Kwanini Hapi anakaimu nafasi ya Makonda?

Kwanini Hapi anakaimu nafasi ya Makonda?

Ceremonial leader kama mkuu wa mkoa nae analikizo ? Nasubir kusikia mkuu wa chuo kikuuu flan nae kaenda likizo
 
Seniority has no mashiko, mimi ni mtu mdogo nakaimu post kubwa tu ofisini na kuna wakongwe kibao.

Watu wanaangalia braiiiiin yako tu
 
Heshima kwenu wana Jf, nikiwa naangalia taarifa ya habari ITV leo saa mbili jioni, nimemwona mkuu wa wilaya ya kinondoni Mh Ally Hapi akiwapongeza Zantel kwa kulipa deni la Ml300, hapo hapo mtangazaji akimwita "kaimu mkuu wa mkoa wa dar es salaam." Mwenye kujua atujuze sababu ya Mh Paul Makonda kukaimiwa, au yupo likizo? Natanguliza shukrani.

Mkuu wa wilaya kukaimu nafasi ya Mkuu wa mkoa ni jambo la kawaida sana wala siyo habari ya kujadili ila RC makonda atakuwa na issue binafsi.
 
Seniority has no mashiko, mimi ni mtu mdogo nakaimu post kubwa tu ofisini na kuna wakongwe kibao.

Watu wanaangalia braiiiiin yako tu
Kwa mfano nani angekaimu nafasi hiyo hapo DSM ukiondoa RC wa pwani
 
Kwa kawaida RC akiwa safari au likizo kuna DC mmoja wapo huwa ana kaimu nafasi hiyo. Lakini ni yule Senior zaidi ya wengine na sidhani kama Hapi ni senior kwa wengine waliopo. Mambo yanakwenda shagalabagala sasa hivi kama club ya pombe ya Wanzuki au dengerua
... Dengelua not Dengerua... Hii ni Pombe ya heshima aisee...
kweli kikore dendelua ni moja ya pombe za asili ya Kitanzania yenye heshima sana.
... Ilo nilo idi Ambiere...
 
Mbona wakati wa awamu ya nne Mhe Melsadick akiwa mkuu wa mkoa wa Lindi aliwahi kukaimu mkuu wa mkoa wa Dar?
Hichi ndicho nilichokua naelewa kua mkuu wa mkoa flani akiwa nje ya ofisi basi mwenzake wa karibu anakaimu. Hii ya DC nilikua sifahamu.
 
Wakuu,

Kisheria nafasi ya Mkuu wa Mkoa akiwa Safari au nje ya Mkoa basi Mkuu wa Mkoa jirani atapaswa kukaimu nafasi hiyo, hivyo hivyo Kwa DC pia DC wa Karibu na wilaya atakaimu nafasi ya DC Kwa kipindi chote atakachokuwa nje ya ofisi na RC ndiye atakayemteua atakayekaimu nafasi ya DC

Kwa upande wa RC basi Waziri mwenye dhamana atamteua RC wa kukaimu. DC hapswi kukaimu nafasi ya RC hivyo hivyo Afsa Tarafa hapaswi kukaimu nafasi ya DC.

DC atamwakilisha RC tu endapo RC atakuwa nje au anadharura. Nafasi ya RC hukaimiwa na RC na siyo DC Kwa sababu viapo vyao ni tofauti kabisa!

Naomba kuwasilisha
 
Kwani hujui ni msimu wa mwisho wa mwaka na likizo ni jambo la kawaida?
 
Heshima kwenu wana Jf, nikiwa naangalia taarifa ya habari ITV leo saa mbili jioni, nimemwona mkuu wa wilaya ya kinondoni Mh Ally Hapi akiwapongeza Zantel kwa kulipa deni la Ml300, hapo hapo mtangazaji akimwita "kaimu mkuu wa mkoa wa dar es salaam." Mwenye kujua atujuze sababu ya Mh Paul Makonda kukaimiwa, au yupo likizo? Natanguliza shukrani.
Hapi anakaim kwa sababu ana uwezo mkubwa kiutendaji. makonda anakaimiwa kwa sababu zilizo nje ya uwezo wake
 
Swali hapa ni sababu ya Mkuu wa mkoa kukaimiwa, hatakama angekuwa amekaimiwa na mtu yeyote, nini hasa sababu ya yeye kukaimiwa? je anaumwa?, ama yuko likizo? just curious.

halafu ukijua anaumwa au yuko likizo utagain nini?

hivi hawa wajinga ajinga wanatoka wapi? umekula maharage ya wapi?
 
Back
Top Bottom