Kwa wanandoa tu.

Kwa wanandoa tu.

Maubero

JF-Expert Member
Joined
Feb 21, 2013
Posts
1,529
Reaction score
483
Habari wadau wa JF!
Mie na mke wangu tunalala kitanda kimoja na mtoto wetu mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi 8.Tumekuwa tukifikiria kumtafutia kitanda chake ili tuutumie uwanja wetu (kitanda) kwa uhuru zaidi.
Ila hatuna uhakika kama umri aliofikia ni muafaka kwa yeye kuhamia kwenye kitanda chake mwenyewe au la.
Hofu yetu ni kwamba, asije akawa ameshaanza kutupiga chabo tukiwa tunachuma matunda yetu.
​Naomba ushauri kwa wenzangu wenye watoto wa umri huu au wenye uzoefu kwenye suala hili.
Natanguliza shukrani
 
usimnyanyapae mtoto laleni nae mpaqka afikie umri wa kutosha,mtoto anahitaji kuwa karibu na mama yake wakati amelala ili kumjengea kujiamni na kuwa na akili njema.
watoto waliokosa joto la mama wakiwa wachanga mara nyingi wanakumbwa na ndoto za ajabu ajabu na wengine kuwachukia wanawake kama ni wa kiume na mwisho wana hatari ya kuwa mashoga.
 
Sasa mdogo wake akija ndo atolewe kitandani? Huyo ana almost miaka miwili. Saa hizi mama anatakiwa awe na kizaygote hapo. Heh!

From day one mtoto hakupaswa kulala nao kitanda kimoja. Nadhani angejiamini zaidi kwa kujitegemea toka mwanzo. Bora awekwe kitanda chake na haraka iwezekanavyo apewe chumba chake.
usimnyanyapae mtoto laleni nae mpaqka afikie umri wa kutosha,mtoto anahitaji kuwa karibu na mama yake wakati amelala ili kumjengea kujiamni na kuwa na akili njema.
watoto waliokosa joto la mama wakiwa wachanga mara nyingi wanakumbwa na ndoto za ajabu ajabu na wengine kuwachukia wanawake kama ni wa kiume na mwisho wana hatari ya kuwa mashoga.
 
panakuwaga pagumu hapo!!!!!!!!!
ni pale mama anapolala katikati huku baba huku mtoto!
daaaah!
ngoja kwanza niendelee kula raha hii makitu nahisi kama ndo basi tena,ile khabari ya kukimbizana na maji kila baada ya mbio kabla sijalala tena kwa kweli ngoja tu niendelee kuisikia kwa wengine!
NIMESHAKUZA!
 
Huo umri bado mtoto ni mdogo anahitaji kulala pamoja na wazazi wake

Kwani huo uwanja ni mdogo kiasi gani jamani hadi mshindwe kujivinjari kisa eti mtoto wenu wenyewe

Kunako majambozi huwa mnaruka sarakasi hadi iwe hatari kwa mtoto wenu? kama sio haina haja ya kumtenga ni mapema mno, walau msubiri miaka 2 na nusu hivi ndio mnamtenga.
 
Habari wadau wa JF!
Mie na mke wangu tunalala kitanda kimoja na mtoto wetu mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi 8.Tumekuwa tukifikiria kumtafutia kitanda chake ili tuutumie uwanja wetu (kitanda) kwa uhuru zaidi.
Ila hatuna uhakika kama umri aliofikia ni muafaka kwa yeye kuhamia kwenye kitanda chake mwenyewe au la.
Hofu yetu ni kwamba, asije akawa ameshaanza kutupiga chabo tukiwa tunachuma matunda yetu.
​Naomba ushauri kwa wenzangu wenye watoto wa umri huu au wenye uzoefu kwenye suala hili.
Natanguliza shukrani

Hii si kwa wanandoa tu hata mie nisie na ndoa inanihusu. Ngoja nikusaidie uone.
Kitaalam na kimalezi inashauriwa kwamba mtoto akifikisha miezi 6 anapaswa kuwa na kitanda chake, akifikisha mwaka mmoja na miezi tisa anapaswa kuwa na chumba chake. Fanya hivyo usiiharibu familia yako kimalezi.... Ubarikiwe
 
Mwanangu alipozaliwa tu, akakuta kitanda chake tayari.
Hili ndo jibu la swali la mtoa maada na ndo hii kitu imefanya tofauti kubwa ya kitabia na kujiamini kati ya matoto yetu ya kibongo na matoto ya kizungu.
 
Una haraka ya nn? Subiri mtoto afike umri wa kuacha ziwa la mamaake ndo uanze kutumia kwa uhuru uwanja wako. Una uchu ww!!
 
