Kwa wale introverts, anti social, na shy people maisha yako ya chuo yalikuwaje? Vipi mtaani kukoje?

Aisee.. Huu uzi!

Kwanza mie nikienda kwa mtu yani mpaka naondoka naona kama kuna vitu nmeboronga kwa muda nlikuwa hapo.

Mpaka sasa hivi sijui kucheza mchezo wowote wa kijamii kama draft, bao, karata, pull table, yani mie hata baiskeli tu sijui kuendesha. Yote hii sababu ya kupenda kukaa peke angu.

Aisee hakuna mtihani mgumu kama kutembelewa na mgeni unaemuheshimu. Mimi hata mtu akiniita kunipa au kuniambia kitu flani huwa napata shida sana.

Hakuna kitu naumiaga kama nmeishiwa sasa nmfuate au nimpigie mtu anipige tafu!

Mungu mwema, sehemu ninayoishi nilichaguliwa mzee wa kanisa tena katika ujana wangu huu, hii imenisaidia angalau kidogo maana mara moja moja lazima usimame mbele ya watu kuongea. Na penyewe kabla ya kwenda kuongea unapata tabu sana tena unafika alafu baadhi ya point zinapotea.

Mke wangu ni muongeaji na huwa ana nisaidia sana hata tukiwa kwenye event flani flani linapokuja suala la mimi kutake place hasa kwenye maombi yeye ndio hufanya kwa Niaba yangu.

Sent using Jamii Forums mobile app




huyo ni Mimi sasaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
juzi kati hapa nkiwa darasani.! mwalimu alipomaliza kufundisha akanisemesha,

Mbaga Jr, em ongea kitu usikae nyuma nyuma kama mata*ko.

aise kuwa introvent nafurahia sana ila hizi changamoto hua zinaniumiza sana.
 
Mimi ni introvert na najivunia kuwa hivyo.

Being an introvert doesn't mean that you'll be antisocial or stressed.

Changamoto ambazo tunazipata sisi introvert ni kwenye mahusiano na watu.
Hatupendi kukaa na watu

-Hatupendi story za kipuuzi,kama udaku na kusema watu,tunataka story zenye facts.

-Hatuna marafiki.

-Kama tukitaka kwenda club tunaenda club tunaenda wenyewe na hatuchezi mziki tunasikiliza tu.

-Mtu akija kukutembelea unatamani aondoke,sio kwamba humpendi basi tu unakuwa hupo comfortable.

-Hupendi kupokea simu,simu ikiita unaiangalia , halafu unamtext muhusika

-Unapenda sana text kuliko calls

-Muda mwingi upo kichwani mwako
Yaaap mkali
 
Hili la kuto kuomba misaada ni kweli fursa nyingi sana zimenipita kwa sababu ya kutokuomba msaada napambana mwenyewe tu, nikitaka kuomba msaada najifikiria sana huyu mtu ninaye muomba msaada atanifikiriaje?

Wakati wa kwenda kununua Nguo au vitu vyovyote napenda vile ambavyo vinatangazwa bei kabisa nafika pale nachagua natoa hela naondoka sipendi ile negotiations na muuzaji mnaanza kubembelezana

Sent using Jamii Forums mobile app
,mambo ya kupunguza bei

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mm nashindwa pia unless ni shida kubwa thn sina alternative nyingine ya kufanya .
Hili la kuto kuomba misaada ni kweli fursa nyingi sana zimenipita kwa sababu ya kutokuomba msaada napambana mwenyewe tu, nikitaka kuomba msaada najifikiria sana huyu mtu ninaye muomba msaada atanifikiriaje?

Wakati wa kwenda kununua Nguo au vitu vyovyote napenda vile ambavyo vinatangazwa bei kabisa nafika pale nachagua natoa hela naondoka sipendi ile negotiations na muuzaji mnaanza kubembelezana

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Braza wewe ni Mimi kila kitu, mpaka nikahisi uenda ni rafki angu ananiongelea
Tabia zangu
1. Kuna mahali tulikuwa tunakaa karibu na njia so nikiwa nje nafanya shughuli nikamuona mtu anakuja, naingia ndani kumpisha apite ili tu tusisalimiane.
2.Kama kuna mahali nitataka kwenda na kuna uwezekano wa usiku ni bora nisubiri tu giza liingie ndio niende kuliko mchana huwa naona kama dunia yote inanitazama nikitoka mchana.
3.Njia ninayoiendea siyo nitakayorudi nayo kama ziko nyingi.
4. Sipendi kwenda Saloon moja hiyohiyo nipo radhi nitumie hata saa moja kwenda sehemu nyingine nikishahisi nimeanza kuzoeleka, hii nimeona hata kwenye maduka haya ya mangi hata sokoni siwezi kurudia kuwa mteja wa mtu mmoja tena na tena.
5.Huwa sipendi kufahamika, hata mtaani kwetu ningeweza natamani wasiwe wananiona naingia geti gani
6. Sipendi nguo za rangi kali maana nahisi kuwa attract watu waniangalie
7.Kama ni gari napenda kwa zaidi liwe tinted
8.Sipendi wageni wakija najifungia chumbani hii ilinipa wakati mgumu sana ndoani, nikijilazimisha naumwa kichwa kwa stress maana nakuwa sipo nao, na mwenzangu hakuwa ananielewa hata kidogo
9. Sipendi kwenda kwa watu
Mengine ni kama ya hao we zangu hapo juu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kukaa sehemu ya watu wengi huwa inanipa tabu sana... unageuka new face huku new face argh huwa najikuta nimechukia tuu.

Simu I talk to my friends few in number, my family hapa nitaongea hata asubuhi au yule mtu najua kabisa atakuwa na issue ya msingi na yeye ni wa msingi but wale watu sijawazoea unakuta ananipigia simu najiuliza tutaongea nini sasa hadi simu inakata.

Naweza kaa mwenyewe hata mwezi bila shida na sioni tabu wala, tena nakuwa na enjoy mno, I cook my favorite food nakula safii tuu.

I visit ndugu ambao nimewazoa tuu, kuna njia napita naanza kwa mamkubwa then nifike kwa bibi, huwa nisipo mkuta kakaa nje napita kama upepo.

Sijawahi hudhuria harusi ya rafiki zangu hata moja huwa na changa, natafuta na nguo viatu ikifika muda wa kwenda sasa naanza kujipa muda ngoja ifike saa 3 hapo, saa 3 ikifika nasema ngoja waanze anze huko nikifika nisikae sana unakuta mpaka nafikia maamuzi siendi muda umeenda.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sisi wenginw tuna tabia hizi kwa sababu tu tumekulia katika mazungira (socialization) ambayo ni ya kiupweke na hivyo hatuna namna. Apart from tabia za kutokupenda kuwa karibu na watu wengi, kuwa na a very limited friendship (mm nna rafiki mmoja tuu kwa zaidi ya miaka 10 now), wengine ni kama tunafahamiana tuu. Mimi mara nyingi sipendi kuongea sana na simu, pia sipendi kupigiwa pigiwa na namba mpya, napenda zaidi texting. Kimahusiano tunapataga wakati mgumu sana, unakuta mwezio anapenda kujichanganya na kukaribisha wageni home sasa mimi huwa mda mwingine nabaki chumbani hadi wageni waondoke, I just dont want to stay and talk to them, nikijitahidi nitaenda kusalimia na kusema nipo bize kidogo halafu ntarudi chumbai hata kucheki muvi tuu. Napenda zaidi kuspend time with my son, with him we can talk and play a bit of footbal although ni mdogo miaka mi3 kasoro.

Siwapendi watu wanaoongea sana ama kujisifu hao hatuwezi kukaa wote hata dakika 5. I dont know who I am, nadhani my son ndo ataniambia km nilitakiwa kuwa nani coz yeye anapata malezi ya wazazi wote wawili and tunafanana sura na huenda tabia tutafanana ili nijijue baadae. Mind you, I also love listening to music alone.
 

Eti ngoja ifike saa3,ikifika unaukata
Kukaa sehemu ya watu wengi huwa inanipa tabu sana... unageuka new face huku new face argh huwa najikuta nimechukia tuu.

Simu I talk to my friends few in number, my family hapa nitaongea hata asubuhi au yule mtu najua kabisa atakuwa na issue ya msingi na yeye ni wa msingi but wale watu sijawazoea unakuta ananipigia simu najiuliza tutaongea nini sasa hadi simu inakata.

Naweza kaa mwenyewe hata mwezi bila shida na sioni tabu wala, tena nakuwa na enjoy mno, I cook my favorite food nakula safii tuu.

I visit ndugu ambao nimewazoa tuu, kuna njia napita naanza kwa mamkubwa then nifike kwa bibi, huwa nisipo mkuta kakaa nje napita kama upepo.

Sijawahi hudhuria harusi ya rafiki zangu hata moja huwa na changa, natafuta na nguo viatu ikifika muda wa kwenda sasa naanza kujipa muda ngoja ifike saa 3 hapo, saa 3 ikifika nasema ngoja waanze anze huko nikifika nisikae sana unakuata mpaka nafikia maamizi siendi muda umeenda.



Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom