Kwa waliozaa kabla ya ndoa

Kwa waliozaa kabla ya ndoa

iMind

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2011
Posts
3,156
Reaction score
5,265
Mimi ni mwanaume nilibahatika kupata mtoto wa kiume nje ya ndoa.
Sasa miaka 10 baadae nimeoa na nimemchukua huyu mtoto wangu naishi naye.

Sasa mke wangu ameniwekea masharti ambayo nafikiri ni magumu kutekelezeka. Naamini kuwa mwanamke niliye zaa naye ana haki ya kumuoma mtoto wake kila anapohitaji kufanya hivyo.

Sasa mke wangu hataki huyu mama mtoto afike nyumbani kumuona. Hataki mtoto aende kwa mama yake. Anataka mama mtoto akitaka mtoto tumtume housegirl ampeleke mtoto hoteli foleni halafu wakimaliza kuongea arudi naye.

Hali hii imeniingiza kwenye migogoro maana mama mtoto anaona namnyanyasa na upande mwingine mke wangu anaona pia namnyanyasa.

Hebu niambieni what is the beat way ku deal na hii situation?
 
Hapo mkeo yupo sawa kabisa...! Afike kwako ili iwaje? Kama mama mtoto anataka kumuona mwanae amfate sehemu tu, sio kwako!
 
kuwe na utaratibu maalum wa kuumuona mtoto, mwingine anajifanya anataka kuona mtoto kumbe ndio anajileta leta kijanja. ila kama mazingira yanaruhusu bora mtoto alelewe na mama yake mzazi tu.
 
Mimi ni mwanaume nilibahatika kupata mtoto wa kiume nje ya ndoa.
Sasa miaka 10 baadae nimeoa na nimemchukua huyu mtoto wangu naishi naye.

Sasa mke wangu ameniwekea masharti ambayo nafikiri ni magumu kutekelezeka. Naamini kuwa mwanamke niliye zaa naye ana haki ya kumuoma mtoto wake kila anapohitaji kufanya hivyo.

Sasa mke wangu hataki huyu mama mtoto afike nyumbani kumuona. Hataki mtoto aende kwa mama yake. Anataka mama mtoto akitaka mtoto tumtume housegirl ampeleke mtoto hoteli foleni halafu wakimaliza kuongea arudi naye.

Hali hii imeniingiza kwenye migogoro maana mama mtoto anaona namnyanyasa na upande mwingine mke wangu anaona pia namnyanyasa.

Hebu niambieni what is the beat way ku deal na hii situation?

Mkeo yuko sawa.fanya mkeo amgezaa kabla na sasa anakuja nyumbani yule bwana alozaa nae,niambie utajisikiaje?
 
Aliyekuwepo ndani ndiyo mwenye nguvu kwa sababu. msikilize mkeo huenda anasababu zake kufanya hayo yote. ila pia mtoto anahaki ya kumuona na kuongea na mama yake. fanya lililojema chekecha akili.
 
Mimi ni mwanaume nilibahatika kupata mtoto wa kiume nje ya ndoa.
Sasa miaka 10 baadae nimeoa na nimemchukua huyu mtoto wangu naishi naye.

Sasa mke wangu ameniwekea masharti ambayo nafikiri ni magumu kutekelezeka. Naamini kuwa mwanamke niliye zaa naye ana haki ya kumuoma mtoto wake kila anapohitaji kufanya hivyo.

Sasa mke wangu hataki huyu mama mtoto afike nyumbani kumuona. Hataki mtoto aende kwa mama yake. Anataka mama mtoto akitaka mtoto tumtume housegirl ampeleke mtoto hoteli foleni halafu wakimaliza kuongea arudi naye.

Hali hii imeniingiza kwenye migogoro maana mama mtoto anaona namnyanyasa na upande mwingine mke wangu anaona pia namnyanyasa.

Hebu niambieni what is the beat way ku deal na hii situation?

Mpeleke mtoto boarding school visiting day Mama yake ataenda huko.

Ila una mtihani mgumu sana kimaisha wengi hapa hawaelewi ni wepesi tu kukushauri waonavyo.

Mtoto anahitaji kumjenga kisaikolojia kwa nini hauishi na Mama yake. Pole sana.
 
Mama mtoto ana haki ya kumuona mwanae ukizingatia mtoto ameishi kwa mama muda mrefu nae anakuwa amemkumbuka mama...

Sasa hapo ni kumuweka sawa huyo mama mtoto kipi kifanyike ili aweze kumuona mtoto kwa uhuru.... Lakini pia ni vyema ukamsikiliza mkeo katika hili nadhani fuata ushauri wa Matola hapo
 
Last edited by a moderator:
kuwe na utaratibu maalum wa kuumuona mtoto, mwingine anajifanya anataka kuona mtoto kumbe ndio anajileta leta kijanja. ila kama mazingira yanaruhusu bora mtoto alelewe na mama yake mzazi tu.

Na mwingine akijifanya anaenda kusalimia mtoto kumbe anahamia taratibu?
 
Umpe nafasi mama wa mtoto kukaa na mwanaye wakati mwingine hasa wa rikizo itapunguza uhitaji wa kuja kumtembelea mara kwa mara,ila mkeo naye asiwe insecure kiasi icho,after all those years bado anaona mzazi mwenzio ni tishio!!Lazima at one point ninyi kama wazazi mtaonana tu,ingawa siafiki swala la mzazi mwenza kuja hapo kwako.
 
Mama mtoto ana haki ya kumuona mwanae ukizingatia mtoto ameishi kwa mama muda mrefu nae anakuwa amemkumbuka mama...

