Nsabhi
JF-Expert Member
- Feb 23, 2011
- 1,093
- 162
Kwa taarifa yako Mwalimu wangu Dr. Ndalichako ameleta mabadiliko makubwa sana katika Baraza la Mitihani. Jambo kubwa kabisa alilolifanya ni kuziba mianya ya wizi wa mitihani. Kumbuka kabla Dr. Ndalichako hajaingia baraza la Mitihani mitihani ilikuwa ikiuzwa kama njugu lakini kwa sasa wizi wa mitihani haupo tena. Bado tunawahiaji sana Wazalendo kama Dr. Ndalichako. Huwezi kumhukumu Dr. Ndalichako kwa tatizo la kiufundi ambalo linaweza kumtokea MTU yeyote unless ndugu yako barubaru unaagenda nyingine. Wazalendo katika nchi hii ni wachache na DR. Ndalichako ni mmoja wao. Tumhukumu kwa haki. Mimi nasema hivi bado tunamuhitaji na hakuna sababu ya msingi ya yeye kujiuzulu.
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imemsimamisha kazi na itamchukulia hatua za kinidhamu Mkuu wa Idara ya Utafiti, Tathmini na Huduma za Kompyuta, Joseph Mbowe baada ya uchunguzi kubaini kuwapo kwa dosari katika ukokotoaji wa alama za mitihani ya somo la Islamic Knowledge katika kompyuta.
Aidha, Wizara hiyo imeagiza Necta kukokotoa upya alama za mitihani ya wanafunzi wa kidato cha sita ya somo hilo waliofelishwa kwa bahati mbaya mwaka huu kutokana na dosari hiyo na tayari matokeo ya alama hizo yametolewa.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo na Ufundi, Philip Mulugo alisema Mei 28, mwaka huu, Wizara ilipokea malalamiko kutoka Baraza la Wakuu wa Shule za Kiislamu, dhidi ya matokeo ya wanafunzi wa kidato cha sita mwaka huu katika somo hilo.
Source: Habari leo
Kwa mantiki hii ilitakiwa na Dr Ndalichako ambaye ndio Mtendaji mkuu wa baraza hilo ni lazima kwa aina yoyote ile ajiuzuru kutokana na kadhia kubwa kama hiyo. Kwani athari walizopata wanafunzi hao walio athirika kisaikologia kutokana na makosa yao ni kubwa sana na vile vile gharama watakazo chukua kufanya marekebisho hayo. Huu ni uzembe mkubwa sana kwa mtu muungwana lazima kujiuzuru .