Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,259
- 20,914
- Thread starter
- #41
Sijaingia kwenye ndoa bado, so ntakujibu kile ambacho nakifikiria na ninachokishuhudia kwenye hizo ndoa....na ndo maana neno "labda" linahusika...
So nawaza labda kabla hawajaingia kwenye ndoa kila mtu alikuwa anajifikiria kama "yeye", Akitaka kufanya kitu "mimi" ndo ilikuwa inahusika zaidi yani ile Me, my self and I...
Lakini kumbuka ndoa inaleta muunganiko wa mambo yote, financial, social n.k
Baada ya ndoa hamna tena umimi bali ni "sisi"
Kama ulikuwa unatoa robo ya mshahara kupeleka kwenu sasa inabidi umshirikishe mwenzio, mapato na matumizi lazima yajulikane na yapitishwe....hapo ndo bifu zitaanza kwa sababu utahisi umeingiliwa uhuru wako...
Halafu sehemu nyingine watu wanayokosea ni ile tabia ya kuvumilia hata visivyovumlika kwa kujipa moyo kuwa baada ya ndoa mambo yatabadilika...
Watu tuna matumaini makubwa sana kabla ya ndoa, so mnapoingia kwenye ndoa na kuona mambo ni yale yale ndo hapo mnawaza kuachana.....!
Sidhani kama inawezekana kuishi pamoja miaka 8 halafu muwe mnaishi kwa aina ya mimi na sio sisi
Mtakuwa mmezaa na huduma zote zinafanyika kama wanandoa kinachokosekana hapo ni ile hati tu ambayo ndio kisheria inawafanya nyie kuwa wanandoa lakini kijamii nyie tayari ni wanandoa
Swali ni kuwa baada ya kudshirikiana yote hayo kwa muda wote huo,inakuwaje baada ya kuipata ile hati ambayo inatutambulisha kisheria kuwa ni wanandoa ndoa inatushinda?