Tatizo huyo jamaa kakalili mambo ya umeme analeta ubishi usio na msingi ajui kuwa zipo solar za 30watt 24v ,32v nk hivyo hiyo hesabu yake ya kukalili itamtokea puani
Nafikiri mmenielewa vibaya,sikuwa na nia mbaya ya kumkwaza yeyote.
Ukitaka kujifunza au kujua zaidi kitu ni vizuri wakati mwingine kukubali kuwa kila kitu kina kanuni(theory) yake kabla ya kukitazama kwa upande wa Practical.
Natambua kuwa kuna watu wamefikiria kuwa nimewadharau kwa kusema ukweli.
Unapotambua kuwa wewe ni mtalaam uliyebobea inabidi uwe na uwezo wa kujua tofauti ya feki na original.
Mahesabu niliyotoa humu ni Solar Original siyo solar feki. Solar feki inabidi uipime juani na meter kama mchangiaji mmoja alivyosema.
Ikiwa nilichosema ni uongo au ujuaji naomba yeyote anayeweza kupata mahesabu sahihi ya kupata Amperes za solar kwa kukotoa,tofauti na formula niliyotumia anieleweshe.
Nitathamini mchango wa yeyote mwenye formula sahihi ya kukotoa amperes za solar tofauti na ninavyojua.