Kwa wasiomjua Magufuli, Je, anafaa kuwa Rais?

Status
Not open for further replies.
Mh. Membe naye atapata muda wa kupumua....Tuna poteza muda mwingi kwenye siasa za maji taka.
 
muulizieni kipindi kile alipokuwa ujenzi kabla hajarudishwa hivi juzi alifanya madudu gani?
hamna mtu hapo,tupa kule
 
I like him. He is good no matter what you say. Ni bora huyu hata kazi zake zinaonekana kuliko wengine. Tena heshima ni kitu cha bure tu hebu mu address vizuri. Ni Dr (wa ukweli) Magufuli tafadhali.
 
NI kweli haya ni madai mazito lakini hauwezi kuyaamini na kuyafanya ndo hali halisi ya bwana Pombe eti kwa kuwa mtu mmoja kajisikia leo kuyatoa. Miaka zaidi ya 10 imepita toka alipotenda baadhi ya haya, ulikuwa wapi kuyasema?

Hata kama madai yako ni ya kweli, umejiangusha wewe mwenyewe maana hukuyatoa mapema. Matokeo yake madai yako yanazidiwa nguvu na utendaji wake na hivyo watu kumwona yeye anafaa zaidi kuliko madai yako.
Una hakika kuwa haya hayakuzungumzwa? au aliyezungumza wakati huo hukumpenda? au chombo alichotumia kutoa habari hukukiamini? haya yapo tena mengi, na hao munaowaona watukufu hizi ndio kazi zao.
 
Kwa ile hoja ya burigi hivi hata kama kweli alifanya hivyo magufuli, ni kosa kubwa la kukosa urais? hata hamna haja ya kuchunguza amefanya makubwa sana, na vyote alivyosema burigi si kwamba kachukua pesa kajiwekea kwenye account yake kwa manufaa yake na familia yake bali ni kwa wapiga kura wake. na sio kama hawa wengine mafisadi wamechukua pesa nyingi kwa ajili yao binafsi. kwa mimi naona hakuna cha kufatilia hapa. ni watu wachache wanataka kumuharibia magufuli.
 
Kitila Mkumbo yuko sahihi kwenye hili. Waziri ni mbunge na si mwanafunzi wa shule ya msingi anayemuogopa kiranja wake. Kama mbunge, dhamana yake kubwa ni kwa wale waliomchagua na si kwa huyo aliyempa cheo cha uwaziri. Waziri makini anapaswa kutetea kile tu ambacho anamini kwa dhati kuwa ni kwa manufaa ya waliomtuma na si kwa sababu aliyemteua anadhani hivyo. Anapoona mambo hayo mawili yanagongana, waziri makini anapaswa kuachia kofia ya uwaziri na kubakiza ile muhimu zaidi ya ubunge. Mwaka 2003 Robin Cook, kiongozi wa chama cha leba bungeni, mwenye wadhfa ya uwaziri, alijiuzuru nafasi hiyo baada ya kutokubaliana na uamuzi wa serikali ya Tony Blair kuvamia Iraq. Waziri mwingine, Clare Short nae ingawa awali aliunga mkono uamuzi wa Blair lakini baada ya kutafakari nae akaamua kuachia ngazi. Ndivyo inavyotakiwa. Kwa upande mwengine, Colin Powell mpaka kesho kutwa atalaaniwa kwa kutoa ushahidi wa uongo Umoja wa Mataifa juu ya WMD za Iraq. Hawezi hata siku moja kujitetea kuwa alifanya hivyo kwa vile aliagizwa na rais wake. Alichosema ni kuwa alidanganywa.

Maadili ya kazi hayana maana utekeleze maamuzi au maelekezo ambayo sio Just. Wakina Himmler, Goebbels, Eichmann na wengine kibao waliokuwa wakiendesha concentration camps chini ya serikali halali ya Nazi Germany, hawakuweza kujitetea kuwa walifuata maagizo ya Fuhrer wao! Mtu ukiwa kiongozi wa ngazi yeyote unatakiwa kupima haki ya kila unachoagizwa.

