawaida nayo bado yako limited kwa baadhi ya magonjwa.

Nafikiri wakati umefika tuwe na sera ya kugharamia matibabu yaliyoshindikana ndani ya nchi na baadhi ya magonjwa yanayotibika hapa nchini lakini yanagharama kubwa sana kwa mtanzania wa kawaida.

Kiongozi mzuri,awe Raisi,Waziri au Mbunge,ni yule atakaetumia nafasi yake serikalini au ndani ya Bunge kuhakikisha tunakuwa na sera ya aina hii si kila wakati viongozi hawa kujitolea kugharamia matibabu ya watanzania hawa kila wanapojitokeza katika vyombo vya habari kuomba misaada.

Nakumbuka hivi karibuni ilitoka taarifa kuwa serikali inajiandaa kusitisha kupekeka watu nje kwa ajili ya matibabu kwa kuboresha hospitali ya Muhimbili ila binafsi naamini bado tu kuna magonjwa hayatatibika hapa nchini na hivyo serikali haiwezi kukwepa jukumu hili ambaolo mara nyingi ni kugharamia vigogo wa serikali na si mwananchi wa kawaida.

Kama kuna sera ya aina hii(jambo ambalo siliamini),basi sera hiyo na sheria zake zitakuwa mbovu na zenye mapungufu makubwa kwani zitakuwa hazina msaada sana kwa mtanzania wa kawaida na hivyo zinatakiwa(kama zipo) kupitiwa upya.

Wabunge wote bila kujali vyama vyenu mna wajibu wa kupeleka hoja binafsi Bungeni juu ya jambo hili na si kuisubiri serikali ambayo kila wakati inahitaji kusukumwa au chama chake ku-copy na ku-paste sera za wenzao kama vile ile sera ya elimu bure, n.k.
 
Ni kama lile la Magufuli kumchangia 10m binti kipofu!nampongeza kwa hilo...ila kama linge kuwa endelevu kwa kutungiwa sera na sheria pamoja na miongozo yake tungefika mbali
 
Hawajastukia mkuu.Wakishtukiza wataweka sera nzuri.
Wanaweza wasishituke kwasababu wao wana sheria zinazowapa upendeleo wa kutibiwa nje ya nchi kwa magonjwa yaliyoshindikana na hata yale yanayoweza kutibiwa nchini.Isitoshe Bima zao ni za hali ya juu ukilinganisha na hizi zetu.
 
Wanaweza wasishituke kwasababu wao wana sheria zinazowapa upendeleo wa kutibiwa nje ya nchi kwa magonjwa yaliyoshindikana na hata yale yanayoweza kutibiwa nchini.Isitoshe Bima zao ni za hali ya juu ukilinganisha na hizi zetu.
Ni kweli mkuu kwa haya uliyoandika.Tuliowatuma waandike sheria wamerujeuka sasa wamekuwa watetezi wa serikali.Ndio hiyo tena 70% hawana elimu ya kutosha.Tunapelekwa tu sababu ya wajinga wengi.
 
Mkuu Salary slip sera ipo na inafanya kazi, ingawa inaweza kuwa haifanyi vizuri kwa utendaji wa kibinadamu. Serikali imekua ikigharamia matibabu ya wananchi wake nje na ndani ya nchi toka zamani tu. Wengi hawatangazwi, wanaotangazwa sana ni wale wanao saidiwa na wasamalia ambao wao wakisha kusaidia lazima wakutangaze kwenye media kama uthibitisho wa matumizi ya hela walio kusaidia kwa walio wachangia, au kutangaza Jina la NGO yao. Kinachokosekana katika utekelezaji wa sera hii ni taarifa ya wanufaika kwa umma na uwazi wa upatikanaji wa huduma hii. Wizara ya afya Kuna kitengo cha kushughulikia wagonjwa wa aina hii. Kinachotakiwa ni madaktari wa hospitali ya Taifa kushauri hivyo baada ya kujua kwamba mgonjwa husika atanufaika na matibabu nje ya nchi....wapuuzie wale wanao tumia nafasi zao kwenda kufanya check up na kutibiwa kamasi. Kuna maskini wengi nimewashuhudia wakipelekwa nje kutibiwa tena wakisindikizwa na wauguzi kwa gharama ya serikali.
 
Reuben James, sasa mbona huyu mrembo aliyepofuka, iliposhindikana Muhimbili ameagizwa aende clouds tv?
Kwanini asingeelekezwa kwenye kitengo husika na kama mrimba haupo lichukuliwe kama tatizo la kitaifa?
Unaonekana ni mwandani kidogo kwenye mambo ya afya, je hii bajeti ya afya ya sasa imetenga kiasi gani kwaajili ya watu kutibiwa nje?
 
Reuben James, kwanini rais hakutumia fursa ya huyu mwanadada kuadress tatizo hili kitaifa?
Je impact ya rais kutoa mil. 10 kwa huyu mtu mmoja kitaifa ikoje?
Je, haiwezekani kwamba rais anatuma ujumbe kwa wote wanaotakiwa kutibiwa nje na wasio na uwezo wamfuate?
Je, kama rais ameonyesha roho ya kujali na huruma kwa huyu atashindwaje kwa hao wengine?
Nafikiri rais angetumia nguvu kubwa kuifanya system ifanye kazi, nafikiri hii ilikuwa fursa ya rais kuwa critical juu ya huduma ya watu kutibiwa nje.
Nafikiri hii ilikuwa fursa ya rais kukitask kitengo husika kuwa functional kwenye swala hili na mengine kama haya.
Angefanya hivyo, serikali yake ingesifika na kuheshimika!
Ila kwa alivyofanya amejipatia sifa mwenyewe na maswali mengi kuhusu utendaji wa serikali yake kama system na hasa utendaji wa wizara ya afya.
 
Reuben James, sasa mbona huyu mrembo aliyepofuka, iliposhindikana Muhimbili ameagizwa aende clouds tv?
Kwanini asingeelekezwa kwenye kitengo husika na kama mrimba haupo lichukuliwe kama tatizo la kitaifa?
Unaonekana ni mwandani kidogo kwenye mambo ya afya, je hii bajeti ya afya ya sasa imetenga kiasi gani kwaajili ya watu kutibiwa nje?
Hiki ndocho hata mimi kinanishangaza. Wagonjwa kila siku wanaomba misaada ya fedha kugharamia matibabu nje ya nchi na mpaka wengine wanapewa form/barua maalumu za kuwatambulisha mitaani kuwa wanahitaji msaada na hivyo wachangiwe.

Isitoshe,kuna mama mmoja marehemu(Hawa Ngulumu kama sikosei) aliewahi kuwa mkuu wa wilaya ya kinondoni, nakumbuka mama huyu baada ya kustaafu alikuja kuugua na alihitaji kutibiwa nje ya nchi ila aliachwa akahangaika mpaka habari zake zilipoandikwa na Mwananchi ndio serikali ikaona aibu na kumpeleka nje(India) kwa matibabu.Hii sera kama kweli ipo, basi itakuwa ni moja ya sera mbovu kabisa katika nchi hii.
 
This is it Salary slip, this is seeing the bigger picture and creating a sustainable and perfoming system through policies and laws.
Big up, good idea!
Mkuu nimeenda shule ila umeniacha njiani
 
Back
Top Bottom