Kwamba Wahutu na Watutsi siku hizi nao ni Watanzania?

Mgibeon

JF-Expert Member
Aug 7, 2011
11,141
20,787
Nilikua nafuatilia hotuba za muheshimiwa Rais alizokua akitoa huko Kigoma na Tabora wakati alipoenda kuzindua miradi mbalimbali ikiwemo barabara na miradi ya maji.

Katika kuongea kwake akasema kwamba Tanzania wakati inasisiwa na Baba wa Taifa ilikua na makabila 121, na katika jambo kubwa alilofanya na alilofanikiwa Hayati huyu ni kuwaunganisha watanzania wote pasikujali makabila yote.. Sasa katika kuongea akasema sasa Tanzania imekua na makabila 123 baada ya makabila mawili kuongezeka Wahutu na Watutsi..

Nimejiuliza sana, hawa ndugu zetu wameingia lini kwenye listi ya makabila yetu? Au kamaanisha kua wale waliohuku Tanzania wamepewa "ukabila" sawa tu na wale wanaopewa uraia"? Au muheshimiwa sana alikua anatania tu? Hebu ndugu zangu nifahamisheni kuhusu jambo hili zito, huenda mimi nilipitwa na habari za kurasimisha makabila haya ya jirani zetu.
 
Nimejiuliza sana, hawa ndugu zetu wameingia lini kwenye listi ya makabila yetu? Au kamaanisha kua wale waliohuku Tanzania wamepewa "ukabila" sawa tu na wale wanaopewa uraia"? Au muheshimiwa sana alikua anatania tu? Hebu ndugu zangu nifahamisheni kuhusu jambo hili zito, huenda mimi nilipitwa na habari za kurasimisha makabila haya ya jirani zetu.

Ni hivi:
Viongozi kipindi cha awamu ya nne walitoa uraia kwa lundo la wakimbizi kutoka Burundi, ambao ndani yake kuna watusi na wahutu

Kwa kuongezea,
Uraia huo uliotolewa kama njugu, inasemekana malengo yake ilikuwa ni kujinufaisha kisiasa, majimbo ya uchaguzi yalianzishwa maeneo waliyopelekwa wakimbizi, na kuna chama kimeongeza idadi ya wabunge wake kupitia hao wakimbizi

Usiku mwema.

 

Ni hivi:
Viongozi kipindi cha awamu ya nne walitoa uraia kwa lundo la wakimbizi kutoka Burundi, ambao ndani yake kuna watusi na wahutu

Kwa kuongezea,
Uraia huo uliotolewa kama njugu, inasemekana malengo yake ilikuwa ni kujinufaisha kisiasa, majimbo ya uchaguzi yalianzishwa maeneo waliyopelekwa wakimbizi, na kuna chama kimeongeza idadi ya wabunge wake kupitia hao wakimbizi

Usiku mwema.

Hapo umenifumbua macho Mkuu, Asante sana.
 
Nilikua nafuatilia hotuba za muheshimiwa Rais alizokua akitoa huko Kigoma na Tabora wakati alipoenda kuzindua miradi mbalimbali ikiwemo barabara na miradi ya maji.

Katika kuongea kwake akasema kwamba Tanzania wakati inasisiwa na Baba wa Taifa ilikua na makabila 121, na katika jambo kubwa alilofanya na alilofanikiwa Hayati huyu ni kuwaunganisha watanzania wote pasikujali makabila yote.. Sasa katika kuongea akasema sasa Tanzania imekua na makabila 123 baada ya makabila mawili kuongezeka Wahutu na Watutsi..

Nimejiuliza sana, hawa ndugu zetu wameingia lini kwenye listi ya makabila yetu? Au kamaanisha kua wale waliohuku Tanzania wamepewa "ukabila" sawa tu na wale wanaopewa uraia"? Au muheshimiwa sana alikua anatania tu? Hebu ndugu zangu nifahamisheni kuhusu jambo hili zito, huenda mimi nilipitwa na habari za kurasimisha makabila haya ya jirani zetu.
Nasikia eti ni Kada mtiifu na mwaminifu wa Chadema Lau Masha ndio alifanikisha suala hilo baada ya kuvuta chochote kitu kutoka shirika la UNHCR Geneva- Uswisi. Kipindi kile akiwa waziri wa mambo ya ndani serikali ya awamu ya nne.
 

Ni hivi:
Viongozi kipindi cha awamu ya nne walitoa uraia kwa lundo la wakimbizi kutoka Burundi, ambao ndani yake kuna watusi na wahutu

Kwa kuongezea,
Uraia huo uliotolewa kama njugu, inasemekana malengo yake ilikuwa ni kujinufaisha kisiasa, majimbo ya uchaguzi yalianzishwa maeneo waliyopelekwa wakimbizi, na kuna chama kimeongeza idadi ya wabunge wake kupitia hao wakimbizi

Usiku mwema.

Sema CCM ilishinikiza hawa banyamulenge na intarahamwe wapewe uraia ili waongeze idadi ya kura ktk chaguzi ya chama cha CCM.
Hawa intarahamwe hawakupaswa kupewa uraia kwa sababu ni muda mrefu kuna ndugu zao walishajipenyeza huku Tz, so wapo wengi kulikuwa hakuna haja ya kuongeza wengine.

