jamiif
JF-Expert Member
- Apr 30, 2012
- 2,413
- 995
wanandoa, ebu tuelezane ukweli hapa, hivi ni kwa lipi hasa linatufanya baadhi yetu tuwe tunatoka nje ya ndoa zetu ilhali tuna wenza wetu tunaowapenda kwa dhati? hivi ina maana pale mnapofunga ndoa mmoja wenu huwa anadanganya au anajaribu ndoa au? tunaweka mazingira yasiyovutia hasa kwa wale wasio kwenye ndoa kutotamani kuingia huko kwa kuwa kila kukicha wanachokisikia kuhusu ndoa ni bad news. jamani karibuni tujuzane ni kwa nini hali hii imekithiri sana siku hizi, na ni namna gani tutajaribu kuelimishana ili basi tuachane na mambo hayo na kuheshimu ndoa zetu.
nawasilisha.
nawasilisha.