Kwanini Dr Ndalichako asijiuzuru?

Kwanini Dr Ndalichako asijiuzuru?

Status
Not open for further replies.
Kwa taarifa yako Mwalimu wangu Dr. Ndalichako ameleta mabadiliko makubwa sana katika Baraza la Mitihani. Jambo kubwa kabisa alilolifanya ni kuziba mianya ya wizi wa mitihani. Kumbuka kabla Dr. Ndalichako hajaingia baraza la Mitihani mitihani ilikuwa ikiuzwa kama njugu lakini kwa sasa wizi wa mitihani haupo tena. Bado tunawahiaji sana Wazalendo kama Dr. Ndalichako. Huwezi kumhukumu Dr. Ndalichako kwa tatizo la kiufundi ambalo linaweza kumtokea MTU yeyote unless ndugu yako barubaru unaagenda nyingine. Wazalendo katika nchi hii ni wachache na DR. Ndalichako ni mmoja wao. Tumhukumu kwa haki. Mimi nasema hivi bado tunamuhitaji na hakuna sababu ya msingi ya yeye kujiuzulu.
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imemsimamisha kazi na itamchukulia hatua za kinidhamu Mkuu wa Idara ya Utafiti, Tathmini na Huduma za Kompyuta, Joseph Mbowe baada ya uchunguzi kubaini kuwapo kwa dosari katika ukokotoaji wa alama za mitihani ya somo la Islamic Knowledge katika kompyuta.

Aidha, Wizara hiyo imeagiza Necta kukokotoa upya alama za mitihani ya wanafunzi wa kidato cha sita ya somo hilo waliofelishwa kwa bahati mbaya mwaka huu kutokana na dosari hiyo na tayari matokeo ya alama hizo yametolewa.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo na Ufundi, Philip Mulugo alisema Mei 28, mwaka huu, Wizara ilipokea malalamiko kutoka Baraza la Wakuu wa Shule za Kiislamu, dhidi ya matokeo ya wanafunzi wa kidato cha sita mwaka huu katika somo hilo.

Source: Habari leo

Kwa mantiki hii ilitakiwa na Dr Ndalichako ambaye ndio Mtendaji mkuu wa baraza hilo ni lazima kwa aina yoyote ile ajiuzuru kutokana na kadhia kubwa kama hiyo. Kwani athari walizopata wanafunzi hao walio athirika kisaikologia kutokana na makosa yao ni kubwa sana na vile vile gharama watakazo chukua kufanya marekebisho hayo. Huu ni uzembe mkubwa sana kwa mtu muungwana lazima kujiuzuru .
 
Hivi Kwanini Sheikh yule asiye na Msikiti ana asiye Mtanzania Alhaji Ponda Issa Ponda asigombee uraisi ? Maana wafuasi wake wako wengi Tanzania......
Wa kumshangaa ni yule anayehoji kuhusu mtu kuitwa au kuwa Sheikh bila ya Msikiti (wa kuongoza)!
Anayewaongoza Waislamu Msikitini katika swala zao tano za kila siku huitwa Imaam! sio Sheikh. Imaam kiujumla ni Muislamu yoyote yule aliyebalehe anaweza kuwa Imam na sio lazima awe Sheikh.

Halafu tuna Muadhini (si lazima awe Sheikh) ,"Daiyah" mwenye kuita watu katika Uislamu(si lazima awe Sheikh) n.k.

Kosa la kuchanganya Usheikh na Uimamu au Muadhini au Daiyah ninaweza kulielewa kama litafanywa na John, Joyce au Joseph...Lakini mtu mwenye kudai kuwa na ilmu halafu kuangukia kaika kosa kama hili?! mhh.
 
