Kwako Juma Aweso na Wizara yako ya Maji

Abeid L Msanganzila

Senior Member
Dec 30, 2018
121
209
Habari za mchana huu wadau wote wa jf?
Poleni na mihangaiko ya kutafta pesa. Mtaani kugumu kweli, kila kitu bei juuu😆

Niende kwenye point!
Wilaya ya Nkasi ni moja ya wilaya za mkoa wa Rukwa. Hii wilaya ina uhaba mkubwa sana wa maji. Mito ni mingi ila asilimia 90 ni mito ya msimu mmoja, yaani msimu wa mvua nyingi! Sasa serikali kupitia wizara yake ya maji ilishaanzisha mradi wa maji ambao huu mradi ulishakamilika ila cha ajabu maji hayatoki.

Kwanini maji hayatoki? Ipo hivi kuna watu walivyoona changamoto ya maji wilayani Nkasi hususani tarafa ya Namanyere waliigeuza fursa kwa kuchimba visima virefu ili kuuza maji kwa wananchi!

Sasa baada ya mradi wa maji kukamilika hawa watu nasikia wanatembeza cheji Halimashauri ili maji ya mradi toka mto mfili yasitoke na ndivyo inavyofanyika hadi sasa! Maji yananunuliwa shilingi 500 kwa ndoo moja ya lita 20!
Watu wanahangaika na maji sanaaa hadi maji yanayonywewa si salama kabisa kwa afya za watu!

Juzi kati walivyosikia kuna ziara ya makamu wa raisi wakayafungulia maji yakaanza kutoka na watu wengi wameyavuta majumbani mwao. Sasa ziara ilivyoyeyuka tayari wamerudi mtindo wao wa zamani wamefunga maji hakuna kutoka.

Wizara ya maji sijui huwa haina utaratibu wa kutembelea miradi yao ili kujiridhisha kama ripoti wanazopokea ofsini ni sahihi ama si sahihi! Wwnachi tunateseka na ugumu wa maisha tunateseka tena na uhaba wa maji/ bei juu za maji. Yani imefika hatua watu tumeanza kupanga ratiba ya kuoga mara mbili kwa wiki.

Najua humu kuna watu walio ndani ya hii wizara, plz tusaidieni wananchi wenu zidi ya wenye nazo jamani! Kisa mtu ana hela basi anataka tununue maji kwake kwa bei juu na tuachane na maji ya mradi wa wizara kwa bei chini.

Nchi ngumu hiii! Aweso amka kijana watu wanalia hukuuuu!
 
Habari za mchana huu wadau wote wa jf?
Poleni na mihangaiko ya kutafta pesa. Mtaani kugumu kweli, kila kitu bei juuu

Niende kwenye point!
Wilaya ya Nkasi ni moja ya wilaya za mkoa wa Rukwa. Hii wilaya ina uhaba mkubwa sana wa maji. Mito ni mingi ila asilimia 90 ni mito ya msimu mmoja, yaani msimu wa mvua nyingi! Sasa serikali kupitia wizara yake ya maji ilishaanzisha mradi wa maji ambao huu mradi ulishakamilika ila cha ajabu maji hayatoki.

Kwanini maji hayatoki? Ipo hivi kuna watu walivyoona changamoto ya maji wilayani Nkasi hususani tarafa ya Namanyere waliigeuza fursa kwa kuchimba visima virefu ili kuuza maji kwa wananchi! Sasa baada ya mradi wa maji kukamilika hawa watu nasikia wanatembeza cheji Halimashauri ili maji ya mradi toka mto mfili yasitoke na ndivyo inavyofanyika hadi sasa! Maji yananunuliwa shilingi 500 kwa ndoo moja ya lita 20!
Watu wanahangaika na maji sanaaa hadi maji yanayonywewa si salama kabisa kwa afya za watu!

Juzi kati walivyosikia kuna ziara ya makamu wa raisi wakayafungulia maji yakaanza kutoka na watu wengi wameyavuta majumbani mwao. Sasa ziara ilivyoyeyuka tayari wamerudi mtindo wao wa zamani wamefunga maji hakuna kutoka. Wizara ya maji sijui huwa haina utaratibu wa kutembelea miradi yao ili kujiridhisha kama ripoti wanazopokea ofsini ni sahihi ama si sahihi! Wwnachi tunateseka na ugumu wa maisha tunateseka tena na uhaba wa maji/ bei juu za maji. Yani imefika hatua watu tumeanza kupanga ratiba ya kuoga mara mbili kwa wiki.

Najua humu kuna watu walio ndani ya hii wizara, plz tusaidieni wananchi wenu zidi ya wenye nazo jamani! Kisa mtu ana hela basi anataka tununue maji kwake kwa bei juu na tuachane na maji ya mradi wa wizara kwa bei chini.
Nchi ngumu hiii! Aweso amka kijana watu wanalia hukuuuu!
Yuko active zaidi kwenye instagram page yake ... Nadhani ukimtumia huu ujumbe ataufanyia kazi.


BT. mmejaribu kuwaona idara ya maji hapo halimashauri kwenu wao majibu yao yakoje kuhusu issue hii uliyoileta huku JF.
 
Yuko active zaidi kwenye instagram page yake ... Nadhani ukimtumia huu ujumbe ataufanyia kazi.


BT. mmejaribu kuwaona idara ya maji hapo halimashauri kwenu wao majibu yao yakoje kuhusu issue hii uliyoileta huku JF.
Wanasingizia umeme eti😄😄 sijui vinaconnection wap hivi vitu ila umeme hausumbui kivile maana mpaka sasa ni siku tano haujakata ata dak tano! Nadhani ni danadana tu! Kuhusu insta nimemtumia ujumbe pia na wizara yake pia nimeitumia huu ujumbe!
 
Hapa kibaha jimbo la Koka jirani kabisa na chuo cha Mwalimu Nyerere,

Tokea siku ya sensa maji hakuna.

Jirani tu hapo Bungo kwa Mheshimiwa Diwani maji yapo.

Ukitaka bodaboda akuchotee dumu moja la lita 20 ni shilingi 600.

Umeme una nafuu haukatiki mara kwa mara.

Wakati mwingine nam miss Mwendazake
 
Hapa kibaha jimbo la Koka jirani kabisa na chuo cha Mwalimu Nyerere,

Tokea siku ya sensa maji hakuna.

Jirani tu hapo Bungo kwa Mheshimiwa Diwani maji yapo.

Ukitaka bodaboda akuchotee dumu moja la lita 20 ni shilingi 600.

Umeme una nafuu haukatiki mara kwa mara.

Wakati mwingine nam miss Mwendazake
Sisi tusio na wasemeaji tunapata tabu aisee, sasa huko kwenu ukute mlichagua upinzani kwahiyo wanawafundisha maisha yanavyokuwa! Nchi ngumu hii ila tunatoboa tu
 
Back
Top Bottom