Siasa za CCM ni hatari kwa taifa.
Huyu mwingine anaongeza ndugu zake officially, Nyerere alikuwa anawajua vizuri hawa lkn hakuwahi kusema tuna makabila 123
 
Nasikia eti ni Kada mtiifu na mwaminifu wa Chadema Lau Masha ndio alifanikisha suala hilo baada ya kuvuta chochote kitu kutoka shirika la UNHCR Geneva- Uswisi. Kipindi kile akiwa waziri wa mambo ya ndani serikali ya awamu ya nne.
Aiseeeee, sasa kwanini Rais wetu mwenye maamuzi magumu asisitishe huo uraia wao?
 
Sema CCM ilishinikiza hawa banyamulenge na intarahamwe wapewe uraia ili waongeze idadi ya kura ktk chaguzi ya chama cha CCM.
Hawa intarahamwe hawakupaswa kupewa uraia kwa sababu ni muda mrefu kuna ndugu zao walishajipenyeza huku Tz, so wapo wengi kulikuwa hakuna haja ya kuongeza wengine.

Siasa za CCM ni hatari kwa taifa.
Huyu mwingine anaongeza ndugu zake officially, Nyerere alikuwa anawajua vizuri hawa lkn hakuwahi kusema tuna makabila 123
Hapa kuna namna mkuu.
 
Ni hivi:
Viongozi kipindi cha awamu ya nne walitoa uraia kwa lundo la wakimbizi kutoka Burundi, ambao ndani yake kuna watusi na wahutu

Kwa kuongezea,
Uraia huo uliotolewa kama njugu, inasemekana malengo yake ilikuwa ni kujinufaisha kisiasa, majimbo ya uchaguzi yalianzishwa maeneo waliyopelekwa wakimbizi, na kuna chama kimeongeza idadi ya wabunge wake kupitia hao wakimbizi

Usiku mwema.
CCM inaliangamiza taifa hili!
 
Hili andiko lisisomwe na kukomentiwa kisiasa,iko hivi ktk sheria za kimataifa zinazohusu haki zs wakimbizi mtu aliyekimbia nchini mwake kwa sababu za kivita na kuwa mkimbizi akikaa nchi aliyokimbilia kwa muda wa miaka 10 anatakiwa kuchagua mawili 1: kurudi nchini alikotoka,ama 2:kama alikotoka hakuna amani au kuna amani aombe kwa hiari uraia wa nchi alikokimbilia .So nchi xote zilizosaini mkataba huu zinawajibu wa kutekeleza,so kwetu tz wakimbizi wa Burundi katika kambi za Mishamo(Rukwa),Ulyankulu(Tabora) na Katumba( mpanda) walifika nchini 1972 wakati wa vita kubwa nchini burundu kwa sasa wana takribani miaka 48 s walicheleweshwa aidha kurudishwa kwao au kuasiliwa uraia

upande wa rais wetu jpm hahusiki yeye amekuts hata kadi za uraia tyr zimeandaaliwa na walipewa kabla hata ya kampeni2015 na mchakato wa kuwapa uraia huo yaani wao kuanza kujiandikisha ulianza 2006 wakati wa jk na ilikuwa kwa sheria ya UNHCR shirika la kuhudumia wakimbizi duniani,so Jpm hahusiki na hawezi kuzuia chochote.wahutu na watuts
 
Wakimbizi wengi wa burundi walioko bundyankulu Tabora, mishamo, n. K, kiimani wengi ni Waprotestanti, kupewa uraia mapema kabla ya uchaguzi kulikuwa na malengo ya kisiasa, ukizingatia uchaguzi wa mwaka2015 uliathiriwa na udini sana, watu wengi hawajui kama ukawa ililenga kuunganisha nguvu za Waislamu na Waprotestanti dhidi ya Wakatoliki kwa kuweka Cuf na Cdm pamoja, hivyo wakimbizi hawa kupewa uraia ili wapige kura kulikuwa kunasaidia upande wa upinzani kwa sababu ya imani yao, na ndo chanzo cha kuanzishwa kwa jumuiya ndogondogo za kiprotestanti ili kupeana mikakati, ni fikra zangu tu msiniombe ushahidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni hivi:
Viongozi kipindi cha awamu ya nne walitoa uraia kwa lundo la wakimbizi kutoka Burundi, ambao ndani yake kuna watusi na wahutu

Kwa kuongezea,
Uraia huo uliotolewa kama njugu, inasemekana malengo yake ilikuwa ni kujinufaisha kisiasa, majimbo ya uchaguzi yalianzishwa maeneo waliyopelekwa wakimbizi, na kuna chama kimeongeza idadi ya wabunge wake kupitia hao wakimbizi

Usiku mwema.
Acheni mitizamo hyo yenye mlengo wa ubaguzi navojua hao waliopewa uraia hawakua makambini kama unavyosema na wamezaliwa Tz toka miaka ya 1972
 
Back
Top Bottom