Kwanini binadamu tunaogopa KIFO?

Kwanini binadamu tunaogopa KIFO?

Wengi tunaogopa kifo sababu hasa hatujui tuna poenda pia mazingira mengi mpaka unapata umauti yanakuja na maumivu, magonjwa, moto, ajali nk nayo ni sababu ndogo ya kuhofia kifo na mazingira mpaka unakufa

Lkn kuna watu wanasema kifo ni transition tu ya kawaida kutoka state moja kwenda nyingine na lengo ku experience hizo ‘states’ na ukifika state ya juu sana na kuwa ‘enlightened being’ siri zote za kifo na creations zinakuwa wazi kwako
 
Wengi tunaogopa kifo sababu hasa hatujui tuna poenda pia mazingira mengi mpaka unapata umauti yanakuja na maumivu, magonjwa, moto, ajali nk nayo ni sababu ndogo ya kuhofia kifo na mazingira mpaka unakufa

Lkn kuna watu wanasema kifo ni transition tu ya kawaida kutoka state moja kwenda nyingine na lengo ku experience hizo ‘states’ na ukifika state ya juu sana na kuwa ‘enlightened being’ siri zote za kifo na creations zinakuwa wazi kwako
Je kuna anaejua hizo siri za kifo hapa duniani?
 
Kuna kipindi kinafika mtu anaacha kabisa kuogopa kufa, nimeshapita huko
 
Hatuogopi kifo ila tunachukia na kuhudhunika watu wetu wa karibu tunaowapenda wanapotengwa nasi tena kwa kufukiwa kama malboro.

Hatuogopi kifo ila tunachukia jinsi kifo kinavyokuja kwa namna ya mateso kama ajali,kutekwa,magonjw,nk ila ingekua KIFO kinakuja kwa mtu kulala na kupitilizia humo humo usingizini (hamna ambae angekiogopa)

Ishu kubwa ni kinakuja kujaje...kikija kikinikuta usingizini (kije hata saivi sikiogopi) ila kama sijui kitakujaje (sitoacha kukiogopa)
 
KIFO Vs UHAI
Siku moja kifo alimuuliza uhai, " Hivi ni kwanini watu wanakupenda wewe na kunichukia sana mimi!?"
Uhai akajibu, "ni kwa sababu mimi ni MWONGO MZURI' ninayewadanganya kwa kila aina ya njia, tena waziwazi tu, lakini wewe ni MKWELI MUCHUNGU.
Kawaida watu wakiambiwa uongo wanaupokea na kuuamini haraka, lakini ukweli huwa ni vigumu kukubali kwa sababu unaumiza na hawapendi kukubali hali halisi."
Na hivyo ndivyo ilivyo.
 
Mtu anakwambia kifo ni kitu cha kawaida hivyo tusiogope ila yeye mwenyewe ni kama sisi kwamba hajawahi kufa na sidhani kama ukimwambia ajitolee kufa kama atakubali ili tuamini kweli kifo ni kawaida hakuna sababu ya kukiogopa.
 
All in all imani mbali mbali zimeleta complications kwenye swala la kifo, mfano adhabu ya kaburi na maisha baada ya kifo na wajanja wachache wanaongeza hiyo pressure ya kifo kama dhana ya kupata wafuasi na njia raisi ya kuwatawala. Yote kwa yote kila kitu kitarudi kwenye origin yake, kama tulikuwa kwa Mungu kabla ya uhai basi baada ya uhai tutarudi kwa Mungu na kama hatukuwepo kabla (uhai) basi baada (uhai) hatutakuwepo hivyo dhana kama Mungu, Moto, Pepo na Shetani zipo kumjenga binadamu kuwa kuna maisha baada ya kifo na atalipwa sawa na matendo yake hapa duniani.
Nimekuwa najiuliza kama kweli kuna Pepo na Moto basi vitakuwa ni vikubwa sana kiasi kwamba havijai kwa kuwa hakuna kifo tena wala kuisha tukifika huko mahali. Tokea kipindi hiko cha nyuma watu walipoanza kufa hadi leo wanakwendaga tu.
 
Ingekuwa basi watu wasingejilipua kisa dini ambazo zinawatia hofu ya kifo.
Dini imewajengea hofu kwa tricky, kwanza kuwahakikishia kuwa kuna maisha baada ya kifo na kuwajengea hofu kuwa usipoenenda kwenye njia hii hadhabu inaanzia kaburini kama nyoka, marungu n.k hadi uko motoni ambapo kuna Moto wa milele ambao ni mkali utachomwa bila kuisha ila ikawapa relief kuwa kuna Pepo ambayao Mungu ndo yupo uko kama utaenenda njia zake basi utapata furaha ya milele.
 
