Kwanini Hapi anakaimu nafasi ya Makonda?

Kwanini Hapi anakaimu nafasi ya Makonda?

Heshima kwenu wana Jf, nikiwa naangalia taarifa ya habari ITV leo saa mbili jioni, nimemwona mkuu wa wilaya ya kinondoni Mh Ally Hapi akiwapongeza Zantel kwa kulipa deni la Ml300, hapo hapo mtangazaji akimwita "kaimu mkuu wa mkoa wa dar es salaam." Mwenye kujua atujuze sababu ya Mh Paul Makonda kukaimiwa, au yupo likizo? Natanguliza shukrani.
Maswali mengine yanatia kichefuchefu jinsi yalivyo ya kijinga!!!
 
Kwa kawaida RC akiwa safari au likizo kuna DC mmoja wapo huwa ana kaimu nafasi hiyo. Lakini ni yule Senior zaidi ya wengine na sidhani kama Hapi ni senior kwa wengine waliopo. Mambo yanakwenda shagalabagala sasa hivi kama club ya pombe ya Wanzuki au dengerua
na kwa waliopo senior ninyule Dada wa Ilala... ila kwakuwa hana MIHEMKO kama wenzake hawezi kukaamishwa... alitakiwa naye awe MTU wa kujitoa ufahamu
 
Heshima kwenu wana Jf, nikiwa naangalia taarifa ya habari ITV leo saa mbili jioni, nimemwona mkuu wa wilaya ya kinondoni Mh Ally Hapi akiwapongeza Zantel kwa kulipa deni la Ml300, hapo hapo mtangazaji akimwita "kaimu mkuu wa mkoa wa dar es salaam." Mwenye kujua atujuze sababu ya Mh Paul Makonda kukaimiwa, au yupo likizo? Natanguliza shukrani.
makondA yupo likzo £@USA
 
Makonda kaenda kula bata huko ughaibuni, inawezekana ile safari ya kwenda kupandikiza mtoto kwa mujibu wa Mange Kimambi imetimia, sie wana shilawadu tutaanza kuhesabu miezi tu, tuoneshwe new born kwenye instagram.
 
Wakuu,

Kisheria nafasi ya Mkuu wa Mkoa akiwa Safari au nje ya Mkoa basi Mkuu wa Mkoa jirani atapaswa kukaimu nafasi hiyo, hivyo hivyo Kwa DC pia DC wa Karibu na wilaya atakaimu nafasi ya DC Kwa kipindi chote atakachokuwa nje ya ofisi na RC ndiye atakayemteua atakayekaimu nafasi ya DC

Kwa upande wa RC basi Waziri mwenye dhamana atamteua RC wa kukaimu. DC hapswi kukaimu nafasi ya RC hivyo hivyo Afsa Tarafa hapaswi kukaimu nafasi ya DC.

DC atamwakilisha RC tu endapo RC atakuwa nje au anadharura. Nafasi ya RC hukaimiwa na RC na siyo DC Kwa sababu viapo vyao ni tofauti kabisa!

Naomba kuwasilisha
Mkuu umenena sawasawa kabisa sasa sijui tatizo la wakuu wa wilaya kusemwa wanakaimu nafasi ya Mkuu wa mkoa linaanzia wapi?ama ni kwa vyombo vya habari au kwa wenye nafasi hizo kutoelewa utaratibu.Hata hivyo Mkuu wa Wilaya anaweza kukaimu Ukuu wa Mkoa iwapo ataapishwa na Rais kukaimu nafasi hiyo.Serikali ya awamu ya nne ilitoa mwongozo mzuri wa kukaimu nafasi ya mkuu wa mkoa/wilaya lakini haukufuatwa sana kwa nafasi ya mkuu wa mkoa mara nyingi wakuu wa mikoa wanapokuwa likizo au safarini humkaimisha mmoja wa wakuu wa wilaya katika mkoa wake
 
Back
Top Bottom