Kwa wana Hanang' iliyoongozwa na Mh Sumaye na sasa Mh Mary Nagu

Tatizo la Hanang' ni pale ofisi za Halmashauri, DED mama Gody Pamba na wasaidizi wake hawana uzalendo na ile wilaya kwani hata OC zinapoingia fedha nyingi hungia kwenye matumizi hewa na hata Nagu anapoambiwa kwa kuwa amemleta kutokana na urafiki wao humkingia kifua. Gody Pamba ameletwa Hanang' na Mary Nagu baada ya Chadema kushinda kata ya Katesh katika uchaguzi mkuu 2005 na DED aliyekuwepo ambaye alikuwa mchapakazi mwenye uwezo wa kuziba mianya ya ufisadi akahamishia halmashauri ya Kishapu, sababu ikiwa ni Chadema kushinda Kata ya Katesh, kukataa kumpa Nagu pesa za kampeni tofauti na taratibu na Majungu toka kwa wakuu wa idara pia yalitumika kumtoa huyu ndg E.L. Shimwela, kwani kwa muda mfupi aliokuwepo Hanang' ufanisi ulionekana na matumizi hewa yalidhibitiwa.
 
Mie naona wanasiasa wakonge wa ccm hawapendi maendeleo ya elimu kwenye majmbo yao, kwa maana watu wakielimika ni challange kwao, huenda wasiwakubali.
Katika tz wilaya ambaye huduma muhimu za jamii ni duni sana, nasema tena sana si kidogo ni Hanang mojawapo ambako mpaka sasa imeongozwa na mawaziri wawili (sumaye na sasa Nagu) lkn wilaya hii huduma muhimu kama vile maji, matibabu na elimu ni duni sn ktk baadhi ya maeneo mfano kata ya Gehandu na B/lalu ambako watu huchota maji kwa masaa 12 ktk baadhi ya maeneo na maji haya mara pengine si salama kwa afya ya binadamu kutokana na meneo yakochotwa haya maji, si jambo la kushangaa kuwakuta watoto weng tu hawajaenda shule wakichunga kutokana na shule kuwa mbali sn ktk baadhi ya maeneo nimewahi ona mwanafunz wa primary akitembea masaa 2 njiani afike shule, huduma za afya kama matibu zipo mbali sn ktk baadhi ya maeneo ambako watu hulazimika kutembea masaa 6-8 mara pengine. je hawa viongozi wetu hawaoni hilo tatizo? kuwa hizi huduma muhimu za jamii ziwepo karibu kwa ajili ya maendeleo ya jamii?. Kweli kwa hili tutafikia tz vision 2025 au ni ndoto?.
 
Maendeleo yatapatilanaje ikiwa Mbunge hakutani na makundi mbalimbali ya jamii kama watumishi, wakulima na wafugaji pamoja na wafanyabiashara kujua changamoto na matatizo yao? Yeye huwa anagwa misaada tu ambayo kwa watanzania ya leo ni kuwanyima haki yao ya kufikiri, tunahitaji tujadili naye namna ya kutatua matatizo yetu siyo kutuhonga na vihela vya ufisadi.
 
Katika tz wilaya ambaye huduma muhimu za jamii ni duni sana, nasema tena sana si kidogo ni Hanang mojawapo ambako mpaka sasa imeongozwa na mawaziri wawili (sumaye na sasa Nagu) lkn wilaya hii huduma muhimu kama vile maji, matibabu na elimu ni duni sn ktk baadhi ya maeneo mfano kata ya Gehandu na B/lalu ambako watu huchota maji kwa masaa 12 ktk baadhi ya maeneo na maji haya mara pengine si salama kwa afya ya binadamu kutokana na meneo yakochotwa haya maji, si jambo la kushangaa kuwakuta watoto weng tu hawajaenda shule wakichunga kutokana na shule kuwa mbali sn ktk baadhi ya maeneo nimewahi ona mwanafunz wa primary akitembea masaa 2 njiani afike shule, huduma za afya kama matibu zipo mbali sn ktk baadhi ya maeneo ambako watu hulazimika kutembea masaa 6-8 mara pengine. je hawa viongozi wetu hawaoni hilo tatizo? kuwa hizi huduma muhimu za jamii ziwepo karibu kwa ajili ya maendeleo ya jamii?. Kweli kwa hili tutafikia tz vision 2025 au ni ndoto?.

umeichukulia Hanang kama kesi maalumu ya kuelezea matatizo ya watz kwa ujumla au? maana yake haya ya Hanang yako kila mahali na sijaelewa kwa nini unataka kuonyesha kama Mh Sumaye na Nagu kama viongozi wa zamani na sasa wa kitaifa walikua na jukumu rasmi na maalumu kwa ajili ya kuendeleza jimbo lao(au kiupendeleo kama unavyotaka wewe), Watz kweli hatueleweki sasa kiongozi wa kitaifa atafanyaje kazi kwenye jimbo lake huku akikabwa na makujumu ya kitaifa? serikali siyo mtu na mtu siyo serikali hizi Hanang hapa tz zimejaa kila mahali na tukianza kusema kila kiongozi wa kitaifa aendeleze kwake tunaanza kujenga ukanda na ukabila bila kujijua.
 
