Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Kuna wanawake kama walivyo wanaume ambao wana matatizo ya kisaikolojia ya kingono. Matatizo haya ni pamoja na pale ambapo mtu hawezi kujizuia kufanya ngono na mtu mmoja au hatosheki hata akifanya ngono saa kadhaa kwa kutwa nzima, endapo mtu ni huyo huyo.
Anatamani tu kubadili nwanaume atakavyo kufanya ngono na wanaume tofauti ndio ndio anajisikia kuridhika na tendo, na sio kwa sababu ya fedha au kunufaika na jambo lingine, la hasha, kinachotafutwa ni kuridhishwa kingono.
Hivyo ni rahisi zaidi kwa mwanamke mwenye silka hiyo kugawa mwili wake kwa mwanaume yeyote atakayemfuata. Kuna wakati malezi huweza kumfanya mwanamke kushindwa kuona sababu ya kuwa na mpenzi mmoja. Malezi yamemfundisha kwamba anaweza kutembea na wanaume wengi bila kujali.
Ndio maana kuna wanawake ambao kufanya ngono za hovyo huku wakiwa wameolewa sio jambo wanalolionea aibu. Kumbuka tumefundishwa katika malezi yetu kuhusu ubaya wa kufanya ngono za hovyo, ndio maana tunasita au kushitakiwa na dhamira kila tunapotaka au tunapofanya hivyo.
Kuna familia mbazo bila kujua au kwa kujua hufundisha watoto kwamba kufanya ngono holela ni jambo la kawaida na mtu hapaswi kuona aibu au kushitakiwa na dhamira. Ndio maana inashauriwa sana kuwa waangalifu kwa mtu kwenda kuoa au kuolewa mahali ambapo mama na (au) baba ni Malaya na hakuna anayeonesha kukerwa na jambo hilo. Inashauriwa kuwa waangalifu kwa sababu kwenye familia kama hizo uwezekano ni mkubwa kwa watoto kuchukua tabia hizo za wazazi.
Anatamani tu kubadili nwanaume atakavyo kufanya ngono na wanaume tofauti ndio ndio anajisikia kuridhika na tendo, na sio kwa sababu ya fedha au kunufaika na jambo lingine, la hasha, kinachotafutwa ni kuridhishwa kingono.
Hivyo ni rahisi zaidi kwa mwanamke mwenye silka hiyo kugawa mwili wake kwa mwanaume yeyote atakayemfuata. Kuna wakati malezi huweza kumfanya mwanamke kushindwa kuona sababu ya kuwa na mpenzi mmoja. Malezi yamemfundisha kwamba anaweza kutembea na wanaume wengi bila kujali.
Ndio maana kuna wanawake ambao kufanya ngono za hovyo huku wakiwa wameolewa sio jambo wanalolionea aibu. Kumbuka tumefundishwa katika malezi yetu kuhusu ubaya wa kufanya ngono za hovyo, ndio maana tunasita au kushitakiwa na dhamira kila tunapotaka au tunapofanya hivyo.
Kuna familia mbazo bila kujua au kwa kujua hufundisha watoto kwamba kufanya ngono holela ni jambo la kawaida na mtu hapaswi kuona aibu au kushitakiwa na dhamira. Ndio maana inashauriwa sana kuwa waangalifu kwa mtu kwenda kuoa au kuolewa mahali ambapo mama na (au) baba ni Malaya na hakuna anayeonesha kukerwa na jambo hilo. Inashauriwa kuwa waangalifu kwa sababu kwenye familia kama hizo uwezekano ni mkubwa kwa watoto kuchukua tabia hizo za wazazi.