Kwanini Nchimbi , IGP Mwema, Kamanda Kamuhanda hawajiuzulu kwa tukio la Iringa, hivi tukio na NECTA na Islamic knowldge lipi Ni baya na ambalo linahitaji watu wawajibike, Hivi nyie ndugu zetu (Waislam ) Baadhi yenu Vichwa vyenu vimejaa Madudu au Matope

wewe ndo hujui ki2 unakurupuka 2 @ madudu cjui matope??
Tatizo lako hujui maana ya kiongozi bora na muwajibikaji.
Kwa kifupi ngoja nikusaidie.
Kiongozi bora ni yule anayekubali kuwajibika endapo tatizo likitokea kwenye kitengo chake ili aipe uhuru tume itayoundwa kumchunguza.
Hichi ndicho wanachokikosa viongozi wengi humu nchini kwa kuwa ving'ang'anizi pale wanapofanya makosa au kuhisiwa.
Chukua mfn uliotokea miezi kadhaa iliyopita Barclays na sehemu nyingi 2 hapa Duniani.
Daima ntampongeza Lowasa kwani alifanya kitendo cha kishujaa sana. Badilika ndg sio kuwakumbatia viongozi wasio waadilifu ktk kazi zao. Kuachia ngazi ukiharibu kazi ni muhimu kwa taifa hili lililojaa viongozi wasio waadilifu.
 
Kwanini Dr Shukuru Kawambwa asijiuzulu ?.

Haitakuwa busara kwa Dr Shukuru Kawambwa kujiuzulu kwa sababu HILI BARAZA LA MITIHANI ni entity yenye sura ya Muungano.

Ukirejea kwenye Article of Union utaona Wizara ya Elimu ya Dr kawambwa inafanya kazi mpaka kigamboni kwani kuna Wizara kama hiyo huko Zanzibar lakin Baraza la mitihani la Taifa lipo moja tu.

Ndio maana nikabainisha wazi Baraza hilo lina sura ya Muungano na nikabainisha wazi kuwa ili sura hiyo iwe wazi ni lazima uwekwe utaratibu ule wenye sura ya Muungano kama zilivyo wizara za muungano au mashirika na taasisi za Muungano kama ilivyo BOT.

Kwa msingi huo Katibu Mtendaji mkuu wa Baraza hili ndio wa mwisho kimamlaka na Kauli ya naibu waziri wa Elimu (Muungano) haina nafasi Znz kwani nako kuna waziri pia.

kama una ziada mkuu ongezea hapa.

 
Leo nimekumbuka maneno ya Rais Kikwete pale aliposema kuwa kuna baadhi ya wakurugenzi na watendaji wake wanafanya madudu kwa makusudi ili waziri husika aadabishwe, kwahiyo huyu mama ni mmoja wapo, ni vema nae akawajibishwa!
 
Leo nimekumbuka maneno ya Rais Kikwete pale aliposema kuwa kuna baadhi ya wakurugenzi na watendaji wake wanafanya madudu kwa makusudi ili waziri husika aadabishwe, kwahiyo huyu mama ni mmoja wapo, ni vema nae akawajibishwa!

Kwa hiyo wewe unamwamini sana Kikwete?
 
Wewe ndio kilaza, tena kilaza kweli kweli. Nafikiri ishu imeshawekwa wazi kwa jinsi gani ilitokea na hatua gani zimechukuliwa kwa mkubwa wa department inayohusika. Sasa juu ya nini muendelee na mashambulizi kwa Katibu Mkuu ambaye hawajibiki moja kwa moja kubadili 3 iwe 2 kama sio ukosefu wa akili?

Stupidly, unasema walifelishwa as if kuna mtu aliwakusudia, ili iwe nini?

Nikuulize kitu kimoja mkuu, kwanini ilipozama meli zanzibar Mv SKAGIT aliewajibika ni waziri? kwani yeye ndie alikuwa anaendesha meli ile? jibu lake ni kwasababu yeye ndio mtendaji wa mwisho katika wizara ile, kwa upande wa visiwani, sasa leo limetokea hili NECTA ndalinacho pia anatakiwa kujiuzuru
 
Ndalichako sio politicians ni mtendaji,mbona mnazunguka why not shukuru kawambwa waziri au kwa sababu anatoka bagamoyo????
 
Binafsi sioni sababu ya yeye kubakia hapo. Kwano kosa kama hilo la kiutendaji ni kubwa sana kwa jamii hasa ukizingatia kuwa limefungamana na mambo ya kiimani. Ikumbukwe ni siku nyingi sana waislam hao hao wa Tanganyika wamekuwa ma msururu wa malalamiko ya kudhurumiwa haki zao na Serikali yao.