umeichukulia Hanang kama kesi maalumu ya kuelezea matatizo ya watz kwa ujumla au? maana yake haya ya Hanang yako kila mahali na sijaelewa kwa nini unataka kuonyesha kama Mh Sumaye na Nagu kama viongozi wa zamani na sasa wa kitaifa walikua na jukumu rasmi na maalumu kwa ajili ya kuendeleza jimbo lao(au kiupendeleo kama unavyotaka wewe), Watz kweli hatueleweki sasa kiongozi wa kitaifa atafanyaje kazi kwenye jimbo lake huku akikabwa na makujumu ya kitaifa? serikali siyo mtu na mtu siyo serikali hizi Hanang hapa tz zimejaa kila mahali na tukianza kusema kila kiongozi wa kitaifa aendeleze kwake tunaanza kujenga ukanda na ukabila bila kujijua.
Hatusunguzh upendeleo hata kidogo, tunasema hawa viongoz wanasikiliz wananchi wao kwa kiasi gani na kushirikiana na wananchi ktk kubali matatizo yanayokabili wananchi na kuhakikisha pesa za miradhi ya jamii inatumika ipasavyo badala ya kuja kuomba kura nakupotea baada ya kupewa dhamana ya kuongoz.
 
Pesa yawezekana zinapelekwa lakini ikiwa ofisi ya halmashauri imejaa mchwa na panya we unategemea nini hapo?
 
hesabu kata ya bassotu linachukuliwa na cdm mgombea wake ni makini sana na ana uwezo mkubwa sana nakupa jina ya romani cypriane mlete wa chama kingine anayeweza kupambana naye na elimu yake ipo juu inatosheleza ni mwalimu amepita vidato na huwezi kumnunua kama wale wengine wanao nunuliwa kwa pesa ndogo sana na kuuza kata

 
Binafsi naifahamu vizuri jimbo la Hanang, na tokea nianze kupiga kura sijawahi kuichagua ccm kutokana na jinsi walivyotutelekeza sisi wananchi wa Hanang.
Jimbo la Hanang limebarikiwa kuwa na mlima ambao una vyanzo vingi vya maji, mfano maeneo ya Nangwa mlimani, Jarodom, Gendabi.
Maji yalitolewa Gendabi na serikali yakapelekwa mashamba ya NAFCO, huku wanakijiji wanateseka kupata huduma ya maji. Vijiji vya Mogitu, Gehandu, Balangdalalu just to mention few vimekuwa vikipata shida ya maji kwa muda mrefu.
Kwa mfano watu gehandu kupata maji nilazima wasafiri zaidi wa kilomita 15 mpaka 20 kupata maji.
Jimbo la Hanang linahitaji kiongozi mwenye ujasiri, ambaye anaweza kuthubutu kwa namna yoyote ile.
Jimbo la Hanang lilipata bahati ya kuwa na waziri mkuu kwa muda wa miaka kumi, lakini hakuna alichosaidia kimaendeleo.
Sumaye kuwa waziri mkuu ndiyo chanzo cha kudorora kwa maendeleo ya wilaya, kutokana na kuyaua mashamba ya NAFCO kwa makusudi. Nakumbuka baada ya kushinda ubunge 1995 na kuteuliwa kuwa waziri Mkuu ziara yake ya kwanza ilikuwa CMSC, akaahidi kuyauza mashamba ya nafco yote hata kwa shilingi kisa hawakumpigia kura, baba yangu alimchallenge sana na kumjibu vibaya, kitendo kilichogharimu ajira yake.
Hanang kwa sasa ina madiwani 25, ambapo 12 wanatoka CCM na 12 wa CDM 1 wa CUF.
Ni imani yangu kuwa 2015 wananchi wa Hanang hawatafanya makosa.

Mkuu na ifutwe kabisa CCM huko Hanang na Sumaye hata Urais aukose kabisa maana kama jimbo tu alishindwa ataweza taifa.
 
kuna eneo linaitwa sagara.na ishipunga maji safi ni story...achana na hanang' shida
 
kuna eneo linaitwa sagara.na ishipunga maji safi ni story...achana na hanang' shida

Mkuu Sagara na Ishponga zipo kwenye jimbo la Singida Kaskazini kwa Nyalandu, huyu huyu anayeutaka urais.

Maccm hovyo kabisa
 
umeichukulia Hanang kama kesi maalumu ya kuelezea matatizo ya watz kwa ujumla au? maana yake haya ya Hanang yako kila mahali na sijaelewa kwa nini unataka kuonyesha kama Mh Sumaye na Nagu kama viongozi wa zamani na sasa wa kitaifa walikua na jukumu rasmi na maalumu kwa ajili ya kuendeleza jimbo lao(au kiupendeleo kama unavyotaka wewe), Watz kweli hatueleweki sasa kiongozi wa kitaifa atafanyaje kazi kwenye jimbo lake huku akikabwa na makujumu ya kitaifa? serikali siyo mtu na mtu siyo serikali hizi Hanang hapa tz zimejaa kila mahali na tukianza kusema kila kiongozi wa kitaifa aendeleze kwake tunaanza kujenga ukanda na ukabila bila kujijua.

umesema kweli
 
Back
Top Bottom