Kwani kudai Katiba mpya kuna dhambi gani?

Prof Koboko

JF-Expert Member
Aug 15, 2020
350
2,549
Hebu tuambizane ukweli, kudai katiba mpya kuna dhambi gani katika taifa hili mpaka kufikia hatua ya kufungulia na kesi za ugaidi? Kwani mjadala tu wa kuidai katiba mpya una tatizo gani hadi kufikia kukamata viongozi wote wa chama kimoja kilichotajwa kufanya mjadala huo?

Hivi ni kweli CCM hamchukui mifano kutoka mataifa mengine mkajifunza kua movement ya katiba ni suala gumu na kulizuia hamuwezi? Dunia imejua kua katiba ya Tanzania ina kasoro kubwa na ndiyo chanzo kikubwa cha ukandamizaji wa haki za binadamu.Hili suala limeamshwa kulizima ni ngumu maana si la CHADEMA pekee, mnakoelekea sasa mtakamata wanaharakati watakaoendesha mijadala hii na si wanasiasa pekee.

Mnamfungulia mashtaka ya Ugaidi kiongozi ambaye tangu kuanza kwake siasa akiwa kijana mdogo wa miaka 20 hajawahi hata kutuhumiwa kutishia kumpiga mtu achana na kuua, hiki mnachokifafanya kilianza kupata shinikizo la kimataifa tutakua salama?

Jeshi letu linatoa maelezo ya kujichanganya kua halijamkamata Mbowe kwa sababu ya mjadala wa katiba, sasa hao viongozi wengine wa CHADEMA wamekamatwa na kwenda kupekuliwa kwa sababu gani? Hii dhambi kubwa ya jeshi letu itatuvusha? Wanadhani hili jambo linaweza kuzimwa kwa wepesi kiasi hicho?

Hivi polisi wanaelewa maana na madhara ya kukamata kiongozi mkuu wa chama kikuu cha upinzani katika taifa lolote lile? Mbaya zaidi kumtuhumu kwa kesi ngumu kama ya ugaidi mtu ambaye hana historia ya matukio hayo maisha yake yote. Ngoja tupate mashinikizo ya jumuiya za kimataifa ndio tutajua,sisi tujawe na viburi vyetu lakini tutaelewa mbeleni.
 
Tanzania ni taifa la kipekee....hatufanani na hayo mataifa kwa mengi.....

Muungano wetu ni wa KIPEKEE....
Tulibahatika kupata "mtume mwafrika" ambaye alifuta UCHIFU....alifuta UKABILA....alifuta UDINI....

Mtume huyo mwafrika ,alipigania UKOMBOZI wa nchi zinazotuzunguka.....Nkrumah hakufanya hayo....Sekou Toure hakufanya hayo....Mandela hakufanya hayo....Kaunda hakufanya hayo.....Kamuzu Banda hakufanya hayo.......

TANZANIA ni "shock absorber" ya mataifa mengi....hususani yanayotuzunguka.......

KUIPINGA CCM NA MAMBO YAKE NI KUIPINGA JMT NA MUASISI WAKE

✓Kutaka katiba mpya ni kutaka SERIKALI 3 zitakazopelekea MUUNGANO uvunjike(wako watanganyika na Wazanzibari wanaitaka hayo).

CHADEMA wana sera ya MAJIMBO....je nayo katiba mpya tuingize MAJIMBO?!!!

Ethiopia inateketea kwa sera za MAJIMBO...watu wamekuwa wabaguzi kimajimbo....leo TIGRAY inataka kujitenga.....FEDERAL GOVERNMENT inapambana kuzuia hayo kwani ikiwa TIGRAY watafanikiwa basi ujue UASI utaamka katika majimbo mengine ,mwishowe TAIFA ZIMA KUBADILIKA .....

Kwanini WAASISI wa taifa la Ethiopia walishindwa kuliona hilo aliloliona hayati Baba wa taifa Julius Nyerere?!!!

Hapa ndipo tunaposema TANZANIA NI TAIFA LA KIPEKEE....