Lakin ni funzo sana kwa Serikali ya JMTz kujifunza zaidi ikiwemo pamoja na kulifanya Baraza hilo la Mitihani kuwa na SURA YA MUUNGANO. Kwa kuamua kama Katibu mtendaji atatoka upande mmoja wa muungano basi naibu wake atoke upande wa pili wa Muungano kama ilivyo kwenye taasisi na wizara zote zenye sura ya Muungano kama BOT etc.

Lakin vile vile ikumbukwe tokea kuanzishwa kwa baraza hilo viongozi wake wakuu kama katibu mtendaji mkuu na naibu wake wote wamekuwa wakristo. Hakuna muislam hata mmoja na hapo ndipo panapozidisha mashaka kwa chombo hicho.

lakin mwisho za mwizi arobaini. sasa ukweli umedhihiri. Laazima Katibu mtendaji mkuu wa Baraza hilo lazima awajibike kwa kujiuzuru ikiwemo pamoja na kuwafikisha mahakamani kutokana na kuwa athri watoto hao kisaikologia na kuwapotezea muda wao.


unatakiwe uwe great thinker ndugu, basi kwa mantiki usemayo ya viongozi wa juu kuwa wakristo, yale ya sensa na kipengele cha udini yangewekwa.
 
Kwa taarifa yako Mwalimu wangu Dr. Ndalichako ameleta mabadiliko makubwa sana katika Baraza la Mitihani. Jambo kubwa kabisa alilolifanya ni kuziba mianya ya wizi wa mitihani. Kumbuka kabla Dr. Ndalichako hajaingia baraza la Mitihani mitihani ilikuwa ikiuzwa kama njugu lakini kwa sasa wizi wa mitihani haupo tena. Bado tunawahiaji sana Wazalendo kama Dr. Ndalichako. Huwezi kumhukumu Dr. Ndalichako kwa tatizo la kiufundi ambalo linaweza kumtokea MTU yeyote unless ndugu yako barubaru unaagenda nyingine. Wazalendo katika nchi hii ni wachache na DR. Ndalichako ni mmoja wao. Tumhukumu kwa haki. Mimi nasema hivi bado tunamuhitaji na hakuna sababu ya msingi ya yeye kujiuzulu.

Mkuu, hata kipindi cha Ndalichako mitihani iliwahi kuibiwa kwa kiwango cha juu, hata akatakiwa kujiuzulu. Alifanya press conference kukataa kujiuzulu. Mimi si support kujiuzulu kwa Ndalichako kwa hili la mitihani ya Islamic knowledge lakini si sawa kumuita ni mzalendo wa kweli. Angekuwa mzalendo wa kweli angejiuzulu mitihani ilipoibiwa baada ya kutoka Dr. Nkumbi.
 
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imemsimamisha kazi na itamchukulia hatua za kinidhamu Mkuu wa Idara ya Utafiti, Tathmini na Huduma za Kompyuta, Joseph Mbowe baada ya uchunguzi kubaini kuwapo kwa dosari katika ukokotoaji wa alama za mitihani ya somo la Islamic Knowledge katika kompyuta.

Aidha, Wizara hiyo imeagiza Necta kukokotoa upya alama za mitihani ya wanafunzi wa kidato cha sita ya somo hilo waliofelishwa kwa bahati mbaya mwaka huu kutokana na dosari hiyo na tayari matokeo ya alama hizo yametolewa.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo na Ufundi, Philip Mulugo alisema Mei 28, mwaka huu, Wizara ilipokea malalamiko kutoka Baraza la Wakuu wa Shule za Kiislamu, dhidi ya matokeo ya wanafunzi wa kidato cha sita mwaka huu katika somo hilo.

Source: Habari leo

Kwa mantiki hii ilitakiwa na Dr Ndalichako ambaye ndio Mtendaji mkuu wa baraza hilo ni lazima kwa aina yoyote ile ajiuzuru kutokana na kadhia kubwa kama hiyo. Kwani athari walizopata wanafunzi hao walio athirika kisaikologia kutokana na makosa yao ni kubwa sana na vile vile gharama watakazo chukua kufanya marekebisho hayo. Huu ni uzembe mkubwa sana kwa mtu muungwana lazima kujiuzuru .

