Nicholaus Kilunga
JF-Expert Member
- Feb 15, 2014
- 1,188
- 570
Leo inatarajiwa kuwa siku ya mwisho wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Davis Mwamunyange kuwatumikia watanzania katika nafasi hiyo ya juu kabisa katika masuala ya ulinzi na usalama.
Jenerali Mwamunyange alikuwa amalize muda wake mwezi Januari mwaka jana lakini rais Mstaafu Jakaya Kikwete aliona ni vyema Jenerali Mwamunyange anayesifiwa kwa kulifanya Jeshi la Wananchi kuwa la kisasa aendelee kuhudumu katika wadhifa huo kwa kipindi kingine cha mwaka mmoja ambao unakoma leo 31.01.2016.
Lakini pia yawezekana rais Magufuli nayeye akaona ni vyema kumuongezea muda wa kuhudumu......
=======
LEO inatarajiwa kuwa siku ya mwisho ya utumishi jeshini kwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Davis Mwamunyange.
Jenerali Mwamunyange ambaye alizaliwa mwaka 1959, alikuwa amalize muda wake Januari 30, mwaka jana, lakini Rais Dk. John Mgufuli alimwongezea mwaka mmoja wa utumishi jeshini.
Mwamunyange ambaye ni Mkuu wa Majeshi wa saba tangu jeshi hilo lianzishwe mwaka 1964, ametumikia nafasi hiyo kwa miaka tisa na mienzi minne sasa.
Wengine ni majenerali wastaafu, Mrisho Sarakikya (1964-1974), Abdallah Twalipo (1974-1980), David Musuguri (1980-1988), Ernest Kiaro (1988-1994), Robert Mboma (1994-2002), George Waitara (2002- 2007).
Januari 30 mwaka jana, akizungumza na waandishi wa habari makao makuu ya JWTZ (Ngome) Upanga, Dar es Salaam, Jenerali Mwamunyange alisema. “Mimi mwenyewe ilikuwa nistaafu kazi leo tarehe 30 Januari 2016, lakini Rais na Amiri Jeshi Mkuu ameamua kunibakiza katika utumishi jeshini kwa mwaka mmoja kuazia leo tarehe 30 Januari, 2016 hadi tarehe 31 Januari 2017,” alisema.
Jenerali Mwamunyage alisema sababu iliyomfanya Rais Dk. Magufuli kumwongezea muda huo, imetokana na kutopata mtu sahihi wa kujaza nafasi hiyo.
Pia Oktoba 30, mwaka jana akiwa kwenye kilele cha sherehe za miaka 52 ya kuanzishwa kwa JWTZ zilizofanyika Bagamoyo mkoani Pwani, Rais Dk. Magufuli alimwahidi Mwamunyange kumpa kazi nyingine baada ya kustaafu kwake.
"Watu wameanza kusema nataka 'kuimilitarize' Serikali (kuendesha serikali kijeshi), lakini ukweli ni kwamba wanajeshi wana sifa nzuri ya maadili na uchapa kazi na hata wewe Mkuu wa Majeshi (Mwamunyange), ukistaafu nafasi zipo za kufanya kazi," alisema Rais Magufuli.
Chanzo: Mtanzania
Kwa jinsi alivyoliunganisha jeshi letu vema na wanajeshi wakawa wamoja zaidi,akaimalisha mafunzo mbalimbali,nidhamu,maslahi ya wanajeshi,mavazi kutoka sare pana pana hadi hizi za kisasa,jinsi alivyomnyamazisha Kagame na chochoko zake kule Congo kupitia kupigwa vibaya kwa M23 na kumnyong'onyesha kwa yale mavifaa ya kisasa siku zile pale uwanja wa uhuru,me namwombea kwa Mungu ampe maisha marefu lakini mh rais JPM akiona inafaa amteue kuwa mkuu wa idala nyeti ya usalama wa taifa ili kulilinda zaidi taifa,kuifanya idala iwe makini zaidi na itilie mkazo mambo ya msingi na yanayowza isaidia nchi zaidi kama vile kufanya ujasusi nyeti wa kiuchumi,kiteknorojia,kifedha na hata ikibidi ujasusi wa kwenye maeneo nyeti kimataifa,na kuwafanya waache kutufatilia sie wachngiaji wa Jf,kuubana upinzani na kuisaidia CCM badala ya nchi,
akienda pale ataunganisha idala mbili muhimu jeshi na idala ya usalama na kwa kuwa anakubalika pote nchi itakuwa imara zaidi na wananchi tutakuwa salama zaidi ya sasa,na uzoefu wake ni muhimu zaidi wakati huu tukikabiliwa na ubabe na vitisho vya bilionea Trump akiwa white house maana kwa kauli zake ataamsha mengi ni vema kama nchi tujipange
ni maoni yangu ya kizalendo tu.plz mabosi wa idala msiagize kucha zangu ziondolewe bado nazipenda