Kwa vile wengi walimuandama Zitto haina maana kuwa alikosea. Yeye alistahili sifa kama kiongozi kusimamia principle zake. Kilichotakiwa kufanywa ni kuonyesha kuwa hizo principle zilikuwa potofu na si kumbeza.

Kwa hali hii, kwenye suala la uuzaji wa nyumba za serikali pamoja na kuwa uamuzi ulikuwa wa kabineti nzima ( si BWM peke yake), waziri aliyepewa dhamana ya kutekeleza maamuzi hayo hawezi kukwepa kuhusishwa na uamuzi huo. Swali lingine linachofuata ni namna utekelazaji huo ulivyofanyika. Je, ulikuwa wa haki na uwazi? Je ulikuwa na mafanikio yeyote kwa maana kuwa serikali ilifaidika vipi? Kama matarajio yetu hayakufikiwa, ni kitu gani kilisababisha hali hiyo? Yote haya ni maswali halali na yanastahili majibu kutoka kwa mtu yeyote aliye makini na mwenye mapenzi na taifa letu. Maswali kama haya yanapaswa kuulizwa kwa yeyote yule ambaye amepewa nafasi ya uongozi katika nchi yetu. Bahati mbaya hatupendi kuuliza maswali magumu maana tunachokitaka ni platitudes!

Amandla.....

Nakubaliana na wewe kwa asilimia kubwa mengi uliyongea yana ukweli mtupu LAKINI ktk system iliyo kamilika.

Kwa jamii ile jinsi ilivyoharibika nafikiri nikumwonea bure Magufuli kuhoji kwamba ugawaji na process ilikuwa just. Kwa Tanzania huwezi simamia kitu chochote kwa u-just, labda usiamamie mwenyewe kila idara, na hata hivyo bado huwezi.

Mimi nafikiri swali ambalo ni genuine la kuulizwa ambalo nakubaliana nalo moja kwa moja kwa hali ya Tanzania, nafikiri ni hili je Magufuli alinufaika je na uuzwaji wa nyumba hizo tulete na vidhibitisho tuache zile hadithi tulizosimuliwa wakati ule kwamba sumaye anamiliki morogoro yote kumbe uzushi mtupu.
 
Kuna haja ya kuzifanyia kazi shutuma za mtoa mada. Baadhi ya shutuma nilishazisikia sana kipindi cha nyuma, tusifanye kosa kudharau hata neno moja la mtoa mada. Badala yake, tuzifanyie uchunguzi wa kina.
 
hili wazo binafsi haliwezi kupostiwa kwenye original post ya burigi lazima uanzishe yako? too many new posts hata za maana sasa hatuzisomi.
 
Nakubaliana na wewe kwa asilimia kubwa mengi uliyongea yana ukweli mtupu LAKINI ktk system iliyo kamilika.

Kwa jamii ile jinsi ilivyoharibika nafikiri nikumwonea bure Magufuli kuhoji kwamba ugawaji na process ilikuwa just. Kwa Tanzania huwezi simamia kitu chochote kwa u-just, labda usiamamie mwenyewe kila idara, na hata hivyo bado huwezi.

Mimi nafikiri swali ambalo ni genuine la kuulizwa ambalo nakubaliana nalo moja kwa moja kwa hali ya Tanzania, nafikiri ni hili je Magufuli alinufaika je na uuzwaji wa nyumba hizo tulete na vidhibitisho tuache zile hadithi tulizosimuliwa wakati ule kwamba sumaye anamiliki morogoro yote kumbe uzushi mtupu.

Mkuu, mbona unanitisha! Inaelekea kwa vile unaamini nchi yetu imeoza basi kila mtu apewe free pass! Kama hatuwezi kumhukumu Mheshimiwa Magufuli kwa sababu nchi imeoza basi kwa nini tunaendelea kuwasakama wakina Vijisenti, Rostam na wengine? Si mmesema nchi imeisha oza, kilichobaki ni kuifukia kaburini sasa kwa nini tuwalaumu kwa kujichukulia chao mapema?

