Baada ya miaka20 ndo wanashtuka!daaaa hawa watu ni hatari sana!
Uzalendo na Uongozi bora unategemea na sera za mtawala. Mkwere aliutafuta Ukuu kwa udi na uvumba, alipoona wenye busara wamemkataa, akatumia wenye mali, unajua kilichofuata.....
Ben hakuutaka kabisaa ukuu, wenye utimamu wa akili wakamuweka Ukuuni, akanogewa...akajiunga na wenye mali, kilichofuata unakijua....
Sasa kama hivyo ndivyo, hata uwe na dhamira ya kiuungu ndani ya kundi la wadanganyika, ilimradi mwenye enzi hataki, basi HAIWEZEKANI. Wenye akiki wataiona dhamira yako na watajua umefungwa mikono na mdomo, wengi watakwambia, mbona hukung'atuka???
Si kwamba uking'atuka wananchi wataunga mkono na pengine watawala watawajibishwa, Hasha! Utakaa pembeni, na yale yale yataendelea.
Kwahiyo, kama dhamira ni ya dhati, kuna ulazima wa kupambana ukiwa ndani.