Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,713
May be kama ulikuja kwenye mashindano,lakini kama ni hoja ziko wazi na zinajisimamia zenyewe
Ni hiyari yako kuzikubali ama kuzikataaa,lakin tutaendelea kusimamia kile tunachokiamin
Kumbe unazungumzia kile unachokiamini na sio unachokijua
Kuna tofauti kubwa sana kati ya kuamini na kujua
Kuamini unaweza kuamini chochote na sio lazima iwe kweli
Unaweza kuamini wewe na Osama ni ndugu wa tumbo moja kabisa na hata Malkia Elizabeth no shangazi yenu
Lakini kujua kunaenda sanjari na utafiti pamoja na ushahidi
Huwezi kusema najua Osama ni mwanamke bila kuonesha kilichokufanya useme hivyo kwa ushahidi
Kama haya uliyoandika hapa ni imani yako inabidi uwatake radhi wana jamvi na uyapeleke haya maelezo yako kwenye nyumba zenu za ibada!!