Swali si Mheshimiwa Magufuli alinufaika vipi na uuzwaji wa nyumba bali ni taifa ilinufaika vipi? Ni lazima palikuwa na sababu na malengo katika zoezi zima ambayo yanapimika. Kwa kifupi, kwa nini uamuzi huo ulifanyika? Na serikali ingefaidika vipi kutokana na zoezi hilo? Sasa inabidi baada ya zoezi ( kama ilivyo kwa mradi wowote) inabidi tuliangalie na kulichambua ili tuone kama tulifanikiwa kutimiza malengo yatu, nini tumeweza kujifunza na kama hatukufanikiwa, kwa nini imekuwa hivyo? Inabidi kujiuliza matokeo ya zoezi zima yamekuwa nini? Kuuliza Mheshimiwa Magufuli alifaidika vipi kwangu mimi hakuna uzito unless kama katika post mortem yetu ikaonekana kuna watu walinufaika kinyume cha taratibu, na yeye akiwa mmoja wao.

Ilibidi zoezi kama hili lifanyike kwenye Richmond, Dowans na kadhalika. Cha muhimu zaidi
si kutafuta mchawi bali ni kujifunza kutokana na makosa yetu!

Amandla.....
 
Sio kila mtu anayeuliza maswali ni mpinzani. Ni wajibu wa kila mmoja wetu kuuliza maswali na wale wenye majibu kutoa majibu. Kuna ishu nyingi kwa mtendaji yeyote aliyekuwa katika nyadhfa za juu kama Mheshimiwa Magufuli. Kwa mfano, kuna masuala ya barabara. Je zote tulizoahidiwa zilijengwa? Na kama zilijengwa kwa kiwango gani na gharama gani? Kama hazikujengwa, nini kilisababisha kutokujengwa kwake? Mheshimiwa Magufuli alisimamia vizuri matumizi ya magari ya miradi na ya serikali. Je serikali iliokoa kiasi gani katika zoezi hilo?

Mheshimiwa Magufuli aliwahi kuwa waziri wa ardhi. Je palikuwa na nafuu katika kero ya upatikanaji wa viwanja? Jee uvamizi wa viwanja na maeneo yalio wazi ulipungua na wale waliofanya hivyo kuchukuliwa hatua? Ni sera gani wizara hiyo ilibuni kuwaboreshea wakazi wa nchi yetu makazi yao?

Mheshimiwa Magufuli aliwahi kuwa waziri wa uvuvi n.k. Je katika wakati wake, uvuvi haramu ulipungua? Jee sekta hii ilipanuka ili kuchangia zaidi katika pato la taifa na lishe ya wananchi wake? Na maswali mengine kama hayo.

Vile vile, yeyote ambaye atajitokeza au atapendekezwa kugombea urais wa nchi yetu, inabidi aulizwe maswali kutokana na utumishi wake au utendaji wake katika sekta yeyote ile aliyoshiriki. Kama alikuwa mfanyabiashara basi itabidi tujue kama alikuwa na mafanikio na jinsi alivyopata mafanikio hayo. Kama alikuwa mbunge awali, nae ni lazima tujue mchango wake katika bunge na kwa wale waliomchagua. Kama alikuwa mtumishi wa Mungu, nae vile vile.

Ni lazima tujitahidi ili tuchague mtu tukiwa macho wazi. Wakati wa visingizio umepita.

Amandla......

