Kwani lazima polisi wajue ninakotoka?

Kwani lazima polisi wajue ninakotoka?

Makamee, kwani ulizuiwa kutembea usiku?

Hawakunizuia ila maswali ya kuniuliza unatoka wapi ni kama vile yalilenga kua sina haki ya kutembea usiku.
 
Last edited by a moderator:
Hawakunizuia ila maswali ya kuniuliza unatoka wapi ni kama vile yalilenga kua sina haki ya kutembea usiku.

Nadhani ulilichukulia hilo swali vibaya au nao hawakulimalizia swali lao, huenda kulikua na tukio mahali wakataka kujua kama ndiko ulikotoka vile vile inawasaidia wao kujua mienendo ya raia kwahiyo nadhani Makamee hilo swali lisikusumbue ni mojawapo ya maswali ambayo ungeyategemea kwa wakati huo kama mwengine alivyosemakuwa ungeulizwa unaenda wapi
 
Last edited by a moderator:
Kwa jinsi nijuavyo mimi nchi hii hakuna zuio la watu kutembea usiku.

Ila kuna la kuhojiwa????!!!
We hujanasa tu tena inabidi "uungwe" doria halafu tukutane na mtu akiendesha baiskeli haina taa naye "aungwe" hakafu baiskeli unapewa wewe ukokote!!!!!!!!
 
Jamani kumbukeni hata Trafic wetu maswali yao ni ya kushangaza,
Anakusimamisha ukiwa na gari badala ya kukagua uzima na vielelezo vya gari anakuuliza mbona hujanyoa ndevu?
 
Huko kwenye mahijab huwa mnaficha mabomu na mihadarati. Ni haki yao kukusachi na kukuuliza.

umesahau pia kuna hawa

priest-gun.jpg



images
 
tatizo la polisi wa bongo badala ya kulinda wao wanawinda!
 
Ni haki ya polisi kujua unatoka wapi kama usiku umekomaa. ni maelezo yako ndio yatakupeleka pabaya au pzr.

Swali la kwamba natoka wapi kiukweli sijaona mantiki yake bora wangeniuliza unaishi wapi?
 
Na usikariri kwamba kila Makamee anaishi Zanzibar pengine,
nipo Nyololo-Irhnga
au Igunga-Tabora
au Mgori-Singida
au Bahi-Dodoma
au Utete-Rufiji
au Kabuku-Tanga
au Tengeru-Arusha
au nipo Mashati,Useri Rombo-Kilimanjaro.
 
Kwa jinsi nijuavyo mimi nchi hii hakuna zuio la watu kutembea usiku.
Kumbuka polisi akikusimamisha anayo mamlaka ya kukuuliza unatka wapi/unaenda wapi. Cha mzingi jibu na toa ushirikiano kisha endelea na uendako. Ukiwajibu vibaya ama usipotoa majibu basi watapata sababu ya kukusumbua
 
Back
Top Bottom