VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Ni mwanangu tena. Ni yule yule wa Chuo Kikuu. Bado ananitambia bila hata kuniambia hadi natamani kumkimbia. Maneno hayo: kwaherini CCM,karibuni UKAWA ameyaandika na kuyatandika karibu kila kona ya nyumba yangu. Ameyaandika kwa kila aina ya mbwembwe bila kutumia wembe. Hata kwenye 'signecha' ya kwenye ujumbe wake mfupi wa maneno ameyaandika. Najua ananichokoza.
Nilishafanya naye midahalo mitatu nyumbani na akanitoa kapa. Yeye anaponda,mimi napenda. Yeye anaikandia CCM na kuidandia UKAWA. Mimi naitetea CCM na kuipuuzia UKAWA. Mchuano mkali nyumbani kwangu. Tena, anatamba kuwa hana haja ya kusafirishwa kwenye basi wala lori kwenda kupiga kura. Anapigia mita chache tu kutoka nyumbani. Ni mtukutu sana.
Amevuka mipaka kiuhakika. Amewashawishi rafikize waje wafikie nyumbani ili wapige kura zao hapa Dar es Salaam. Na wengine, akishirikiana na wenzake, wamewachangia nauli na kuwaandalia malazi mahali ili waje wapige kura. Anaapa kuhakikisha kuwa anawaleta Dar es Salaam wapiga kura wasiopungua hamsini. Ili mradi tu awaongezee kura UKAWA. Najuta kuwa mwanademokrasia bila ghasia.
Amenidokeza kuwa zaidi ya asilimia 80 wanachuo kikuu watapiga kura zao walipoandikishwa. Anatambia mipango ya viwango iliyopangwa. Ameniahidi kuniambia Jumamosi ya tarehe 24/10/2015. Amepania kwelikweli. Haishi kuimba na kuandika: KWAHERINI CCM, KARIBUNI UKAWA. Bado sijajua anaaga na kukaribisha wapi hasa.
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Nilishafanya naye midahalo mitatu nyumbani na akanitoa kapa. Yeye anaponda,mimi napenda. Yeye anaikandia CCM na kuidandia UKAWA. Mimi naitetea CCM na kuipuuzia UKAWA. Mchuano mkali nyumbani kwangu. Tena, anatamba kuwa hana haja ya kusafirishwa kwenye basi wala lori kwenda kupiga kura. Anapigia mita chache tu kutoka nyumbani. Ni mtukutu sana.
Amevuka mipaka kiuhakika. Amewashawishi rafikize waje wafikie nyumbani ili wapige kura zao hapa Dar es Salaam. Na wengine, akishirikiana na wenzake, wamewachangia nauli na kuwaandalia malazi mahali ili waje wapige kura. Anaapa kuhakikisha kuwa anawaleta Dar es Salaam wapiga kura wasiopungua hamsini. Ili mradi tu awaongezee kura UKAWA. Najuta kuwa mwanademokrasia bila ghasia.
Amenidokeza kuwa zaidi ya asilimia 80 wanachuo kikuu watapiga kura zao walipoandikishwa. Anatambia mipango ya viwango iliyopangwa. Ameniahidi kuniambia Jumamosi ya tarehe 24/10/2015. Amepania kwelikweli. Haishi kuimba na kuandika: KWAHERINI CCM, KARIBUNI UKAWA. Bado sijajua anaaga na kukaribisha wapi hasa.
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam