franksarry
JF-Expert Member
- Nov 9, 2009
- 1,284
- 481
Ndg yangu mtoa mada kuna kanuni za kuchepuka umezikiuka ndio maana unapata matatizo. Kwanza huyo dada sio mchepuko hiyo ni nyumba ndogo yako ambayo unaionea wivu na unataka kuimiliki peke yako kitu ambacho ni kinyume na utaratibu wa uchepukaji maana ukitaka kuwa alone hapo na mdada atataka akumiliki ndio pale unapotelekeza familia au kushtukiwa na mkeo. Ukitaka kuchepuka tafuta mtu mwenye jamaa (ila asiwe ameolewa) ili kama akiwa anahitaji tulizo anamtafuta jamaa yake na wewe unamega kipindi mnapopata nafasi, kumiliki demu peke yako wakati una mke lazima huyo demu atazingua kwa kuwa hutakuwa unamtimizia mahitaji yake ya kimwili haswa usiku wakati huko na mkeo. Natamani nikupe somo refu ila muda ndio hauruhusu
Gharama pia hupungua..

Kuegemea kwenye familia tu siyo vizuri buana!