Kwanini baada ya kuoana tumeachana?

Kwanini baada ya kuoana tumeachana?

^^
Kuna tofauti ya maisha kabla ya ndoa, ndani, na baada ya ndoa. Kabla ya ndoa ni kukubaliana ili usipoteze penzi, ndani ya ndoa ni sheria, na baada ya ndoa ni kanuni ya majuto na lawama.
^^
Hebu tukae hapo kabla ya ndoa .......

Haya mambo unayavumilia kwa miaka 8 halafu yanakuja kukushinda kumaliza hata mwaka baada ya ndoa?
 
Habari za jioni?

Ntumai mpo poa .....

Kama kawaida huwa siji na hoja hapa bila kuifanyia utafiti angalau kidogo na kupata mwanga,niliwahi kusikia na kusoma sana kwenye majarida na magazeti na zaidi nimeshuhudia watu wakiniambi jambo hili kuwa,kama kuna watu waliishi kwenye mahusiano kwa muda mrefu na kupendana na kuishi kwa amani kama mke na mume lakini hakukuwa na ndoa yaani yale makaratasi na ikaja wakaoana hupita muda mfupi na wanaachana

Nimekutana ma mahusiano ya aina hii ma 5 yaani watu walikuwa hawajaoana na waliishi maisha ya furaha kabisa lakini baada tu ya kuoana walitengana

Nilijaribu kuwauliza sababu hakuna aliyenipa sababu ya kushikika lakini kila mtu alikuwa anamtupia lawama mwenzake kuwa ndiuo alisababisha ndoa kufa,ukiwauliza kama ni mwenzake ni kitu gani kiliwafanya wasiachane wakati ule hawajafunga ndoa kunakuwa hakuna jibu

Hadi sasa sijapata jibu lakini kitu ambacho nina uhakika nacho kuna idadi kubwa sana ya mahusiano ambayo yamechukua muda mrefu nayalipokuja kubadilika na kuwa ndoa watu hawa ambao waliishi kwa amani muda mrefu sana wanaachana

Inawezekana kuna mtu ambae anaweza kuwa ana jibu ya hili naomba anijibu .....!!

kwani Mungu aliposema Msizini alikua na mana gani?
Hapo jibu ni moja tu mnapokua katika uchumba na kuzini mmnakua rafiki wa shetan sasa mnapofunga ndoa mnakua adui yake mana mshaingia ktk hatua bora lazima aingize mkono wake.
 
kwani Mungu aliposema Msizini alikua na mana gani?
Hapo jibu ni moja tu mnapokua katika uchumba na kuzini mmnakua rafiki wa shetan sasa mnapofunga ndoa mnakua adui yake mana mshaingia ktk hatua bora lazima aingize mkono wake.

Na wale ambao wanaachana kwenye huo uzinzi ni kitu gani kiliwafanya wakaachana?
 
So ushauri ni kuoana na mtu ambaye hamjawahi kukaa kwenye mahusiano ya muda mrefu kabla ya ndoa au?

^^
Hakuna kanuni moja inayotawala mahusiano ya aina zote. Hutegemea aina ya watu na kile kinachozaliwa baada ya tabia za wawili hawa kuambatana. Mahusiano ya uchumba sugu siyashauri. Yana changamoto nyingi ambazo ni mara chache kufikia katika ndoa. Wala uchumba wa muda mfupi sana si mzuri, unaficha mengi yanayoweza kuepukwa. Kila kitu kinahitaji kiasi.
^^
 
The devil at work. Kabla ya ndoa you are already his; siku ya ndoa mnamfukuza. Then anatafuta weak point (hasira, tamaa,chuki, wivu, uchoyo, ulafi, ulevi) then anajiattach na kuwaattack. Ndoa kaputi, back to uzinzi.
 
Hebu tukae hapo kabla ya ndoa .......

Haya mambo unayavumilia kwa miaka 8 halafu yanakuja kukushinda kumaliza hata mwaka baada ya ndoa?

^^
Miaka 8 upo kwenye uchumba? Unasubiri nini kitokee ambacho dunia haijui?.. Hayo ni mahusiano ya wizi, na aghalabu huishia kuvunja ndoa maana wezi wawili hawakai kichaka kimoja
^^
 
The devil at work. Kabla ya ndoa you are already his; siku ya ndoa mnamfukuza. Then anatafuta weak point (hasira, tamaa,chuki, wivu, uchoyo, ulafi, ulevi) then anajiattach na kuwaattack. Ndoa kaputi, back to uzinzi.

Sidhani kama nimekuelewa ......

Naomba ufafanuzi tafadhali!
 
^^
Miaka 8 upo kwenye uchumba? Unasubiri nini kitokee ambacho dunia haijui?.. Hayo ni mahusiano ya wizi, na aghalabu huishia kuvunja ndoa maana wezi wawili hawakai kichaka kimoja
^^

The thing is mmekaa kwamuda huo bila kufunga ndoa na nakuomba tu ufanye uchunguzi kwani haya mahusiano yapo sana,lakini baada tu ya kufunga ndoa mambo yanakuwa mengine

Kwanini?

Hilo ndilo swali la msingi!
 
ndio kwa mtazamo wangu

Kuwa na hakika kwa 100% inamaana kuwa there is no room for doubt,hii inamaana kuwa hakuna kuwa na uhakika wa kiwango hicho halafu ikawa kwa mtazamo wako

Sijui kama umenielewa!
 
Mkuu sidhani ...

Kwenye mahusiano ndio mahali ambapo unamuangalia mwenzako kama anakufaa,sasa mnapoingia kwenye ndoa hapo ni kufa na kuzikana na hapo ndipo ambapo uvumilivu unahitajika

Inakuwaje mmeishi kwa miaka mi 5 halafu mkisha funga ndoa tu hata mwaka hauishi mnakuwa mmeachana?

Sijaingia kwenye ndoa bado, so ntakujibu kile ambacho nakifikiria na ninachokishuhudia kwenye hizo ndoa....na ndo maana neno "labda" linahusika...

So nawaza labda kabla hawajaingia kwenye ndoa kila mtu alikuwa anajifikiria kama "yeye", Akitaka kufanya kitu "mimi" ndo ilikuwa inahusika zaidi yani ile Me, my self and I...
Lakini kumbuka ndoa inaleta muunganiko wa mambo yote, financial, social n.k
Baada ya ndoa hamna tena umimi bali ni "sisi"
Kama ulikuwa unatoa robo ya mshahara kupeleka kwenu sasa inabidi umshirikishe mwenzio, mapato na matumizi lazima yajulikane na yapitishwe....hapo ndo bifu zitaanza kwa sababu utahisi umeingiliwa uhuru wako...

Halafu sehemu nyingine watu wanayokosea ni ile tabia ya kuvumilia hata visivyovumlika kwa kujipa moyo kuwa baada ya ndoa mambo yatabadilika...
Watu tuna matumaini makubwa sana kabla ya ndoa, so mnapoingia kwenye ndoa na kuona mambo ni yale yale ndo hapo mnawaza kuachana.....!
 
Back
Top Bottom