Sasa hapo ni kumuweka sawa huyo mama mtoto kipi kifanyike ili aweze kumuona mtoto kwa uhuru.... Lakini pia ni vyema ukamsikiliza mkeo katika hili nadhani fuata ushauri wa Matola hapo

Tungekuwa na utaratibu wa Magharibi ningesema tofauti. Ila kwetu sisi wabongo na vijitabia vyetu vya kutoheshimu ndoa za watu, namuunga mkono mke.

Mleta mada akae na mzazi mwenzake wapange jinsi ya kumlea mtoto bila kumsababishia matatizo ya kisaikolojia. Ila katika mchakato huo, wawe waangalifu wasifunje ndoa.

Hakuna ruhusa hata mara moja, mama wa mtoto kujileta leta nyumbani kisa ni kuja kumwona mtoto!
 
sijui nisemeje, lakini ukweli haiwezekani huyo mama wa mtoto aje hapo kuona mtoto, tena haikubaliki, moyo wa mwanamke umebeba mengi, yaani sijui ni semeje ili unielewe, tafuta namna ambayo mama wa mtoto atamuona mwanae lakini sio nyumbani ukoishi na mkeo, kama inawezekana huyo bidada anakaa karibu basi awe anapelekewa mtoto anashinda nae au kukaa nae then anamtuma mtu anamrudisha, sio habari ya yeye kukanyaga hapo nyumbani, kwanza unaweza kusabisha matitizo ambayo hukutarajia, unajua akili za wanawake wewe? kwanza hata wewe acha kucheka cheka na huyo mwanake, mlizaa yakaisha, hapo ni suala la mtoto tu, habari ya mazoea ya kufuatana nyumbani mmhm!, awe anapelekewa mtoto kwishaaaaaa.


Mungu weeeee! ningekuwa mimi hata muda wa kuja jf kuuliza usingepata, siku nyingi ningekuwa nimefanya maamuzi magumu, mwanamke aliezaa na mme wangu aje nyumbani kwangu. kiruuuu
 
Mimi ni mwanaume nilibahatika kupata mtoto wa kiume nje ya ndoa.
Sasa miaka 10 baadae nimeoa na nimemchukua huyu mtoto wangu naishi naye.

Sasa mke wangu ameniwekea masharti ambayo nafikiri ni magumu kutekelezeka. Naamini kuwa mwanamke niliye zaa naye ana haki ya kumuoma mtoto wake kila anapohitaji kufanya hivyo.

Sasa mke wangu hataki huyu mama mtoto afike nyumbani kumuona. Hataki mtoto aende kwa mama yake. Anataka mama mtoto akitaka mtoto tumtume housegirl ampeleke mtoto hoteli foleni halafu wakimaliza kuongea arudi naye.

Hali hii imeniingiza kwenye migogoro maana mama mtoto anaona namnyanyasa na upande mwingine mke wangu anaona pia namnyanyasa.

Hebu niambieni what is the beat way ku deal na hii situation?
Rudi ukaoe ndaniyandoa mkewako nihuyo uliemwacha tamaazinatuumiza ukweli damuaitokuacha name amani namajonziyahuyumama ushauri tu
 
nashukuru tumeuona heri kwako pia.
mpaa heri yamakampya jamani,,shem husinyo na wote ukosalimia niko ugangda narekebisha amani jeshini kumechafuka jamaakaanza fukuzafukuza hatawqliorudi nao anaarest wasiende hatachooni mbaya anaitaji kuongeanao sasa una,uarrest mutu alafu unataka ongea nae tena bila mwanasheriawake loh niko namaji ya tbjoshua najqribukumwaga hukujeshini
 
Mpeleke mtoto boarding school visiting day Mama yake ataenda huko.

Ila una mtihani mgumu sana kimaisha wengi hapa hawaelewi ni wepesi tu kukushauri waonavyo.

Mtoto anahitaji kumjenga kisaikolojia kwa nini hauishi na Mama yake. Pole sana.

Ushauri mzuri sana huu. Soon nitakuwa kwenye position ya mleta mada. Moja ya Jambo ambalo limekuwa lina niumiza kichwa ni hili

Mzee wangu alinipa ushauri kama huu wa kumpeleka mtoto boarding lakini boarding kwa mtoto mdogo nayo ni tatizo kidogo. Utashindwa kumfuatilia maendeleo yake kwa ukaribu ukizingatia walimu wenyewe hawa wa siku hizi ni tabu. Lakini pia wakati wa likizo bado tatizo litakuwa palepale.

Mimi Nadhani kama unaishi na wazazi wako Au shangazi yako mkoa mmoja mtoto awe anapelekwa Huko halafu mama yake anaenda kuonana naye. Kuwe na kuna ratiba maalumu,Mfano kila Jmosi.

Kimsingi mke wako yupo sahihi,huyo mama wa mtoto wako hatakiwi kabisa kugusa kwenu wala mtoto hatakiwi kwenda kwake maana atamjaza ujinga.
 
mpaa heri yamakampya jamani,,shem husinyo na wote ukosalimia niko ugangda narekebisha amani jeshini kumechafuka jamaakaanza fukuzafukuza hatawqliorudi nao anaarest wasiende hatachooni mbaya anaitaji kuongeanao sasa una,uarrest mutu alafu unataka ongea nae tena bila mwanasheriawake loh niko namaji ya tbjoshua najqribukumwaga hukujeshini

Mpwa nimeshakuelewa
 
Back
Top Bottom