Wengine wanaendaga guest me nilishaona et kisa waenjoy vzur sasa cjui siku zote wanalalaje

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Mimi wanangu huwa nawalaza kwa kitanda chao siku ya kwanza tunaporudi toka hospt.
hii siyo kwa sababu ya kutawala kitanda, ila kwa sababu ya kumlinda mtoto pia. Nimeshawahi kusoma watoto wachanga wanalaliwa na wazazi wao, basi inanipa wasiwasi sana kulala na mtoto kitandani.
Mwaka 1+ unaweza kumweka chumbani kwake.... hawa watoto mimi nawaogopa sana.
kuna siku mtoto wa uncle wangu alikuwa na miaka 2+ alikuja kunilalamikia kuwa baba anampiga sana mama usiku akiwa amelala, na hapo mtoto alikuwa analala kitanda chake lakini chumba kimoja na wazazi. Nilimwamisha chumba siku hiyo bila kumwambia mamake sababu, nikaomba nilale naye mimi. Nilipoondoka nikamwambia aunt mtoto aendelee kulala chumba cha wadada, ikawa hivyo
 
Miaka miwili ni muafaka ila wakwangu nililala nao kwenye kitanda chao ila chumba kimoja hadi miaka minne ndo nikwatenga peke yao tukaanza kula maisha.
 
Habari wadau wa JF!
Mie na mke wangu tunalala kitanda kimoja na mtoto wetu mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi 8.Tumekuwa tukifikiria kumtafutia kitanda chake ili tuutumie uwanja wetu (kitanda) kwa uhuru zaidi.
Ila hatuna uhakika kama umri aliofikia ni muafaka kwa yeye kuhamia kwenye kitanda chake mwenyewe au la.
Hofu yetu ni kwamba, asije akawa ameshaanza kutupiga chabo tukiwa tunachuma matunda yetu.
​Naomba ushauri kwa wenzangu wenye watoto wa umri huu au wenye uzoefu kwenye suala hili.
Natanguliza shukrani

Day one akakaae Kwenye chumba chake inamfundisha kuwa independent weka baby monitor au camera with emotion detector .Inakuwa ngumu kwa sababu always wanakuja chumbani .kwani Hana chumba chake?mtoto akizaliwa lazima awe na chumba chake .kama wa kike tengeneza nursery room nzuri pink pink dolls and turn the room into Disney world atan'gang'ania chumba chake weka pink carpet ,nice comforter she will love .
 
usimnyanyapae mtoto laleni nae mpaqka afikie umri wa kutosha,mtoto anahitaji kuwa karibu na mama yake wakati amelala ili kumjengea kujiamni na kuwa na akili njema.
watoto waliokosa joto la mama wakiwa wachanga mara nyingi wanakumbwa na ndoto za ajabu ajabu na wengine kuwachukia wanawake kama ni wa kiume na mwisho wana hatari ya kuwa mashoga.
Since day one mtoto analala mwenyewe .Unaweka monitors ( sound and emotion detectors ) .Inajenga kujiamini kwa mtoto .Hujawahi ona mtu mzima Anaogopa kukaa mwenyewe .Mtu anakaa na roommates Hajiamini .USA 2 weeks mtoto anaenda Day care .
 
Day one akakaae Kwenye chumba chake inamfundisha kuwa independent weka baby monitor au camera with emotion detector .Inakuwa ngumu kwa sababu always wanakuja chumbani .kwani Hana chumba chake?mtoto akizaliwa lazima awe na chumba chake .kama wa kike tengeneza nursery room nzuri pink pink dolls and turn the room into Disney world atan'gang'ania chumba chake weka pink carpet ,nice comforter she will love .

Since day one mtoto analala mwenyewe .Unaweka monitors ( sound and emotion detectors ) .Inajenga kujiamini kwa mtoto .Hujawahi ona mtu mzima Anaogopa kukaa mwenyewe .Mtu anakaa na roommates Hajiamini .USA 2 weeks mtoto anaenda Day care .
mara ya mwisho umefika lini bongo?
au mleta mada anaishi USA au nchi nyingine zilizoendelea?
hizo monitor zinatumia mishumaa au taa za chemli?
 
usimnyanyapae mtoto laleni nae mpaqka afikie umri wa kutosha,mtoto anahitaji kuwa karibu na mama yake wakati amelala ili kumjengea kujiamni na kuwa na akili njema.
watoto waliokosa joto la mama wakiwa wachanga mara nyingi wanakumbwa na ndoto za ajabu ajabu na wengine kuwachukia wanawake kama ni wa kiume na mwisho wana hatari ya kuwa mashoga.
Raha tupu JF lol!
 
Since day one mtoto analala mwenyewe .Unaweka monitors ( sound and emotion detectors ) .Inajenga kujiamini kwa mtoto .Hujawahi ona mtu mzima Anaogopa kukaa mwenyewe .Mtu anakaa na roommates Hajiamini .USA 2 weeks mtoto anaenda Day care .
Wake up!
Uko wapi?
Schoolchildren-in-Kibera--001.jpg
 
Back
Top Bottom