Kwa uchafu unaoendelea nchi nzima ni vema Waziri wa Tamisemi akajiuzulu au atimuliwe

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,703
218,238
Huu ujinga unaotendwa na watendaji wa vijiji na kata nchi nzima wa kuhakikisha fomu za wagombea wa upinzani hazipokelewi kwa udi na uvumba, haujawahi kuwepo kwa kiwango kama hiki tangu nipate akili, sijawahi kuona serikali ya ccm isiyojiamini kama hii tangu nchi hii iachwe na wakoloni, ni aibu kubwa sana.

CCM imeishiwa pumzi kabisa ! bila watendaji hakuna kitu.

Natoa wito kwa Waziri Jaffo kujiuzulu mara moja kwa vile ameshindwa kusimamia mchakato wa haki wa uchaguzi wa serikali za mitaa, fomu za wagombea zinachanwa, zinakataliwa, wengine wanakimbiwa na watendaji hadi kufikia baadhi ya watendaji kuvunjika miguu baada ya kuanguka kwenye korongo, huku Waziri akinyamaza tu.

Aibu iliyoletwa awamu hii haijawahi kuletwa kwenye nchi hii tangu mfumo wa vyama vingi uanze.
 
Mngekuwa ni watu wa kupongeza pale mazuri yanapofanyika bila shaka hata malalamiko yenu yangesikilizwa. Ila sasa hivi mnaonekana vituko tu kwa sababu hakuna jambo mmewahi kupongeza.
 
Wacha mkome na mkomae muliambiwa mnapoteza muda kujiandikisha mkawa wabishi..!
 
Hamna mtu wa kujiuzulu hapa Tanzania kwa kuwa wanajua Watanzania ni makondoo. Lakini Watanzania mkiamua mnaweza!! Kwani huko Tunisia Arab Spring ilianzaje? Ilianza kwa kijana Mohamed Bouaziz aliyemaliza Chuo Kikuu, akakosa kazi na akaamua kufanya biashara ya kimachinga.

Alijichoma kwa moto baada ya Askari wa Jiji kuvunja biashara yake na picha zikachukuliwa na zikaingia kwenye mitandao ya jamii, wakawasiliana na wakalianzisha. Waliposema wanaingia mtaani hakukuwa na Polisi wala Jeshi la kuwazuia mpaka Rais Ben Ali akakimbia nchi.

Eti watu wanasema tuogope vurugu tusikae kama Somalia au Burundi, sasa faida ya amani iko wapi kama haki za kikatiba na demokrasi zinakanyagwa na Meko. Meko hataki hata kuhojiwa na Bunge.

Nchi zenye mabadiliko zilifanikiwa siyo kwa maamuzi ya watu wote bali ni kwa wachache waliojitolea kuleta mabadiliko.
 
Back
Top Bottom