Kwanini Askari wetu hubeba silaha za kivita!!

Kwanini Askari wetu hubeba silaha za kivita!!

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
25,176
Reaction score
48,460
Wamwela!!.jpg

Silaha kama hizi zilizobebwa na Askari hawa wa Jeshi la Polisi nchini mwetu zimekuwa ni zana za kawaida kabisa kubebwa na Askari polisi kwenye mikusanyiko ya watu wengi tena raia wasio na Silaha.

Sasa swali la kujiuliza ni kwa nini Askari wetu hao wabebe silaha za kivita dhidi raia wasio na silaha yoyote? Kwa mfano kwenye mikutano ya siasa kuna sababu gani ya kubeba silaha za kivita. Kwani polisi huwa wanahisi kuna jambo gani la hatari litakalotokea na kuhitaji ujibizanaji kwa kutumia SMG, LMG au AK 47?
 
Mimi hapo nawaona wapo porini wanasaka majangiri ndiyo maana wameshika kiona mbali(darubini), hakuna raia hapo
 
Ngoja tuwape kalamu ili ufurahi....
 
Wanazishika kuringishia nchi jirani waone nao wanazo, lakini jambazi mwenye panga anawamaliza na kuondoka na hizo silaha zao za kupigia picha.
 
Hata panga hutumiwa kama siraha ya kivita mf Rwanda na Liberia
 
Ungejaribu kuuliza kijiweni kwenu kwanza kabla haujatuletea humu huenda hata vijana wa maskani wangeweza kukupa jibu...
 
Magazine zenyewe wamefunga na mpira ,hatari tupu tu
Angalia vzr, wamebeba magazine mbili mbili... Kikawaida moja ndio inawekwa kwenye bunduki hiyo nyingine wameifunga(kuziweka pamoja) in case ya kwanza ikiisha unapachua na kupachika nyingine,
 
Angalia vzr, wamebeba magazine mbili mbili... Kikawaida moja ndio inawekwa kwenye bunduki hiyo nyingine wameifunga(kuziweka pamoja) in case ya kwanza ikiisha unapachua na kupachika nyingine,
Ni sawa mkuu hakuna vitu vya kufungia mpaka iwe mipira ya manati ??
 
Hili swali kila siku huwa najiuliza....
kuna watu hawaoni athari zake

lakini moja ya athari zake ni jamii kuzoea silaha kubwa zikiwa wazi ovyo ovyo
Mkuu mtutu hauzoeleki,
 
Unazoea silaha kwa kuziona tu? Sidhani hata huko wanakopigana wanaweza sema wamezoa kulengwa risasi.
 
Back
Top Bottom