#KatibaMpyaSiHitajiLaKilaMtanzania
#JMTMilele
#KaziIendelee
#PundaAfeMzigoUfike
#MzigoNiUtulivuWetu
#MzigoNiAmaniYetu
 
Ufike mahali uache upumbavu watu kama nyie ndio mnaomshabikia Ole Sabaya, wapuuzi wa nchi hii nyie.
Sawa mkuu....

Humu ndani umewahi kuniona nikimshabikia ndg.Sabaya ?!!

Usitujumuishe sote Kaka...

#KaziInaendelea
 
Tanzania ni taifa la kipekee....hatufanani na hayo mataifa kwa mengi.....

Muungano wetu ni wa KIPEKEE....
CCM
FB_IMG_1601280139466.jpg


Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Kusema ukweli,tangu niifahamu CCM ilipoanzishwa mpaka sasa,sijawahi kuona kipindi chama kimekuwa kioga , kiongo, kijinga, kikatili,kishamba,kinafiki,kishetani na kimekosa kabisa rasilimali watu timamu kama kipindi hiki cha kuanzia 2015 mpaka sasa.
Ile CCM ya hoja imeondoka na Kikwete!!??
Tatizo ni nini?
 
Tanzania ni taifa la kipekee....hatufanani na hayo mataifa kwa mengi.....

Muungano wetu ni wa KIPEKEE....
Tulibahatika kupata "mtume mwafrika" ambaye alifuta UCHIFU....alifuta UKABILA....alifuta UDINI....

Mtume huyo mwafrika ,alipigania UKOMBOZI wa nchi zinazotuzunguka.....Nkrumah hakufanya hayo....Sekou Toure hakufanya hayo....Mandela hakufanya hayo....Kaunda hakufanya hayo.....Kamuzu Banda hakufanya hayo.......

TANZANIA ni "shock absorber" ya mataifa mengi....hususani yanayotuzunguka.......

KUIPINGA CCM NA MAMBO YAKE NI KUIPINGA JMT NA MUASISI WAKE

✓Kutaka katiba mpya ni kutaka SERIKALI 3 zitakazopelekea MUUNGANO uvunjike(wako watanganyika na Wazanzibari wanaitaka hayo).


CHADEMA wana sera ya MAJIMBO....je nayo katiba mpya tuingize MAJIMBO?!!!

Ethiopia inateketea kwa sera za MAJIMBO...watu wamekuwa wabaguzi kimajimbo....leo TIGRAY inataka kujitenga.....FEDERAL GOVERNMENT inapambana kuzuia hayo kwani ikiwa TIGRAY watafanikiwa basi ujue UASI utaamka katika majimbo mengine ,mwishowe TAIFA ZIMA KUBADILIKA .....

Kwanini WAASISI wa taifa la Ethiopia walishindwa kuliona hilo aliloliona hayati Baba wa taifa Julius Nyerere?!!!

Hapa ndipo tunaposema TANZANIA NI TAIFA LA KIPEKEE....

#KatibaMpyaSiHitajiLaKilaMtanzania
#JMTMilele
#KaziIendelee
#PundaAfeMzigoUfike
#MzigoNiUtulivuWetu
#MzigoNiAmaniYetu
Ivi kwani kuipinga CCM ni dhambi, je kuna jambo gani kuuuubwa la kujivunia kutoka CCM zaidi ya kutengeneza matabaka ktk jamii ie wao(watawala) na sisi(wananchi)
Kwani hatuwezi kuwa na serikali 3 lakini kila eneo Lina mamlaka yake ie tunayo serikali ya ZNZ je serikali ya Tanganyika iko wapi?
Huyo nyerere unayemzungumzia alishawahi kukiri udhaifu wa katiba tuliyonayo,pia changamoto za maendeleo ya tanzania(ujinga,maradhi na magonjwa) akatoa suluhu kuna tunahitaji siasa Safi, ardhi na watu, je Tanzania tuna siasa Safi kwa maana ya utawala bora, utawala wa sheria, uwajibikaji nk kifupi yeye mwenyewe nyerere alipenda tujikosoe sio kuwa miungu watu
Kwa kumalizia tu,Tanzania haifanani na haitafanana na taifa lolote kwa sababu tuna mila,desturi na tamaduni zetu tofauti zinazotulinda na kulinda umoja wetu mfano nani aliweka sheria kuwa kitoweo Tanzania lazima achinje muislami na sio DINI nyingine, licha ya kuwa na makabila mengi lakini tuna kiswahili kinawaunganisha wote
Kwaiyo hebu jaribu kuficha ujinga wako kidogo tu maana kuna muda hata kizazi chako kitakushangaa ikiwezekana kukukataa kabisa
 
Kila kikundi kulijitokeza ma kuanzisha harakati za Madai Yao wanayoona yanafaa kwa kuhamasisha vurugu itakuwa ngumu sana kutoboa Katika nchi hii maana suala la katiba linamvutano mkubwa KIASI Cha kututoa kwenye barabara kuu.

Awamu iliyopita alikataa kabisa lakini awamu hii wamekubali lkn apewe muda ili kuiwekea mkakati ili isikwame tena lakini hawa jamaa wanataka kulazimisha! Kila kitu.Kupanga ni kuchagua
 
Ndio alithubutu.....

SGR....
NDEGE...
BWAWA LA MWALIMU NYERERE....
MAKAO MAKUU YA SERIKALI DODOMA.....
UKUTA WA MBUGUNI MERERANI....

👆👆👆👆👆👆👆👆
Hayakuonekana huko nyuma

#KaziIendelee
Ivyo vitu ulivyotaja ni vizuri pale hali ya maisha ya watu inapokua bora ila kama bado hali ya maisha ni mbaya havina tija. Kimsingi maendeleo ya vitu yanakwenda na maendeleo ya watu Sasa hapa Tanzania hiyo SGR inamsaidia namna gani bibi yako kule kijijini ili awe na kipato Cha uhakika, hiyo mindege inawasaidiaje vijana kupata ajira na kuwa na kipato Cha uhakika, Hilo bwawa la nyerere linawezeshaji utawala wa sheria, haki za binadabu na uwajibikaji wa viongozi na wananchi. Kifupi hayo yote unayoyataja Kama hayataleta dhamani kwenye maisha ya mtanzania ni kazi bure tu kama tupo Korea kaskazini uchina na kwingineko
 
Madai Katiba Yapo.Hii dharau kwa Watanzania ni mbaya , kuzuia njia za busara mnawakomaza Watanzania wafikirie njia mbadala. Wazee wa Taifa hili na Wenye hekima wapo wapi!? Viongozi wa dini mpo wapi??
 
Kusema ukweli,tangu niifahamu CCM ilipoanzishwa mpaka sasa,sijawahi kuona kipindi chama kimekuwa kioga , kiongo, kijinga, kikatili,kishamba,kinafiki,kishetani na kimekosa kabisa rasilimali watu timamu kama kipindi hiki cha kuanzia 2015 mpaka sasa.
Ile CCM ya hoja imeondoka na Kikwete!!??
Tatizo ni nini?
Kikwete huyu mliyekuwa mnamuita dhaifu? Au kuna mwingine?
 
Ivyo vitu ulivyotaja ni vizuri pale hali ya maisha ya watu inapokua bora ila kama bado hali ya maisha ni mbaya havina tija. Kimsingi maendeleo ya vitu yanakwenda na maendeleo ya watu Sasa hapa Tanzania hiyo SGR inamsaidia namna gani bibi yako kule kijijini ili awe na kipato Cha uhakika, hiyo mindege inawasaidiaje vijana kupata ajira na kuwa na kipato Cha uhakika, Hilo bwawa la nyerere linawezeshaji utawala wa sheria, haki za binadabu na uwajibikaji wa viongozi na wananchi. Kifupi hayo yote unayoyataja Kama hayataleta dhamani kwenye maisha ya mtanzania ni kazi bure tu kama tupo Korea kaskazini uchina na kwingineko
Kwa hiyo hakuna uhusiano wa MAENDELEO YA VITU NA MAENDELEO YA WATU ?!!!
 
Back
Top Bottom