Haya maswali uliyouliza ni mazuri na kama kweli ulitaka mjadala wa namna hii basi ilikuwa unaya shot mapema tu badala ya kutanguliza hisia kuwa watu wanaosifia utendaji wa Magufuli ni sawa na wale waliokuwa wakimshabikia Kikwete,hoja ambayo nashukuru kuna member hapa amekujibu vizuri sana.
Lazima tukubaki kwamba,hakuna binadamu yeyote aliyekamilika.Magufuli kama binadamu hajakamilika,hivyo ni wazi kuwa hata katika utendaji wake kuna makosa alishayafanya na atayafanya.HAKUNA BINADAMU/KIONGOZI ASIYEFANYA MAKOSA.Kwahiyo Magufuli kufanya makosa isiwe nongwa.Muhimu ni kupima uzito wa hayo makosa na kisha kulinganisha na uzito wa mafanikio yake ya kiutendaji katika Taifa hili.Sasa isiwe ni kutafuta vijimakosa tuu alivyowahi kufanya na kuvishikia bango eti hafai kuwa kiongozi as if labda Tanzania tulishawahi kuongozwa na Malaika au tuna Malaika tunayemtegemea kuja kutuongoza.
Sipingi kujadili mabaya ya Magufuli,lakini mpaka sasa sijaona baya la msingi kusema eti hafai kuwa kiongozi hasa nikimlinganisha na wanasiasa wengi ninaowasikia kuwa wana nia ya kugombea Urais Tanzania.
 
Unfortunately hata mimi nafahamu tabia binafsi ya huyu mheshimiwa Magufuli wakati akiwa mwanafunzi wa UDSM ni kama ilivyoandikwa hapo juu; ila nilidhani ilikuwa ni tabia ya uanafunzi, na baada ya kuwa kiongozi alishaacha tabia hiyo. Nimekuwa nasoma ripoti za ufanisi wake kikazi, na wala sijawahi kuangalia utendaji wake upande wa pili.
 
Hilo la kufanya utafiti zaidi juu ya Magufuli naliunga mkono; katika utafiti huo pamoja na mambo mengine ni vema kuchunguza kiwango cha utajiri alionao kwa kulinganisha na vyanzo vyake halali vya mapato. Kwa mfano, inasemekana karibu asilimia 80 ya majengo yote yaliyoko makao makuu ya wilaya ya Chato ni yake.
 
hili wazo binafsi haliwezi kupostiwa kwenye original post ya burigi lazima uanzishe yako? too many new posts hata za maana sasa hatuzisomi.

Naunga mkono hoja.Mods please ziunganisheni na ile nyingine manake bado iko moto inajadiliwa na huyu mkuu hana hoja yoyote ya kuijadili independently
 
Haya maswali uliyouliza ni mazuri na kama kweli ulitaka mjadala wa namna hii basi ilikuwa unaya shot mapema tu badala ya kutanguliza hisia kuwa watu wanaosifia utendaji wa Magufuli ni sawa na wale waliokuwa wakimshabikia Kikwete,hoja ambayo nashukuru kuna member hapa amekujibu vizuri sana.
Lazima tukubaki kwamba,hakuna binadamu yeyote aliyekamilika.Magufuli kama binadamu hajakamilika,hivyo ni wazi kuwa hata katika utendaji wake kuna makosa alishayafanya na atayafanya.HAKUNA BINADAMU/KIONGOZI ASIYEFANYA MAKOSA.Kwahiyo Magufuli kufanya makosa isiwe nongwa.Muhimu ni kupima uzito wa hayo makosa na kisha kulinganisha na uzito wa mafanikio yake ya kiutendaji katika Taifa hili.Sasa isiwe ni kutafuta vijimakosa tuu alivyowahi kufanya na kuvishikia bango eti hafai kuwa kiongozi as if labda Tanzania tulishawahi kuongozwa na Malaika au tuna Malaika tunayemtegemea kuja kutuongoza.
Sipingi kujadili mabaya ya Magufuli,lakini mpaka sasa sijaona baya la msingi kusema eti hafai kuwa kiongozi hasa nikimlinganisha na wanasiasa wengi ninaowasikia kuwa wana nia ya kugombea Urais Tanzania.

Bado ninasimama pale pale. Hamna tofauti kati tulivyoshabikia viongozi wote waliotangulia.

Hauwezi kujitetea kuwa hakuna binadamu asiye na makosa katika nafasi muhimu kama hii. Kama hakuna binadamu au kiongozi asiyefanya makosa basi mnamuonea Mheshimiwa rais Kikwete, Mkapa na wengine maana nao si binadamu kama huyu mnayemtetea!

Mnachonisikitisha ni kuwa, hamuweki bayana mafanikio yake. Kusema kuwa utendaji wake wote tuliuona haitoshi. Tuambieni ni wapi na wapi alifanikiwa kama hawa wakina Burigi walivyoweka wazi yale waliyoona kuwa ni mapungufu yake. Kwa kufanya hivyo mtatusaidia wote kuweza kupima na kufikia uamuzi utaoridhisha nafsi zetu.

Inawezekana Mheshimiwa Magufuli ana sifa za kuwa rais wa nchi yetu, sijui. Inawezekana vile vile kuwa urais haumfai bali uongozi mwengine ndio unamfaa. Na inawezekana pia kuwa kote huko hafai. Ni nyinyi wenye maelezo ndio mtakaoweza kutusaidia au hata kumsaidia kama ana lengo kweli la kugombea urais maana maswali haya yatakujaulizwa tu, tutake tusitake.

Amandla....
 
Mze kila mtu ana good na bad History hata magufuri ana mema mengi tu amefanyia taifa hili mfano ameweza kusimamia wizara mbalimbali kwa ufanisi mkubwa kulinganisha na wenzake waliopata kupita katika wizara hizo mfano ujenzi wa barabara aliweza kusimamia vizuri zaidi na hiyo ndiyo sifa tunayompamba nayo sana kwa kweli hata mimi ninampongeza lakini hata humo ukiangalia kwa ndani utagundua kuwa kuna vitu vingi alifanya ambavyo kimaadili vinamwangusha kuwa kiongozi bora na ukweli utabaki ndani ya samaki kumi walioza angalau yeye hajafikia hali mbaya anaweza kiliwa hata kwa ndimu

We burigi unaonekana una chuki binafsi na John Pombe Magufuli. TAKUKURU WAPO,KWANINI ULISHINDWA KUMPELEKA TAKUKURU ukamkamatisha pesa za MOTO??? Huu ni umbeya Burigi. Kwa taarifa yako Magufuli HATOI WALA KUPOKEA RUSHWA.Yeye ni mmoja wa wana CCM wachace wenye misimamo na wasioyumba. Ndiyo maana KILA WIZARA ANAYOPEWA ANAIMUDU!

Ukweli ni kwamba kule CCM hakuna MSAFI HATA MMOJA. Viongozi wote wa CHAMA CHA MAFISADI wameoza,they are corrupt to the core.Viongozi WASAFI KWA SASA WAKO CHADEMA TU. VYAMA VINGINE VOTE NI UOZA MTUPU.

Hata hivo Magufuli is MUCH BETTER THAN THE REST OF THEM.
Kama akigombea URAIS NA KIWETE ni afadhali umpe MAGUFULI KULIKO MKWERE KIWETE. Tunajua hakuna mwanadamu aliye perfect 100%. Kwanza Magufuli ni Dk. wa ukweli na akili yake jamaa imetulia, Mkwere Kiwete hawezi kumfikia Magufuli kwa KUCHAPA KAZI na hata wakikaa darasani nakuhakikishia Mkwere haoni ndani.

Burigi ulicholeta hapa ni umbeya na chuki binafsi. Yawezekana aidha wewe au ndugu yako ndiyo mliopewa mshiko ili kumwachia Magufuli kiti cha Ubunge. Hata mngeligombea msingemshinda jamaa bado Wazinza,Wsukuma na Wahaya wanamkubali . Magufuli katika CCM bado yuko juu. NILITAMANI KIWETE AMWEKE KWENYE WIZARA YA NISHATI NA MADINI HALAFU WATZ tungelishuhudia MGAWO ukiwa ni historia.
 
Ni muhimu kupata taarifa kama hizi kwa watu wanaofikiriwa kuwa viongozi wetu, na si vizuri kuwakatisha tamaa wanaotoa taarifa hizi na kuwapa watu fulani utakatifu wakati pengine hawana.

Nakumbuka mwaka 2005 watu walivyokuwa wamepagawa kwenye forum ya uchaguzi.com (kama JF ya leo), ulikuwa huwezi kusema neno lolote watu wakaelewa na ulikuwa unaitwa majina yote ya usaliti hapa duniani ukimkosoa mgombea wao kipenzi. Niliandika makala kuhusu sababu 15 kwa nini CCM wamteue SAL-ngumi, mateke na matusi niliyopata kutoka kwa wana uchaguzi.com siwezi kusahau, na leo ndiyo hao wanaoongoza kumpiga mawe aliyekuwa mgombea wao kipenzi.

Sasa tusirudie kosa tulilofanya mwaka 2005 kwa kuendekeza ushabiki wa kijinga na kudharau watu wanaotupatia taarifa za upande wa pili wa wale wanaotaka kuwa viongozi wetu. Huu sio muda wa ushabiki na ubazaza usio na mantiki.

Lazima kila kiongozi tumpime vya kutosha na lazima tugeuze kila jiwe.

DR. Mkumbo Nakuunga mkono sijui kwa nini watu wameamua kumshambulia mtoa mada ghafla bila hata kufikiri sana. Hebu tuyafanyie kazi yaliyoandikwa kuhusu huyu Waziri na nafikiri tujipe mda wa kutosha ili kudhibitisha hizi tuhuma nzito. Kama ni siasa za maji taka au maji safi tutajua. Kama unamkubali Magufuli kwa unayaoyaona kwa nini usimtilie shaka unapopewa information za private life yake
Lazima apite katika chekecheo na watanzania tujiridhishe ili leo na kesho tusianze kujutia maamuzi tutakayofanya kama ukweli utakuja dhihirika baadaye.
Nani asiyejua wale wanaopenda waonekane mbele za watu kuwa wana fanya vizuri wengi ni hugeuka kuwa wasaliti wakubwa wa waliowapa fursa ya kuwaongoza. Hivyo lazima tuwe makini
 
Wandugu,
Binafsi nimegundua kuwa Burigi ni jasiri sana. Alichokifanya nimekuwa nakisikia sehemu kadhaa na mara zote "reaction" ya watu imekuwa karibu sawa na ya humu ukumbini.

LAKINI NAOMBA JAMBO MOJA,

Kwa nini tusiache "prejudice" halafu tukachunguza na kupima alichokileta hapa ukumbini halafu tukajua ukweli? Kuna wengi tu humu ama tunawafahamu watu waliofanya ama wanafanya kazi zinazowafanya wamfahamu Mh. Magufuli, kwa nini tusifanye utafiti halafu tukauleta hapa (kwa manufaa ya taifa letu)? Maana kama Mh. Magufuli anafaa basi asije kupigwa majungu tukakosa kiongozi mzuri, lakini pia tusije tukapata kiongozi bomu ikija kubainika kuwa tuliyoambiwa ni ya kweli.

Naomba kutoa hoja.

mimi sijapenda wazo lako binafsi kwani tunamjadili magufuli kama nani saizi kwenye swala zima la kuwa raisi na unavyosema tusije kupata kiongozi mbovu una maanisha nini? Umesikia ndiye raisi wetu 2015
 
Kwa ile hoja ya burigi hivi hata kama kweli alifanya hivyo magufuli, ni kosa kubwa la kukosa urais? hata hamna haja ya kuchunguza amefanya makubwa sana, na vyote alivyosema burigi si kwamba kachukua pesa kajiwekea kwenye account yake kwa manufaa yake na familia yake bali ni kwa wapiga kura wake. na sio kama hawa wengine mafisadi wamechukua pesa nyingi kwa ajili yao binafsi. kwa mimi naona hakuna cha kufatilia hapa. ni watu wachache wanataka kumuharibia magufuli.

Binafsi sina imani na kiongozi yeyote akitokea CCM, hata kama angekuwa mzuri kiasi gani akishakuwa chini ya CCM hafai tena, anatekwa na nguvu ya mafisadi. Tusijadili tena viongozi kutoka CCm. Tutumie muda mwingi kutafuta viongozi mbadala kutoka vyama vingine.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom