Kwanini binadamu tunaogopa KIFO?

Kwanini binadamu tunaogopa KIFO?

 
Habari zenu wakuu?leo nilikiwa nafkiria kuhusu kifo nikawa najiuliza hilo swali hapo juu,kwanini watu hawazoei kifo ingawa ni jambo ambalo huwa linatokea kila siku katika jamii?
Mtu unazaliwa mpaka unakua unasikia habari za watu kufa kwa namna moja au nyingine wakiwa watoto vijana na wazee hakichagui umri wengine ni watu wa karibu yako lakini bado hauzoei.

Kuna msemo unasema kila nafsi itaonja mauti na wengi wanalijua hili kwamba lazima tufe hata tufanyeje, ukiiishi kwa wema utakufa ukiishi kwa ubaya utakufa, ukiwa maskini utakufa ukiwa tajiri utakufa sasa kwanini tunaogopa wakati hiki kifo hakiepukiki?inafikia muda watu huogopa kudai haki zao za msingi kwa kutishiwa kuuwawa wakati anajua atakufa tu!
Hiki kifo kinatumiwa kama silaha na watawala kufanya mambo yao bila ya tabu.

kwanini wanapokufa watu wetu wa karibu huwa tunalalamika na kuhuzunika?
Kama wapo wasioogopa kifo au kuondokewa na jamaa zao nadhani dunia nzima hawazidi %5

sasa swali langu ni hilo kwanini hiki kifo hakizoeleki?
Je kwasababu ya kutopewa elimu juu ya jambo hili au elimu inayotolewa ni ya kubahatisha yani hao wanayoifundisha hawana uhakika na wanalosema?
mwisho tufanyeje ili tukizoee kifo tusikiogope?

karibuni wote tujadili wenye kuamini Mungu yupo na wasio amini uwepo wake,wenye dini na msio na dini karibuni sana.View attachment 1155838
 
Mkuu fear of the unknown ndio kinachotusumbua..
Watu hatuna uhakika na tunapoenda..
Lakini akija mtu kutoka upande wa pili akatuchana live mambo yalivyo baada ya kufa sidhani kama tutakua waoga tena
 
Mi siogopi kifo.... ukifa unapewa mademu 72 na raha za peponi. Why should l worry?
Mkuu hizo raha sidhani kama kila mtu kaambiwa atapata mpaka utimize vigezo na masharti.
 
Naamini watu wanogopa kuwaacha wapendwa wao, ndugu , jamaa na marafiki, starehe, anasa za dunia., dunia inanoga sana hata kama hauna pesa uhai unanoga sana..

Mpka sasa hakuna anaejua ukweli kuhusu after life na hilo ndyo jambo la kuogofya sana . hatujui tunakwenda wapi...

"Kuna siku nilifaint kwa sekunde kadhaa.. Kwakwei sikuhiisi chochote, sikujihisi popote.. Kila kitu kilizima kabisa..." Kifo kinaweza kuwa ivo ukifa umekufa
 
Kifo ni miongoni mwa mysterious ambayo inamtatiza Sana binadamu.
Wengi wanaogopa kifo lakini ukimuliza anaogopa nini hasa hukosa majibu,kwa ufahamu wangu pindi kiumbe hai kinapokufa(binadamu) hakuna kinachoendelea zaidi ya hapo anakuwa hayupo.
Ukifa umekufa hakuna kinachoendelea baada ya kufa.Swali la kujiuliza kwani mnyama anapokufa huwa anaenda wapi?
 
Kifo ni miongoni mwa mysterious ambayo inamtatiza Sana binadamu.
Wengi wanaogopa kifo lakini ukimuliza anaogopa nini hasa hukosa majibu,kwa ufahamu wangu pindi kiumbe hai kinapokufa(binadamu) hakuna kinachoendelea zaidi ya hapo anakuwa hayupo.
Ukifa umekufa hakuna kinachoendelea baada ya kufa.Swali la kujiuliza kwani mnyama anapokufa huwa anaenda wapi?
Utajuaje kuwa ukifa hakuna kinachoendelea maana hapo wewe tukikuuliza maisha yako ulipokuwa tumboni mwa mama yako huna hata unachojua ila kweli uliwahi kuishi tumboni,sasa kama maisha yako ya tumboni tu huyajui ndio utaweza kutuambia masuala ya mtu akifa?
 
It's all has do with your mind...

Kuna kipindi hali ya kuogopa kifo hukutokea... kuna kipindi unaona hata ukifa sawa tu...


Cc: mahondaw
 
Tunaogopa kwa sababu huko tuendako hatukujui na hatutarudi tena kuleta mrejesho.....
 
Ila trust me hatutaenda kokote mkuu Bali tunapokufa tunakuwa non-existed kama tunavyokuwa wakati hatujazaliwa.
Pale unapokosea jambo fulani nafsi huwa inakusuta kabla hujaambiwa kuwa ni kosa, tayari unakuwa umeshajua hili ni kosa, je unadhani umejuaje kuwa umekosea?? Huo ndio ushahidi kuwa ulikuwepo kabla ya kuzaliwa.
 
Naamini watu wanogopa kuwaacha wapendwa wao, ndugu , jamaa na marafiki, starehe, anasa za dunia., dunia inanoga sana hata kama hauna pesa uhai unanoga sana..

Mpka sasa hakuna anaejua ukweli kuhusu after life na hilo ndyo jambo la kuogofya sana . hatujui tunakwenda wapi...

"Kuna siku nilifaint kwa sekunde kadhaa.. Kwakwei sikuhiisi chochote, sikujihisi popote.. Kila kitu kilizima kabisa..." Kifo kinaweza kuwa ivo ukifa umekufa
Mi nliwahi kupigwa nusu kaputi na kufanyiwa upasuaji,nachokumbuka ni kabla ya sindano na hata fahamu zilikua zinarudi kwa shida...yaan sikuhisi hata kama nlilala yaan its like ume-skip movie
 
Mi nliwahi kupigwa nusu kaputi na kufanyiwa upasuaji,nachokumbuka ni kabla ya sindano na hata fahamu zilikua zinarudi kwa shida...yaan sikuhisi hata kama nlilala yaan its like ume-skip movie
And that's death bro
 
Issue ninkuacha vitamu vya duniani mapema na kutangulia , kila muda unavyosonga na utamu unazidi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom