mkuu walidanganywa na kuingizwa mkenge na putin, bada ya putin kuona mambo hayaendi kama alivyodhania akaona alianzishe kule mashariki halafu israel wakijibu nchi nyingine za kiarabu ziingie vitani iwe songomingo ndio maana muda huo huo nae akazidisha vita ukraine akitegemea us watabanwa kule israel hawatatoa misaada ukrain. hivyo kiulaini atashinda vita. waarabu wana mkataba na israel unaitwa ABRAHAM pamoja na kipigo gaza hawajavunja mkataba. Waarabu wao ZILONGWA MBALI ZITENDWA MBALI.1. Alianza vizuri HAMAS kuwapigania wapalestina na waarabu kwa ujumla vita vyao dhidi ya mvamuzi wao sugu 7 Oct 2023.
2. Bahati mbaya waarabu hadi wapalestina wa West Bank wameufyata na kumwachia mtiti wote peke yake!
3. Mafanikio yake kwenye vita hivi yalikuwa:
a) Kumpata Israel kukubali kuongea.
b) Kumpata Israel kukubali kubadilishana wafungwa.
c) Kumfanya Israel na Marekani kuitambua sura ya HAMAS. Kumbe nani anaongea na gaidi?
4. Lakini alipo HAMAS sasa, ni heri angeamua kujitoa mhanga; yeye na jamii yake yote.
5. Kwamba wakati wa kubadilishana wafungwa, Israel anaendelea kukamata na kuuwa wapalestina wengine.
6. Kwamba walioachiwa wanaweza kuuwawa na hata kukamatwa tena wakati wowote.
7. Kwamba Israel kasema lengo lake ni kumfuta HAMAS duniani.
8. Kwamba lengo ni kumsubiri amalize kuachilia mateka tu, halafu akione cha mtema kuni!
View attachment 2827378
Kulikoni HAMAS kuendelea kukenua kinyonge hivi?