Kwa waliosoma Majengo secondary Moshi

Kwa waliosoma Majengo secondary Moshi

Natamani Manispaa wairudishe ile shule yetu ya Msingi kwani nimesoma hapo na wazazi wetu walichangia ujenzi wa madarasa mnayojisifia nayo eti ya sekondari kwani hao mapadri walishindwa kuijenga sehemu nyingine?

Ufisadi mtupu ulitumika hapa eti kanisa!nalo linaingia katika mikataba ya kifisadi! haiwezekani!!!!!!!!!!.

Nasema tutairudisha tu hii shule siku moja iendelee kuwa ya msingi au sekondari ya kata, Nasema iko siku haiwezekani serikali iiuzie kanisa shule yetu tena ya msingi eti sekondari ya kulipia huu ni wizi mtupu hakuna la kujisifia hapa tena ufisadi unaolihusisha kanisa ehee!!!.

Mkuu thibitisha ukweli wa unayonena sio kueneza propaganda za chuki. S/kali inafurahia mchango wa Majengo secondary katika sekta ya elimu. Acha itikadi za udini hapa jf
 
Natamani Manispaa wairudishe ile shule yetu ya Msingi kwani nimesoma hapo na wazazi wetu walichangia ujenzi wa madarasa mnayojisifia nayo eti ya sekondari kwani hao mapadri walishindwa kuijenga sehemu nyingine?

Ufisadi mtupu ulitumika hapa eti kanisa!nalo linaingia katika mikataba ya kifisadi! haiwezekani!!!!!!!!!!.

Nasema tutairudisha tu hii shule siku moja iendelee kuwa ya msingi au sekondari ya kata, Nasema iko siku haiwezekani serikali iiuzie kanisa shule yetu tena ya msingi eti sekondari ya kulipia huu ni wizi mtupu hakuna la kujisifia hapa tena ufisadi unaolihusisha kanisa ehee!!!.

Haaaa lakini si pia shule ya msingi ipo
 
Napenda kuwakumbusha Kuwa Majengo ni shule ambayo Sita sahau mana nilijifunza Mengi kupitia Broo Lyimo nimemmiss sana Kama wewe ni wa Majengo tukumbishane chochote kuhusu shule yetu wadau.

cjasoma majengo,bt naiheshimu sana hii shule..ina mchango mkubwa sana katika maisha yangu..long live majengo.
 
Pamoja na kwamba wengi mnaiponda hii shule, lakini ukweli unabaki kwamba ubora wa shule ni kichwa chako!! Sisi tumesoma pale miaka hiyo ya 2000 na tukanyoosha vizuri tuu.. Uzuri ni kwamba shule hii ukiamua kuwa serious, materials + walimu wazuri wapo, ila ukiamua kuwa muuza sura ndio hivyo tena!
Nimewakumbuka sana walimu wa enzi hizo sijui kama bado wapo kina Mr. Lyatuu, Mr. Mlay, Mr. Sendoro (RIP), Mr. James, "Prof" Makundi, Miss Mkonyi, Mama Minja, Mushi B, Pedejee Kichawele.. na kuna yule mzee mpishi Mr. James.. mlinzi Mzee Ali tulikua tunamtoa shing 100 anatuacha tunaenda kula Fast Fry.. dah..
Halafu kuna wanafunzi walikuwa maarufu sana miaka ya 98 - kina Edgar Kisakisa, Ombeni, Mawenya.., sijui wako wapi ssa ivi? Na kile kiduka pale ndani cha matozi waliokuwa wanashindia "matofali" na coca mwaka mzima sijui kipo? dah..
 
Haaaa lakini si pia shule ya msingi ipo
Ilipo shule ya msingi ndiyo ilitakiwa iwe sekondari hilo ndiyo eneo halali la misheni ya katoliki,ilipo sekondari hivi sasa ilikuwa shule ya msingi toka miaka ya 1930
 
Mkuu thibitisha ukweli wa unayonena sio kueneza propaganda za chuki. S/kali inafurahia mchango wa Majengo secondary katika sekta ya elimu. Acha itikadi za udini hapa jf
Inaniuma roho kwani nimesoma hapo ikiwa shule ya msingi wala si udini ila kilichofanyika ni mchezo mchafu,hii ilikuwa shule ya msingi toka miaka ya 1930.hadi juzijuzi ilipoporwa.
 
Mimi nilimaliza Majengo mwaka 1993 kulikuwa hakuna high school. By then Head Master alikuwa Pius Kihuru RIP, ila i remember some of the teachers JB, Masoud, Kichawele. Nilipata div 2 that time one zilikuwa rare kulikuwa hakuna kidesa, nilienda Pugu High School then nikaenda Salzurg Austria kwa degree course. Sasa hivi ni mfanyabiashara mjini Arusha I own a tour company, partner katika hoteli zilizoko porini na pia ni Consultant katika mambo ya hoteli.

kila shule inaweza kuwa mbaya au nzuri ni jitihada zako binafsi zinahitajika.

Hello so class met ninaowakumbuka - Edwin Ngosi, Edwin Sanda, Casmir Mawalla, Teotim Swai, Getrude Urio,
 
Inaniuma roho kwani nimesoma hapo ikiwa shule ya msingi wala si udini ila kilichofanyika ni mchezo mchafu,hii ilikuwa shule ya msingi toka miaka ya 1930.hadi juzijuzi ilipoporwa.

Haikuporwa kama unavyofikiri. Wakati Majengo secondary ikianzishwa kuliko na shule tatu za sekondari ndani ya manispaa ambazo ni mawenzi, old moshi na moshi tech. Shule hizi zilikua hazitoshelezi idadi ya watoto wanaomaliza shule ya msingi kwani wakati huo kulikua na shule za msingi nyingi tu kama Majengo, kibo, Kilimanjaro, njoro, langoni, Mandela, Padua, msaranga, kiboriloni, mawenzi, jamhuri, muungano, korongoni, mwenge, n.k. Zote hizi watoto waliomaliza elimu ya msingi wasingetoshea kwa sekondari tatu za mawenzi, old moshi na moshi tech. Ndipo s/kali ikaruhusu ndani ya shule ya msingi mawenzi kuanzishwe kibo sekondari na ndani ya shule ya msingi Majengo kuanzishwe Majengo sekondari. Serikali ilifanya uamuzi sahihi kabisa
 
Haikuporwa kama unavyofikiri. Wakati Majengo secondary ikianzishwa kuliko na shule tatu za sekondari ndani ya manispaa ambazo ni mawenzi, old moshi na moshi tech. Shule hizi zilikua hazitoshelezi idadi ya watoto wanaomaliza shule ya msingi kwani wakati huo kulikua na shule za msingi nyingi tu kama Majengo, kibo, Kilimanjaro, njoro, langoni, Mandela, Padua, msaranga, kiboriloni, mawenzi, jamhuri, muungano, korongoni, mwenge, n.k. Zote hizi watoto waliomaliza elimu ya msingi wasingetoshea kwa sekondari tatu za mawenzi, old moshi na moshi tech. Ndipo s/kali ikaruhusu ndani ya shule ya msingi mawenzi kuanzishwe kibo sekondari na ndani ya shule ya msingi Majengo kuanzishwe Majengo sekondari. Serikali ilifanya uamuzi sahihi kabisa

Uongo huo kama ni uamuzi wa serikali kwa nini ilianzisha sekondari ya kulipia,hivi ni wangapi waliamua shule ya msingi ya serkali iwe sekandari ya kulipia ina maana watoto wa wasiokuwa nacho wasipate elimu kwa kukosa ada? tena wakati maamuzi hayo yanafikiwa Kilimanjaro ilikuwa inaongoza kwa kuwa za sekondari nyingi za kulipia nakumbuka wakati wa likizo huwezi kupata usafiri wa basi kwenda Dar hata treni ilikuwa ni shida hadi wanafunzi waishe kusafiri.Hata hivyo shule za sekondari za serikali zilikuwa zinatosha idadi ya wanafunzi wa wakati huo kulikuwa na sekondari zingine zilizoanzishwa kama Mji mpya,Msaranga pamoja na zilizokuwepo kwa catchment ya wakati huo zilikuwa zinatosha, na Kilimanjaro walishaanza toka zamani kuchangia ujenzi wa madarasa.

Hoja ya msingi hapa ni kwanini serikali iliiuza shule yetu kwa kanisa kuanzisha sekondari ya kulipia? na siyo sekondari ya serikali kama ilivyokuwa Mawenzi? pia kwa nini serikali kwa maana ya Manispaa kuuza nguvu za wazazi wetu waliochangia ujenzi wa madarasa ya shule ya msingi ya wakati huo ya Majengo ambayo sasa hivi ni sekondari ya Majengo.

Kama haufahamu jambo hili litaendelea kuitafuna CCM na haitaweza kupata kiti cha ubunge hata udiwani Moshi kati kamwe kwani siyo mimi tu inaniuma karibu nusu ya watu wa makamu walio moshi hivi sasa kama siyo wao waliosoma shule ya msingi majengo basi ni wazazi wao au babu zao.Kinachosikitisha zaidi ni kuwa CCM wanamsimamisha mgombea ambaye ni mtuhumiwa namba moja katika sakata la uuzwaji wa hii shule eti awe mbunge.yetu macho lakini iko siku.
 
I luv majengo sec,ni best place ever,mie nimemaliza six 2010! Brother lyimo ni master mzur sana aliweza kuiongoza shule vzr
 
Hahahaha kweli kabisa mkuu

umeonaee saiv pepa la form 2 au 4 likikaribia madogo wote kutoka Kiborilon,Uru,Rau, shule za mosh vijijin wanaingia mitaa ya majengo kusaka gaka au tangopori km wanavyoita yan ni full majanga kwa mdau wa elimu mchunguzi anaetoka maeneo haya atakuwa shahidi wa hili.
 
Back
Top Bottom