Mkuu nakuunga mkono, hata hivyo haiwezi tu kuishia kwa Dr.Ndalichako kujiuzulu,lazima twende zaidi ya hapo. Kuna uzi nimepost kwenye jukwaa la siasa-moved to Jukwaa la Elimu na sasa topic Closed.[h=2](NECTA na matokeo batili ya mtihani somo la Islamic Knowledge!)[/h]Hii ndio Tanzania yetu na Religious Inbalance!
 
Nimependa hiyo ya Ponda

Halafu, hlili swala la mtihani wa dini kuwekwa ktk baraza la taifa... WHY , si watu waazishe mabaraza yao ya kidini, watoe mitihani yao.

Why kutumia pesa zetu, kugharimia mitihani ya KIDINI????
 
Wote ni vizuri sana na uungwana zaidi kwao kujitathmini na kuona uzito wa kosa kwa jamii na ukizingatia jamii ndio iliyogundua kosa hilo sio wao. Basi kiungwana walipaswa kujivua gamba.

Labda kwa kuwa utaratibu huo siku hizi haupo huko Tanganyika. Lakinkwa aina yoyote wote walitakiwa kung'oka ili kulinda hishma ya baraza hilo kwa watahiniwa na wananchi kijumla..

sasa kwa kuwa sasa umepata somo, na kuelewa kwanini, heading yako haikuwa hivyo kwamba waziri wa elimu na mkurugenzi wa Necta wajiuzuru au kufutwa kazi?
mbona hao makafir bila kujali itikadi zao kwnye suala la Daudi Mwangosi wamesema wazi wazi bila kuficha kitu kwamba nchimbi , mwema na kamuhanda waondoke bila kujali huyu ni muungwana na yule ni kafiri. ukiweka vitu vyako namna hii unakuwa objective na sio subjective, halafu hili la kusema murugenzi akitoka upande huu, naibu upande huu, je ratio ya upande huu na huu ipoje? maana ukiwa msomi mambo yako lazima yawe ya kisomi somi.
 
endelea kutukana coz umezoea, imani yangu hainifundishi matusi.

Kwenye mihadhara lengo ni kuelimishana na sio kukejeli, ndomana wachungaji na viongozi mbalimbali wa kikristo pamoja na waumini wao nao wanahudhuria.
Tungekuwa tunakejeli au kuwatusi wasingekuja.
Tena wanakuja wachungaji wajuzi wa uislam, wengine mpaka kiarabu wanaongea.
Lengo ni kuelimisha sio kutusi kama wewe unavyofanya.
Umenielewa mkuu?

acha uzuzu wewe soma kwanza.
 
Haitakuwa busara kwa Dr Shukuru Kawambwa kujiuzulu kwa sababu HILI BARAZA LA MITIHANI ni entity yenye sura ya Muungano.

Ukirejea kwenye Article of Union utaona Wizara ya Elimu ya Dr kawambwa inafanya kazi mpaka kigamboni kwani kuna Wizara kama hiyo huko Zanzibar lakin Baraza la mitihani la Taifa lipo moja tu.

Ndio maana nikabainisha wazi Baraza hilo lina sura ya Muungano na nikabainisha wazi kuwa ili sura hiyo iwe wazi ni lazima uwekwe utaratibu ule wenye sura ya Muungano kama zilivyo wizara za muungano au mashirika na taasisi za Muungano kama ilivyo BOT.

Kwa msingi huo Katibu Mtendaji mkuu wa Baraza hili ndio wa mwisho kimamlaka na Kauli ya naibu waziri wa Elimu (Muungano) haina nafasi Znz kwani nako kuna waziri pia.

kama una ziada mkuu ongezea hapa.

kwa hiyo necta itakuwa chini ya wizra gani? ya muungano iliyo chini ya ofisi ya makamu wa raisi? basi huyo waziri ajiuzulu, maana hakuna chombo chote tanzania hii kisicho chini ya wizara fulani?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom