Kwa ujenzi huu wa stendi Kahama

Kwa ujenzi huu wa stendi Kahama

Aliyefika stendi ya Kigoma nafikiri atakuja kuwaeleza jinsi stendi hiyo ilivyojenga kistadi
Huo ni mkoa wa pembezoni na kwa eneo la stendi hiyo linawatosha. Mahitaji yaki pile up kama ilivyo morogoro utarudi humu umejaa povu kwa malalamiko
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Huyo ni msukuma hawana "r"
Wengine hawana "l" wana "r" eg wakurya.
Wengine hawana "s" wana "th" eg wapare.
Wengine hawana "m" wana "n" eg wamakonde
Wengine hawana "ng' " wana "ng" eg wahaya
Wengine hawana "dh" wana "za" eg wanyamwezi
Wengine hwana "k" wana "ky" eg wanyakusa.

Na kazalika. Hiyo ndiyo Tanzania. Taifa kubwa pekee duniani lenye makabila 123 lakini halina ukabila.
 
Yeah, wasukuma
Hapana. Kahama ni wanyamwezi, siyo wasukuma. Hakuna kabila linaloitwa wasukuma. Kwenye hii jamii ambayo ni complex yenye lugha inayofanana lakini yenye tofauti ndogondogo kutegemea na eneo, ambayo ina watu takribani million 20 kati ya jumla ya watanzania milioni 50 kwa sasa:

Msukuma ni yule ambaye yuko kasikazini kwako. Yule ambaye yuko kusini kwako unamwita Mdakama, yule aliye mashariki yako unamwita Mnakiyaa na yule aliye magharibi yako unamwita Mnangw'eli. Maana ya neno sukuma ni kasikazini, dakama ni kusini, kiyaa ni mashariki na ngw'eli ni magharibi. Majina haya yanatumika tu kwa watu ambao lugha inafanana fanana. Huwezi kwa mfano kumwita Mtende aka Mkurya mnakiyaa hata kama yuko mashariki yako kwani lugha yake ni tofauti kabisa, au Mkerwe umwite msukuma kwa sababu tu yuko kasikazini kwako hususani wewe ni wa Mwanza kwani lugha yake ni tofauti kabisa.

Kabla ya ujio wa ukoloni, jamii hii ilikuwa inatawaliwa na himaya za kitemi. Himaya ya kitemi ya Mirambo (ya unyanyembe) ilijumulisha wilaya ya Kahama (ambayo wakati ule ilijumulisha pia wilaya za Bukombe, Ushetu na Mbogwe kwa sasa), Nzega na wilaya zote za mkoa wa Tabora kwa sasa. Watu wa utemi huu walianza kufanya safari za exploration kama zile walizokuwa wanafanya akina Vasco Dagama. Waliweza kufika hadi pwani ya Msimbazi (kwa sasa inaitwa Dar es Salaam) kwa kabila la Wazaramo. Na kutoka hapo waliweza kufika hadi visiwa vya Pemba na Uunguja. Hiyo ilikuwa ni kwenye karne ya 16 hadi 17! Walisafiri kwa mguu. Safari hadi Msimbazi iliwachukuwa miezi 3 wakitumia njia ambayo wajerumani walikuja kujenga reli ya kati.

Maeneo waliyopita walikutana na jamii za watu waliongea lugha tofauti na za kwao. Ili kuwezesha safari zao ilibidi kufanya urafiki na watu hao na kuwafanya watani zao. Waliwapa majina ambayo sasa ndiyo yanatumika kama majina ya makabila yao. Kutoka Igunga walikutana na jamii waliyoiita Balamba (Waramba), neno ambalo maana yake sitaisema. Baada ya hapo wakakutana na jamii ambayo inapenda sana kulala njiani kama magogo. Wakawaita Wagogo. Kutoka pale wakakuta jamii ambayo ni waongeaji sana lakini wanachoongea wala hakieleweki kabisa. Wakawaita Walugulu. Hatimaye wakafika pwani, wakakuta jamii ya tujitu tufupi lakini twenye uwezo wa kuzamia majini na kusafiri hadi visiwa vya Pemba na Unguja vikitumia ngalawa. Vijitu hivi wakaviita Vizaramo. Wakavifanya urafiki ili viwafundishe kuzamia kwenye hiyo bahari. Vizaramo vikawauliza "Nyie mnatokea wapi haswa?". Wakajibu " Mbali Kuleee!!! Unyanyembe" wakisota magharibi. Vizaramo vikauliza, "Kule ambako mwezi huwa unatoka?". Wakajibu "Ndiyo". Basi kuanzia hapo Vizaramo vile vikawa vinawaita watu hawa Wanyamwezi badala ya wanyanyembe -- yaani kumbe hawa jamaa ndiyo hunya ule mwezi unaotokeaga kule.

Hivyo hakuna kabila la wasukuma. Kuna wanyanyembe, wanyamwezi, wanyantuzu, wagika, wanunguli, babeshi na kadhalika kwenye jamii hii ya thelutthi moja ya watanzania iliyoenea kila sehemu ya nchi ambayo kwa siku za karibuni mmeanza kuiita kabila.
 
Bora hata hizo, kule kwetu Songea wamejenga stand mpyaa dah inasikitisha stand kama soko wamejaza maframe ya biashara tuu..hata raman haieleweki...hiyo ya Korogwe nimeipenda
 
  • Thanks
Reactions: PNC

Attachments

  • IMG_20170605_202057_248.jpg
    IMG_20170605_202057_248.jpg
    11.1 KB · Views: 68
  • IMG_20171001_131225_330.jpg
    IMG_20171001_131225_330.jpg
    44.3 KB · Views: 68
Stendi ya ovyo kuliko zote Tanzania ni ya Mwanza nyegezi ambayo ndiyo stand kuu ya ya Mwanza. Pale pesa ilitafunwa ile mbaya na wajanja.
 

Attachments

  • msamvu (1).jpg
    msamvu (1).jpg
    52.7 KB · Views: 212
  • msamvu (1).jpg
    msamvu (1).jpg
    52.7 KB · Views: 68
  • MSAMVU2.jpg
    MSAMVU2.jpg
    15 KB · Views: 66
  • MSAMVU4.jpg
    MSAMVU4.jpg
    42.6 KB · Views: 65
Kahama Mji wenye pesa mingi mingi pale waweke tu kila kitu kinachowezekana
 
Kama ujenzi utakwenda kama ulivyo kwa stendi Kahama nafikiri ndio itakuwa stendi bola zilizowahi kujengwa hapa Tanzania
50525183ce4d0bedd61b3eaa7bd5d53a.jpg

03ac6712c5295db38777ad45c9dc5958.jpg

Vp mkuu ujenzi ushaanza?...kama bado siku wakianza ulete uzi mwingine nina site yangu hapo inatazamana na hilo eneo watalojenga hiyo stand
 
Back
Top Bottom