Kwa wanandoa tu.

Kwa wanandoa tu.

Day one akakaae Kwenye chumba chake inamfundisha kuwa independent weka baby monitor au camera with emotion detector .Inakuwa ngumu kwa sababu always wanakuja chumbani .kwani Hana chumba chake?mtoto akizaliwa lazima awe na chumba chake .kama wa kike tengeneza nursery room nzuri pink pink dolls and turn the room into Disney world atan'gang'ania chumba chake weka pink carpet ,nice comforter she will love .

Since day one mtoto analala mwenyewe .Unaweka monitors ( sound and emotion detectors ) .Inajenga kujiamini kwa mtoto .Hujawahi ona mtu mzima Anaogopa kukaa mwenyewe .Mtu anakaa na roommates Hajiamini .USA 2 weeks mtoto anaenda Day care .

Hapo kwa red inakuaje hiyo EMOTION detector? Kwamba baby akikasirika, akiogopa au akifurahi nyie mnapata signal huko kwa chumba kuu? Dah wapi hiyo US Natalia ?
 
Last edited by a moderator:
Mimi wanangu huwa nawalaza kwa kitanda chao siku ya kwanza tunaporudi toka hospt.
hii siyo kwa sababu ya kutawala kitanda, ila kwa sababu ya kumlinda mtoto pia. Nimeshawahi kusoma watoto wachanga wanalaliwa na wazazi wao, basi inanipa wasiwasi sana kulala na mtoto kitandani.
Mwaka 1+ unaweza kumweka chumbani kwake.... hawa watoto mimi nawaogopa sana.
kuna siku mtoto wa uncle wangu alikuwa na miaka 2+ alikuja kunilalamikia kuwa baba anampiga sana mama usiku akiwa amelala, na hapo mtoto alikuwa analala kitanda chake lakini chumba kimoja na wazazi. Nilimwamisha chumba siku hiyo bila kumwambia mamake sababu, nikaomba nilale naye mimi. Nilipoondoka nikamwambia aunt mtoto aendelee kulala chumba cha wadada, ikawa hivyo

Mwenyewe last week tu mama mmoja jirani yangu kagonga vyombo (mvinyo) akamlalia mwanae wa miaka miwili mapaka mtoto akatangulia mbele za haki..
Rest in peace mtoto.
 
Wa kwetu ana mwaka na miezi tisa tunalala naye and we love it. Sijui siko atakapoanza kulala peke yake itakuwaje, tutammiss sana but kwa sasa hata wazo la kuwa analala peke yake hatuna. Kila mtu ana namna yake ya malezi, hakuna formula moja. Obviously kama ni watu wa magomvi kila siku huko chumbani, si nzuri kwa mtotn but kama mko peaceful, why not sleep with ur baby? Inatengeneza bond kati ya wazazi na mtoto. Do what is best 4ur family.
 
Mwenyewe last week tu mama mmoja jirani yangu kagonga vyombo (mvinyo) akamlalia mwanae wa miaka miwili mapaka mtoto akatangulia mbele za haki..
Rest in peace mtoto.
cc. Aine
 
Last edited by a moderator:
Mwenyewe last week tu mama mmoja jirani yangu kagonga vyombo (mvinyo) akamlalia mwanae wa miaka miwili mapaka mtoto akatangulia mbele za haki..
Rest in peace mtoto.

masikini, sijui aliliaje. it will take her to grave kwakweli!
 
ni mama alishindwa kulet go; lol
si unajua watoto wa mwisho huwa atukui!
ha haaaa, bahati yako ni mdada.....
ungekuwa mkaka ungemsumbua sana mkeo.....
kuna aunt yangu alinipa bonge la onyo kuwa nisiolewe na mtoto wa mwisho, lol!
 
Nyumba za kupanga,chumba cha mtoto utakitoa wapi na ugumu huu wa maisha? mwanetu ana miaka2 na miezi 8 tunalala nae na wala hakuna tatizo! malezi hutofautiana!
 