KIFO Vs UHAI
Siku moja kifo alimuuliza uhai, " Hivi ni kwanini watu wanakupenda wewe na kunichukia sana mimi!?"
Uhai akajibu, "ni kwa sababu mimi ni MWONGO MZURI' ninayewadanganya kwa kila aina ya njia, tena waziwazi tu, lakini wewe ni MKWELI MUCHUNGU.
Kawaida watu wakiambiwa uongo wanaupokea na kuuamini haraka, lakini ukweli huwa ni vigumu kukubali kwa sababu unaumiza na hawapendi kukubali hali halisi."
Na hivyo ndivyo ilivyo.
Una uhakika uhai na kifo vinaongea?au ni story tu
 
All in all imani mbali mbali zimeleta complications kwenye swala la kifo, mfano adhabu ya kaburi na maisha baada ya kifo na wajanja wachache wanaongeza hiyo pressure ya kifo kama dhana ya kupata wafuasi na njia raisi ya kuwatawala. Yote kwa yote kila kitu kitarudi kwenye origin yake, kama tulikuwa kwa Mungu kabla ya uhai basi baada ya uhai tutarudi kwa Mungu na kama hatukuwepo kabla (uhai) basi baada (uhai) hatutakuwepo hivyo dhana kama Mungu, Moto, Pepo na Shetani zipo kumjenga binadamu kuwa kuna maisha baada ya kifo na atalipwa sawa na matendo yake hapa duniani.
Nimekuwa najiuliza kama kweli kuna Pepo na Moto basi vitakuwa ni vikubwa sana kiasi kwamba havijai kwa kuwa hakuna kifo tena wala kuisha tukifika huko mahali. Tokea kipindi hiko cha nyuma watu walipoanza kufa hadi leo wanakwendaga tu.
Kifo ni kifo tu mkuu hakuna hata mmoja ambaye anaweza kujitolea kufa ili kuonesha kuwa kifo ni kitu cha kawaida,hata wasioamini maisha baada ya kufa nao pia hukiogopa kifo ingekuwa watu wanaogopa kifo kwa sababu za adhabu za kaburini au motoni basi wangeogopa kufanya hayo yanayopelekea kupata hizo adhabu kama ambavyo watu wanaogopa kufanya uhalifu kwa kuhofia kuishia jela.
 
Dini imewajengea hofu kwa tricky, kwanza kuwahakikishia kuwa kuna maisha baada ya kifo na kuwajengea hofu kuwa usipoenenda kwenye njia hii hadhabu inaanzia kaburini kama nyoka, marungu n.k hadi uko motoni ambapo kuna Moto wa milele ambao ni mkali utachomwa bila kuisha ila ikawapa relief kuwa kuna Pepo ambayao Mungu ndo yupo uko kama utaenenda njia zake basi utapata furaha ya milele.
Sasa wewe nenda kanisani au msikitini halafu watishe tu kuna bomu uone kama hao wenye kuenenda kwenye hiyo njia sahihi kama watabaki hapo,wote watakimbia kuepuka kifo.
 
Sasa wewe nenda kanisani au msikitini halafu watishe tu kuna bomu uone kama hao wenye kuenenda kwenye hiyo njia sahihi kama watabaki hapo,wote watakimbia kuepuka kifo.
Zipo sababu nyingi zinazofanya binadamu kuogopa kifo pamoja na watu kutojua wanapokwenda baada ya kifo huu ni udhaifu ulio wazi hivyo dini zimetengeneza theories mbali mbali ku pressure huu udhaifu kwa manufaa pengine yao binafsi au na Mungu, ingawa hakuna clear perspective yakusema hii ndio sahihi kuhusu kifo, hata ukiwauliza hao viongozi wa hizo imani (sijatumia Dini) watakwambia imeandikwa kwenye vitabu tena atakupa na mistari kabisa. Hivyo hata yeye binafsi nje na vitabu vitakatifu hajui chochote kuhusu kifo.
 
Ni nature ya kiumbe chochote chenye uhai kuogopa kifo. Sio binadamu tu hata wanyama wanaogopa kifo. Nadhani tumeumbwa kwa namna hiyo ili tuweze kusurvive katika hii dunia. Hivi kifo kingekuwa kitu Cha kawaida ni nani angebaki duniani?!
 
Hivi mbona wazungu huwa hawalii kama sisi? Sie mpaka kugaragara, yowe kali! Kuzimia hata kufa kabisa. Wenzetu hawanaga uchungu/upendo kama wetu au ni nini?
 
Hivi mbona wazungu huwa hawalii kama sisi? Sie mpaka kugaragara, yowe kali! Kuzimia hata kufa kabisa. Wenzetu hawanaga uchungu/upendo kama wetu au ni nini?
Hatuwezi kufanana na ndiyo maana kuna wazungu wakifiwa na mbwa tu anahuzunika na kufanya msiba kabisa ila sie huku tunashangaa na kuona ujinga.
 
Zipo sababu nyingi zinazofanya binadamu kuogopa kifo pamoja na watu kutojua wanapokwenda baada ya kifo huu ni udhaifu ulio wazi hivyo dini zimetengeneza theories mbali mbali ku pressure huu udhaifu kwa manufaa pengine yao binafsi au na Mungu, ingawa hakuna clear perspective yakusema hii ndio sahihi kuhusu kifo, hata ukiwauliza hao viongozi wa hizo imani (sijatumia Dini) watakwambia imeandikwa kwenye vitabu tena atakupa na mistari kabisa. Hivyo hata yeye binafsi nje na vitabu vitakatifu hajui chochote kuhusu kifo.
Mkuu pamoja na kukubali kuwa watu wanaogopa kifo kwa sababu mbalimbali ila bado wewe umekazania dini tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom