Kwa wanaume wa bongo: Kuwa na wanawake wengi sio sifa kwenye maisha!!

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,609
8,753
Nimeshangazwa sana na fikra za kizamani ambazo nimeziona Tanzania kwa wanaume. Mimi kama mwanaume ambaye sikuwa Tanzania kwa muda mrefu nimesikitishwa sana na tabia ya kihuni ya wanaume hasa walio na wake.

Tanzania kuna magojwa na kila familia ina ndugu ambaye amepatwa na ukimwi lakini nimeshangazwa na tabia ya wanaume kuwa na wanawake wa pembeni wakati wana wake nyumbani. Cha kushangaza wanaume hata marafiki zangu wamekuwa wakishinda kwenye klabu za baa baada ya kazi na wanawake wa pembeni huku wake zao wakiwa pekee na watoto nyumbani. Swali je kwanini umeoa kama hauko tayari kutulia?, Je mke wako ukimpelekea magojwa kama ya ukimwi ni nani ataangalia watoto wako kama wote ni wagojwa? Je hizo pesa ungeziweka na kuzitumia na mke wako kwenda kupumzika sehemu huoni kwamba ni muhimu zaidi?. Kitu ambacho ni cha ajabu zaidi ni kwa wanaume wengi kuona kama kitu hiki ni cha sifa na ukipata pesa kidogo ni lazima uonyeshe watu kwamba una uwezo wa kuwa na wanawake wengi!!.

Tofauti wa wanaume wengi tulio ugaibuni tatizo letu ni kupata wanawake wazuri kwani tunajua umuhimu wa wake wazuri kwenye maisha. vilevile tumekuwa tunajitegemea wengi kuanzia miaka 21-23 hivyo tumekuwa mapema sana. Wengi vilevile tumeona wanawake wa kila aina hivyo mambo ya wanawake si mageni hata kidogo. Lakini tukiamua kuoa tunatulia kwani tunajua kwanza sio sifa kwa jamii kuwa na wanawake wengi lakini vilevile tumekuja huku kutafuta na si kujionyesha au kufanya uhuni. Hivyo kwa mawazo yangu Wanaume wa nje ni bora sana kwenye ndoa kuliko wanaume wengi wanaoishi Tanzania ambao wengi ni wahuni wa kutupwa.

Ushauri ni wanaume wenzangu acheni ushamba na uhuni sio sifa kuna familia nyingi sana sasa wana wajane kwasababu ya magojwa, watoto wanahitaji pesa ya bar kwa elimu, nchi yetu inahitaji tujihusishe na shughuli za maendeleo ya nchi yetu masikini. Kikubwa zaidi ni kwamba itakuwa vizuri ukitumia muda wa jioni kufanya mazoezi kwani Tanzania hata huduma ya afya ni ya kiwango cha chini sana.

Mimi siandikagi kwenye mapenzi lakini nimeona hili badilikeni ni mawazo tu.
 
Sifa ya wanaume kuwa na wanawake wengi ni sawa na sifa ya mwanaume kunywa chupa nyingi za beer bar lazima asimulie na wenzake wamsifu. So pathetic!
 
Kuna mtu aliandika kwa michuzi 'eti' ndio maana jamaa wa ughaibuni'aka wabeba box' wakitua bongo wanakaribishwa na kusuruhisha migogoro ya mapenzi ya jamaa zao 'washinda bar'......matokeo yake mbeba box anajipigia maana anajua sana ku care!
 
Hahahahahahahahahha
Kaunga umenichekesha! Ukitembelea status za wasichana wengi utaona wameandika hivi either its complicated or in relation ship!



It's complicated! Source Mdogo wangu!
 
Last edited by a moderator:
Haya wameshakusikia wadada wa bongo subiri pm.

Kazi kuharibiana tu

Hahahahahh
Ila seriously wakaka wa kibongo kiapo cha ndoa mnakichukulia lightly sana; yaani kama routine tu, sidhani kama huwa mnakaa chini na kutafakari kabla ya ndoa.
 
Nasikia nyumba ndogo suna,, sema mkeo asijue hata iweje..

Ni laana na mikosi. Kile kiapo ni kitakatifu, ni mara mia usiape uchukue mwanamke umzalishe n then uwe na nyumba ndogo zako 7 kuliko kuenda kinyume na kiapo kitakatifu.

Wanasema kila unayeingia naye kimwili basi ni convenant umefanya hivyo unabeba baraka, laana na mikosi yake! So waweza kuwa mwili mmoja na wanawake 8 si ushereani huo.
 
Nashukuru kwa wachangiaji hakuna mtu perfect duniani! lakini tuwape sifa zaidi wale wanaojitahidi kuwa perfect kwenye maisha kiuchumi, kifamilia, kisiasa, uzalendo. Huwezi kuwa na uzalendo nyumbani kama huna uzalendo kwenye familia. Kuna tofauti kubwa kama umezidiwa na kutoka na mtu lakini kama hiyo ni tabia na sifa kwa jamii si vizuri. Wake wengi wakipewa nafasi ni wazuri hata kimapenzi kuliko hao wanawake wa nje. Nachoomba kikubwa tusisifie na kufanya eti ndiyo wanaume tulivyo kwani sikweli maisha ni uvumilivu.
 
Back
Top Bottom