KakaJambazi
JF-Expert Member
- Jun 5, 2009
- 18,716
- 12,075
Nina digital stabilizer ya tropical Power, wakati mwingine inaonyesha "Input ni 218V,,Output = 231V"
Inawezekanaje hii?
Inawezekanaje hii?
unaitumia kwenye nini?
Mimi sioni kama kuna tatizo lolote. Yawezekana output yake ni 230V na haiwezi kuwa accurately. Hivi ikiwa 229V au 231V bado inakaribiana kabisa. Usihofu. Wakati mwingine inategemeana na vifaa vilivyounganishwa katika stabilizer hiyo.
Voltage Stabilizer, Tafsiri rahisi:
voltage, ni kiwango cha umeme
stabilizer, inatokana na neno stable, kinachosababisha kuwa stable
stable ni sifa ya kutulia, kutobadilikabadilika.
Voltage Stabilizer upande mmoja inapokea umeme wa kiwango kinachowezakubadilika toka kwenye line,
upande wa pili inatoa umeme wa kiwango fulani kwenda kwenye matumizi.
Hivyo,
Voltage Stabilizer ni chombo kilichokusudiwa kutoa kwa ajili ya matumizi, umeme wa kiwango kisichobadilika 'stable' hata kama kiwango cha umeme toka kwenye line kitakuwa kinapanda na kushuka ovyo ovyo.
Kitu cha kujali ni kuwa Voltage Stabilizer itoe umeme wa kiwango kinachohitajiwa na chombo unachotumia (mfano 230V). Iwapo line voltage itapanda zaidi ya kiwango hiki, stabilizer itashusha itoke 230V, na ikishuka (mfano 200V), stabilizer itafidia itoke 230V.
Ndani ya Stabilizer kuna auto transformer (steps up or down) kufanikisha hilo.
Iwapo hiyo uliyonayo ni Digital maana yake ni kwamba digital circuit ndiyo inaiongoza transformer wakti gani wa kupandisha na kwa kiasi gani na wakati gani wa kushusha na kwa kiasi gani.
Hata hivyo,
TV za siku hizi zimetengezewa Auto voltage circuit (check name plate nyuma ya TV yako karibu na mahali pa kuchomeka waya wa umeme).
Iwapo utakuta maandishi mfano wa haya, 190~260V AC, ina maana kuwa umeme wa Tanesco ukishuka hadi 190V, TV yako itaendelea kufanya kazi na ukipanda hadi 260V bado hakutakuwa na tatizo.
Kwa hiyo kimsingi chombo chako hakihitaji stabilizer bali kinahitaji Surge Protector, chombo cha kujihami dhidi ya umeme unaosababisha madhara. Bei yake ni ndogo kuliko ile ya stabilizer, jipatie Protector na hifadhi Stabilizer kwa matumizi yenye huo uhitaji.
Asante kwa kuhitaji kueleweshwa, nakaribisha maswali mengine kuhusu vyombo vinavyotumia umeme.
mkuu mimi ninahitaji kujua mchanganyiko uliyotumika kuiwezesha tube light kuwaka. Maana hizi taa huwa zina element mbili.yaani mwanzo na mwisho.ila katika utendaji wake taa huonekana yote imewaka.pia hizi taa kunawakati huwa zinagoma kuwaka zinakuwa zina blink tu.ila ukipima kipimo kinakuonyesha kuwa ni nzima.
Hicho kifaa chako sio stabilizer ila ni regulator, stabilizer huwa inafanya output kuwa stable, ila regulator yenyewe ina uwezo wa kuongeza umeme ukiwa mdogo na kupunguza umeme ukiwa mkubwa!!
ya kichina hiyo mkuu be careful
ya kichina hiyo mkuu be careful
Hicho kifaa chako sio stabilizer ila ni regulator, stabilizer huwa inafanya output kuwa stable, ila regulator yenyewe ina uwezo wa kuongeza umeme ukiwa mdogo na kupunguza umeme ukiwa mkubwa!!
hongera kwa maelezo mazuri,ila mimi nina maswali 2Voltage Stabilizer, Tafsiri rahisi:
voltage, ni kiwango cha umeme
stabilizer, inatokana na neno stable, kinachosababisha kuwa stable
stable ni sifa ya kutulia, kutobadilikabadilika.
Voltage Stabilizer upande mmoja inapokea umeme wa kiwango kinachowezakubadilika toka kwenye line,
upande wa pili inatoa umeme wa kiwango fulani kwenda kwenye matumizi.
Hivyo,
Voltage Stabilizer ni chombo kilichokusudiwa kutoa kwa ajili ya matumizi, umeme wa kiwango kisichobadilika 'stable' hata kama kiwango cha umeme toka kwenye line kitakuwa kinapanda na kushuka ovyo ovyo.
Kitu cha kujali ni kuwa Voltage Stabilizer itoe umeme wa kiwango kinachohitajiwa na chombo unachotumia (mfano 230V). Iwapo line voltage itapanda zaidi ya kiwango hiki, stabilizer itashusha itoke 230V, na ikishuka (mfano 200V), stabilizer itafidia itoke 230V.
Ndani ya Stabilizer kuna auto transformer (steps up or down) kufanikisha hilo.
Iwapo hiyo uliyonayo ni Digital maana yake ni kwamba digital circuit ndiyo inaiongoza transformer wakti gani wa kupandisha na kwa kiasi gani na wakati gani wa kushusha na kwa kiasi gani.
Hata hivyo,
TV za siku hizi zimetengezewa Auto voltage circuit (check name plate nyuma ya TV yako karibu na mahali pa kuchomeka waya wa umeme).
Iwapo utakuta maandishi mfano wa haya, 190~260V AC, ina maana kuwa umeme wa Tanesco ukishuka hadi 190V, TV yako itaendelea kufanya kazi na ukipanda hadi 260V bado hakutakuwa na tatizo.
Kwa hiyo kimsingi chombo chako hakihitaji stabilizer bali kinahitaji Surge Protector, chombo cha kujihami dhidi ya umeme unaosababisha madhara. Bei yake ni ndogo kuliko ile ya stabilizer, jipatie Protector na hifadhi Stabilizer kwa matumizi yenye huo uhitaji.
Asante kwa kuhitaji kueleweshwa, nakaribisha maswali mengine kuhusu vyombo vinavyotumia umeme.
hongera kwa maelezo mazuri,ila mimi nina maswali 2
1.nijuavyo mimi kazi ya saketi breka,ile inayokaa karibu na main switch ndani ya nyumba ni kuzuia shoti ya umeme mkondo geu au altenating current ,sasa kwa nini vitu mfano Tv,redio ndani vinaungua bila circuit breaker kujua/kudetect ?
2.kuna jambo moja huwa nalifahamu kinadharia tu ila practically niliwahi kujaribu lakini niliishia njiani ni hivi "krichoff" alisema katika saketi yeyote nyaya za umeme mbili au zaidi zinapokutana katika pointi moja(node).basi pointi hiyo inakuwa neutral,yaani haina umeme!!
"in any closed circuit/loop/mesh the summation of currents let say i1 +i2+i3=0" and "the summation of potential difference at that particular point v1+v2+v3 also is equal to zero,jambo ambalo kinadharia nalikubali kabisa..Sasa swali langu ni kwamba je unaweza kushika kwa mikono mitupu sehemu kama junction box bila madhara?,binafsi nshawahi kuunganisha live na neutral ktk switch halafu nikataka niguse junction yake lakini nilisita kidogo baada ya kuona cheche kwa mbaali..kwa hiyo bado nina contradiction kati ya nilichokisoma na nilichokiona..kama una ufahamu na mambo haya nifafanulie