Mimi na wife kila mtu ana kitanda chake, chumba kimoja,atayemhitaji mwenzake anamfuata kitandani kwake.Watoto wana chumba chao(Mmoja ana 3yrs na mwingine 1yr)
 
Mimi na wife kila mtu ana kitanda chake, chumba kimoja,atayemhitaji mwenzake anamfuata kitandani kwake.Watoto wana chumba chao(Mmoja ana 3yrs na mwingine 1yr)

hii nayo kali, hii ndoa kweli jamani?
 
huwa nampunguzia idadi ya kunyonya usiku kadiri anavyokua.
anapokuwa mchanga ananyonya mara kwa mara maana naamini anachoka kuvuta mapema, ndo maana nalala naye chumbani kwangu.
anapokua huwa maximum kumnyonyesha usiku ni mara 3, na ndo maana nakaa ananyonya mpaka achoke na kuacha mwenyewe, then akilala nina uhakika anaweza lala zaidi ya masaa 3.
kuna siku naweza amka mara moja tu.
nb. huwa simwamshi mtoto kunyonya, namnyonyesha akiwa ameamka. mara nyingi watoto wanaamshwa na kulowa mkojo au njaa. kama kulowa tu nikimbadilisha huwa analala tena, na mimi narudi kulala
Asante FP na Aine.kuna kitu najifunza kutoka kwenu.
 
Last edited by a moderator:
usimnyanyapae mtoto laleni nae mpaqka afikie umri wa kutosha,mtoto anahitaji kuwa karibu na mama yake wakati amelala ili kumjengea kujiamni na kuwa na akili njema.
watoto waliokosa joto la mama wakiwa wachanga mara nyingi wanakumbwa na ndoto za ajabu ajabu na wengine kuwachukia wanawake kama ni wa kiume na mwisho wana hatari ya kuwa mashoga.

Sasa mdogo wake akija ndo atolewe kitandani? Huyo ana almost miaka miwili. Saa hizi mama anatakiwa awe na kizaygote hapo. Heh!

From day one mtoto hakupaswa kulala nao kitanda kimoja. Nadhani angejiamini zaidi kwa kujitegemea toka mwanzo. Bora awekwe kitanda chake na haraka iwezekanavyo apewe chumba chake.

.... King'asti nakubaliana na wewe nami nimeshanga kidogo hoja ya boscontaganda..wazungu tangu siku ya kwanza mtoto anatengwa...
 
ha haaaa, bahati yako ni mdada.....
ungekuwa mkaka ungemsumbua sana mkeo.....
kuna aunt yangu alinipa bonge la onyo kuwa nisiolewe na mtoto wa mwisho, lol!
Huyo aunt alikuambia ukiolewa na mtoto wa mwisho kutatokea nini?Nauliza kwa kuwa jirani yangu ni last born kwao na anaishi vizuri na mkewe.
 
Nyumba za kupanga,chumba cha mtoto utakitoa wapi na ugumu huu wa maisha? mwanetu ana miaka2 na miezi 8 tunalala nae na wala hakuna tatizo! malezi hutofautiana!
..inawezekana..
 
usimnyanyapae mtoto laleni nae mpaqka afikie umri wa kutosha,mtoto anahitaji kuwa karibu na mama yake wakati amelala ili kumjengea kujiamni na kuwa na akili njema.
watoto waliokosa joto la mama wakiwa wachanga mara nyingi wanakumbwa na ndoto za ajabu ajabu na wengine kuwachukia wanawake kama ni wa kiume na mwisho wana hatari ya kuwa mashoga.
Kama kuna sociologist atusaidie kufanya utafiti kuhusiana na kipengele cha RED." Association between homosexuallity and childhood parental care". sijui niko sahihi?unajua tena, kiingereza chetu cha shule za kata(cha kuungaunga)
 
FP huyo kumbuka ni mlevi jamani, inasikitisha sana atahukumiwa daima, RIP baby
sidhani kama hiyo ilikuwa siku yake ya kwanza kulewa.......
kama siku nyingine alikuwa analewa na hiyo ajali haijawahi kutokea basi ujue hata mtu ambaye halewi anaweza kupata hiyo ajali pia. Ajali ni ajali Aine
 
Last edited by a moderator:
.... King'asti nakubaliana na wewe nami nimeshanga kidogo hoja ya boscontaganda..wazungu tangu siku ya kwanza mtoto anatengwa...
siyo wazungu tu Gefu....
mimi mbongo hata nje ya TZ sijatoka na sijawahi lala na mtoto kwa kitanda changu
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom